Author Archives: Dr. Makirita Amani

About Dr. Makirita Amani

Dr. Makirita Amani ni daktari wa binadamu, mwandishi, mhamasishaji na mjasiriamali. Dhumuni lake kubwa kwenye maisha ni KUWASAIDA WATU KUBORESHA MAISHA YAO NA KUFIKIA MAFANIKIO MAKUBWA KUPITIA KAZI ANAZOFANYA. Mawasiliano 0717396253 email makirita@kisimachamaarifa.co.tz

3083; Piga kelele.

By | June 10, 2023

3083; Piga kelele. Rafiki yangu mpendwa,Kwenye kitabu cha CHUO CHA MAUZO nimeandika; ustaarabu pekee kwenye biashara ni kuuza.Nimeandika hivyo kwa sababu kuna baadhi ya watu wanajiona ni wastaarabu sana hivyo kuna baadhi ya mambo hawawezi kufanya kwenye biashara.Halafu kwa bahati mbaya sana, wanakuwa hawauzi.Yaani mtu anajifanya mstaarabu, wakati hafanyi mauzo (more…)

Barua ya VI; Kushirikishana Maarifa.

By | June 9, 2023

Barua ya VI; Kushirikishana Maarifa. Rafiki yangu Mstoa,Tunaishi kwenye zama za maarifa na taarifa, ambapo nguvu kubwa ipo kwa wale wenye maarifa na taarifa sahihi na kufanyia kazi. Pamoja na maarifa na taarifa kupatikana kwa wingi kwenye zama hizi, bado wengi sana wameshindwa kuzipata na kufanyia kazi, kitu ambacho kimepelekea (more…)

3082; Siyo kupanga, ni kufanya.

By | June 9, 2023

3082; Siyo kupanga, ni kufanya. Rafiki yangu mpendwa,Kwenye safari ya mafanikio, kila mtu huwa ana mipango mizuri ya jinsi ya kufikia mafanikio anayoyataka.Lakini licha ya hilo, bado ni watu wachache sana ambao wanayapata mafanikio wanayokuwa wanayataka. Hilo linaweza kukushangaza, iweje wengi wawe na malengo na mipango ya kufanikiwa, lakini wachache (more…)

3081; Mambo yasiwe mengi.

By | June 8, 2023

3081; Mambo yasiwe mengi. Rafiki yangu mpendwa,Kwa kuwa tunataka sana kufanikiwa kwenye maisha yetu, huwa hatuoni kama sisi wenyewe tunaweza kuwa kikwazo kwenye mafanikio yetu. Lakini ukweli ni kwamba sisi wenyewe huwa tunakuwa kikwazo kwa mafanikio makubwa tunayoyataka kwa sababu ya mambo kuwa mengi. Kadiri mtu anavyokuwa na orodha ndefu (more…)

3080; Mwili na mazingira.

By | June 7, 2023

3080; Mwili na mazingira. Rafiki yangu mpendwa,Tunaweza kuona tuna mambo mengi sana ambayo tunakabiliana nayo kwenye safari yetu ya mafanikio makubwa. Lakini kiuhalisia, mambo hayo yote yamegawanyika kwenye makundi makubwa mawili; mwili na mazingira. Mapambano ya kwanza kwetu ni ya kimwili.Miili yetu ni kikwazo cha kwanza kwetu kuyafikia mafanikio makubwa (more…)

3079; Hapana sahihi kwako.

By | June 6, 2023

3079; Hapana sahihi kwako. Rafiki yangu mpendwa,Kama ambavyo tunajua, tupo kwenye msimu wa kusema HAPANA.Ni msimu wa kupeleka umakini na juhudi zote kwenye vitu vichache na kuachana na vingine vyote. Watu hudhani kusema hapana ni rahisi sana, kwa sababu vitu unavyokataa ni ambavyo huvitaki.Lakini hilo siyo sahihi.Hapana sahihi kwako ni (more…)

3078; Maji yanayoizamisha meli.

By | June 5, 2023

3078; Maji yanayoizamisha meli. Rafiki yangu mpendwa,Sote tunajua ya kwamba meli huwa inaelea kwenye maji.Pamoja na uzito wake mkubwa, meli hiyo huwa inaendelea kuelea vizuri tu.Lakini hiyo yote ni kama maji yataendelea kubaki nje ya meli.Ni pale maji yanapoingia ndani ya meli ndiyo meli inapoanza kuzama. Kumbe basi, maji yanayoizamisha (more…)

3077; Kwa nini umekubali?

By | June 4, 2023

3077; Kwa nini umekubali? Rafiki yangu mpendwa,Sisi binadamu tuna uwezo mkubwa sana wa kufanya chochote kile tunachotaka kufanya.Tunachohitaji tu ni sababu kubwa ya kwa nini tufanye kitu hicho.Tunapokuwa na sababu kubwa huwa tunaitimiza. Unapokuwa na msukumo mkubwa wa kufanya kitu, huwa unahakikisha unakifanya kweli.Na unapokosa msukumo mkubwa wa kufanya kitu, (more…)

3076; Kubadilika na kutokubadilika.

By | June 3, 2023

3076; Kubadilika na kutokubadilika. Rafiki yangu mpendwa,Hendry Ford, aliyekuwa mwanzilishi wa magari, alikuwa mtu mbishi sana kubadilika.Baada ya kuja na gari ambalo lilipendwa sana na watu, hakutaka kubadili chochote, badala yake aliendelea kuzalisha gari hilo hilo kwa muundo ule ule.Licha ya kushauriwa sana kubadilika, aliendelea kubaki kwenye kile alichoamini ndiyo (more…)

Barua ya V; Kuhusu Kuishi Kwa Falsafa Na Maisha Ya Mafanikio.

By | June 2, 2023

Barua ya V; Kuhusu Kuishi Kwa Falsafa Na Maisha Ya Mafanikio. Rafiki yangu Mstoa,Moja ya vitu vinavyofanya watu wengi wasiyafurahie maisha ni kutokuishi maisha halisi kwao.Wengi wanaishi maisha ya kuiga na kuwaridhisha wengine.Wengi sana wanaishi maisha ya maigizo kwa nje, huku ndani yao wakiwa tofauti kabisa. Tumekuwa tukiona watu ambao (more…)