Author Archives: Dr. Makirita Amani

About Dr. Makirita Amani

Dr. Makirita Amani ni daktari wa binadamu, mwandishi, mhamasishaji na mjasiriamali. Dhumuni lake kubwa kwenye maisha ni KUWASAIDA WATU KUBORESHA MAISHA YAO NA KUFIKIA MAFANIKIO MAKUBWA KUPITIA KAZI ANAZOFANYA. Mawasiliano 0717396253 email makirita@kisimachamaarifa.co.tz

2624; Kanuni ya heshima au imani.

By | March 8, 2022

2624; Kanuni ya heshima au imani. Watu wamekuwa wanalalamika kwamba hawaheshimiwi au hawaaminiwi. Lakini ukiangalia kwa uhalisia, tatizo huanzia kwa watu kutokujiheshimu au kujiamini wenyewe. Leo napendekeza kanuni rahisi ambayo ukiifuata utajijengea heshima kubwa na kuaminika na wengine. Kanuni hiyo inakwenda hivi; Heshima/imani = utekelezaji/ahadi Ili heshima au imani iwe (more…)

#SheriaYaLeo (128/366); Wanaotumia udhaifu kukutawala.

By | March 8, 2022

#SheriaYaLeo (128/366); Wanaotumia udhaifu kukutawala. Kuna watu huwa wanatumia udhaifu walionao kukutawala wewe bila ya mwenyewe kujua. Wanakuwa na tabia fulani sugu ambayo inakukwamisha wewe, lakini unapojaribu kuwakabili kwenye tabia hiyo wanajionyesha hawana hatia na wewe ni mtu mbaya na usiyejali. Wanaweza kuwa na tabia sugu ya kuchelewa kila wakati. (more…)

2623; Gharama zilipojificha.

By | March 7, 2022

2623; Gharama zilipojificha. Kipo kichekesho kinaeleza mgahawa ambao ulitumia mbinu ya masoko kuwashawishi wateja kununua kwa wingi. Mgahawa huo uliweka tangazo kwa nje likieleza; kula leo watalipa wajukuu wako. Watu walivutiwa na hilo na kuingia kuagiza chakula. Baada ya kula wahudumu waliwaletea bili. Hapo ndipo wateja wakawa wanagoma kwamba tangazo (more…)

#SheriaZaLeo (127/366); Unachoona siyo uhalisia.

By | March 7, 2022

#SheriaZaLeo (127/366); Unachoona siyo uhalisia. Watu huwa wanatumia mwonekano wa nje kuwahadaa wengine. Pale wanapokuwa na udhaifu fulani, huwa wanatengeneza mwonekano unaoficha udhaifu huo. Lengo lao ni kuwanasa wengine kwa namna ambayo wao watanufaika zaidi. Wewe kuwa makini usinase kwenye mitego huo. Jua siyo kila unachoona kwa nje ndiyo uhalisia (more…)

2622; Sababu zipo tayari.

By | March 6, 2022

2622; Sababu zipo tayari. Kama unataka kufanya kitu, au hutaki kukifanya, sababu zipo tayari. Kama utafanikiwa au utashindwa, sababu zipo tayari. Yaani sababu tayari ziko mbele yako, ni wewe tu uchague unataka nini, halafu uchukue sababu zinazoendana na kile unachotaka. Kama unataka kweli kupata kitu, sababu za kukitaka tayari unazo. (more…)

#SheriaYaLeo (126/366); Kuwa makini na watu unaowachokoza.

By | March 6, 2022

#SheriaYaLeo (126/366); Kuwa makini na watu unaowachokoza. Watu huwa wanabadilika, hakuna anayebaki pale alipoanzia. Mtu anaweza kuwa chini leo, lakini siku zijazo akawa juu kabisa. Hivyo kuwa makini sana na watu unaowachokoza, kuwadharau au kuwatukana. Leo anaweza asiwe na nguvu ya kukufanya chochote, lakini siku zijazo akawa na nguvu na (more…)

2621; Machache kuhusu wewe yanawatosha.

By | March 5, 2022

2621; Machache kuhusu wewe yanawatosha. Sisi binadamu tuna kasumba moja, kadiri tunavyokijua zaidi kitu ndivyo tunavyokichukulia kawaida na kukidharau. Lakini pale tunapokuwa hatukijui sana kitu huwa tunakiheshimu na kukichukulia kwa uzito mkubwa. Kwa kujua hili, wawekee watu mipaka ya kujua kuhusu mambo yako. Kadiri watu wanavyojua machache kuhusu maisha yako (more…)

#SheriaYaLeo (125/366); Usidanganyike na mwonekano wa nje.

By | March 5, 2022

#SheriaYaLeo (125/366); Usidanganyike na mwonekano wa nje. Mara nyingi watu wamekuwa wanatengeneza mwonekano fulani wa nje ambao unaficha nia yao halisi. Kwa nje wanaigiza kama wajinga na wasiojua vitu fulani. Lengo lao ni kuwahadaa watu ili wasijue nia zao na kuwa kikwazo kwao. Wewe kuwa makini, usikimbilie kuamini mwonekano wa (more…)

2620; Matumaini na uhakika.

By | March 4, 2022

2620; Matumaini na uhakika. Watu huona matumaini kama kitu cha kujifurahisha, ambacho siyo uhalisia. Hupenda zaidi uhakika kwenye kila jambo. Lakini ukweli ni kwamba katika hali ya kawaida, kuujua ukweli ni vigumu sana. Hivyo kujipa uhakika kabla hujaujua ukweli ni kujiweka kwenye hatari kubwa, kuwa kikwazo kwako mwenyewe kupiga hatua. (more…)

#SheriaYaLeo (124/366); Wahukumu kwa tabia zao, siyo maneno yao.

By | March 4, 2022

#SheriaYaLeo (124/366); Wahukumu kwa tabia zao, siyo maneno yao. Kwenye safari yako ya mafanikio na maisha kwa ujumla, jifunze kutokudanganyika na maneno ambayo watu wanakuambia, badala yake angalia tabia wanazokuonyesha. Watu husema maneno ya kila aina na kujaribu kuficha nia zao halisi kwa maneno mazuri. Lakini matendo yao huwa hayadanganyi, (more…)