Author Archives: Dr. Makirita Amani

About Dr. Makirita Amani

Dr. Makirita Amani ni daktari wa binadamu, mwandishi, mhamasishaji na mjasiriamali. Dhumuni lake kubwa kwenye maisha ni KUWASAIDA WATU KUBORESHA MAISHA YAO NA KUFIKIA MAFANIKIO MAKUBWA KUPITIA KAZI ANAZOFANYA. Mawasiliano 0717396253 email makirita@kisimachamaarifa.co.tz

2510; Kwa nini hubadiliki?

By | November 14, 2021

2510; Kwa nini hubadiliki? Kuna nukuu moja maarufu sana inayosema; miaka mitano ijayo utakuwa mtu yule yule uliye sasa isipokuwa kwa watu utakaokutana nao na vitabu utakavyosoma. Ni kauli rahisi lakini yenye funzo na maana kubwa sana. Kwamba mafanikio yetu kwenye maisha yanatokana na mabadiliko yanayotokea kwenye maisha yetu. Mabadiliko (more…)

#SheriaYaLeo (14/366); Epuka Njia Ya Uongo.

By | November 14, 2021

#SheriaYaLeo (14/366); Epuka Njia Ya Uongo. Njia ya uongo ni ile ambayo inatuvutia kwa sababu zisizo sahihi – fedha, umaarufu, kuwaridhisha wengine na kadhalika. Sababu hizo zinakusukuma kufanya kitu ambacho siyo sahihi kwako, ambacho kinakuzuia usiishi kusudi na wajibu wako. Kama unafanya kwa ajili ya umaarufu, unaishia kuona utupu ulio (more…)

2509; Kwa nini hupendi unachofanya?

By | November 13, 2021

2509; Kwa nini hupendi unachofanya? Kutokupenda kazi au biashara unayofanya ni kikwazo kikubwa cha mafanikio yako. Huwezi kufanikiwa kwenye kitu ambacho hukipendi, hata kama kinalipa kiasi gani. Huenda wewe ni mmoja wa wale ambao wanafanya wasichopenda, leo nataka upate jawabu hapa ili kuchukua hatua sahihi. Mahali pa kuanzia ni kujua (more…)

#SheriaYaLeo (13/366); Bobea kwenye vitu vidogo.

By | November 13, 2021

#SheriaYaLeo (13/366); Bobea kwenye vitu vidogo. Pale unapokuwa umekabiliwa na mapungufu badala ya uimara, huu ndiyo mkakati unaopaswa kufanyia kazi; puuza udhaifu wako na kataa ushawishi wa kutaka kuwa kama wengine. Badala yake weka juhudi zako zote kwenye vitu vidogo vidogo ambavyo uko vizuri katika kuvifanya. Usihangaike na mambo makubwa (more…)

2508; Kama Huna Cha Kufanya, Usifanye Chochote.

By | November 12, 2021

2508; Kama Huna Cha Kufanya, Usifanye Chochote. Kuna mambo mawili makubwa yanaendelea kwenye zama tunazoishi sasa. Moja ni kila mtu amechoka kweli kweli, haijalishi amezalisha matokeo gani. Mbili ni ubunifu na uvumbuzi umepungua sana. Yote hayo yanasababishwa na tabia ya watu kukosa muda ambao hawana kitu cha kufanya. Kwenye zama (more…)

2507; Siyo wa tofauti kama unavyodhani.

By | November 11, 2021

2507; Siyo wa tofauti kama unavyodhani. Kuna vitu ambavyo huwa vinawatokea watu wengi kwenye maisha yao kutokana na yale wanayofanya au vile walivyo. Yaani wanachopata ni matokeo ya hatua walizochukua au namna walivyo. Inakuwa imezoeleka hivyo kiasi kwamba ukimwona tu mtu anafanya kitu fulani au yulo kwa namna fulani, unajua (more…)

#SheriaYaLeo (11/366); Nini Kinakupa Shauku Zaidi?

By | November 11, 2021

#SheriaYaLeo (11/366); Nini Kinakupa Shauku Zaidi? Kila mmoja wetu kuna kitu ambacho akikifanya anajisikia vizuri zaidi na kupata msukumo wa kuendelea kukifanya kwa muda mrefu bila kuchoka. Katika kufanya kitu hicho, mtu unakuwa na nguvu kubwa na ubunifu ambao wengine wanaushangaa. Wakati kwa wengine kufanya kitu hicho ni kazi ngumu, (more…)

2506; Kitakachokutoa Njia Panda.

By | November 10, 2021

2506; Kitakachokutoa Njia Panda. Mara kwa mara huwa tunajikuta kwenye njia panda fulani katika safari yetu ya maisha. Kutokana na mambo mbalimbali yanayokuwa yanaendelea, unakuwa hujui nini hasa ufanye kati ya mengi yaliyo mbele yako. Ni katika hali hizi za njia panda ndipo wanaofanikiwa na wanaoshindwa hutofautiana. Wanaofanikiwa huwa wana (more…)

#SheriaYaLeo (10/366); Kubali na Ishi Uajabu Wako.

By | November 10, 2021

#SheriaYaLeo (10/366); Kubali na Ishi uajabu wako. Kuna namna ambavyo uko tofauti kabisa na watu wengine. Utofauti huo umewafanya watu wakuone wewe ni mtu wa ajabu. Uajabu wako huo umekuwa unawafanya baadhi ya watu wakuchukie, wakudharau, wakupinge na hata wakukosoe. Kwa sababu tunapenda sana kukubalika na wengine, huwa tunakuwa tayari (more…)