Author Archives: Dr. Makirita Amani

About Dr. Makirita Amani

Dr. Makirita Amani ni daktari wa binadamu, mwandishi, mhamasishaji na mjasiriamali. Dhumuni lake kubwa kwenye maisha ni KUWASAIDA WATU KUBORESHA MAISHA YAO NA KUFIKIA MAFANIKIO MAKUBWA KUPITIA KAZI ANAZOFANYA. Mawasiliano 0717396253 email makirita@kisimachamaarifa.co.tz

2619; Siyo hawamudu, bali hawajali.

By | March 3, 2022

2619; Siyo hawamudu, bali hawajali. Kama unauza kitu, iwe ni bidhaa au huduma na wateja uliowapata hawapo tayari kulipia, ni rahisi kuona labda hawamudu. Utakimbilia kuona bei ndiyo kikwazo kwao, ni kubwa kwao na hivyo hawamudu. Na wanaweza kukuambia hivyo kweli. Lakini hata utakapojaribu kupunguza bei, bado hawatakuwa tayari kununua. (more…)

#SheriaYaLeo (123/366); Wakabili wanaocheza rafu.

By | March 3, 2022

#SheriaYaLeo (123/366); Wakabili wanaocheza rafu. Katika safari ya mafanikio na maisha kwa ujumla, utakutana na watu ambao wanacheza rafu. Hawa ni wale ambao wapo tayari kutumia kila namna kupata kile wanachotaka. Kwa nje watu hao hujionyesha ni wema, wastaarabu na wanaojali. Ila kwa ndani watu hao ni sumu, wenye mbinu (more…)

2618; Unayapenda mafanikio, ila hayakupendi.

By | March 2, 2022

2618; Unayapenda mafanikio, ila hayakupendi. Wakati naanza huduma hii ya mafunzo, ushauri na ukocha wa mafanikio, nilikuwa naamini kila mtu anawesa kufanikiwa. Kwamba mtu akishakuwa tu na nia ya kufanikiwa, akapata maarifa na miongozo sahihi, basi hakuna namna atashindwa kufanikiwa. Kadiri ninavyoendelea kufanya kazi kwa ukaribu kabisa na walio wengi, (more…)

#SheriaYaLeo (122/366); Kila mtu yupo kwenye mchezo.

By | March 2, 2022

#SheriaYaLeo (122/366); Kila mtu yupo kwenye mchezo. Kwenye safari ya maisha, kila mmoja yupo kwenye mchezo wa madaraka. Kuna kitu kila mtu anapigania kukipata. Iwe ni fedha, mafanikio, utajiri, madaraka, umaarufu na mengine. Lakini sasa, watu wamegawanyika katika makundi matatu. Kundi la kwanza ni wanaojifanya hawapo kwenye mchezo. Hapa kuna (more…)

2617; Kwenye uzio.

By | March 1, 2022

2617; Kwenye uzio. Huingii ndani na wala hutoki nje. Hiyo ni hali ambayo wengi wamekuwa wakijikuta hasa wanapohitajika kufanya maamuzi. Na hilo ndiyo limekuwa linafanya wengi wasubiri mpaka tarehe ya mwisho (deadline) ndiyo wafanye kitu. Kukaa kwenye uzio hakujawahi kuwa na manufaa, zaidi ya kumpotezea muda. Utaona unapata muda zaidi (more…)

#SheriaYaLeo (121/366); Usionekane mkamilifu sana.

By | March 1, 2022

#SheriaYaLeo (121/366); Usionekane mkamilifu sana. Unapokuwa kwenye eneo au kundi ambalo unashirikiana na wengine ili uweze kupata mafanikio unayoyataka, kuonekana mkamilifu sana ni kikwazo kikubwa kwako. Kadiri unavyoonyesha uwezo wako mkubwa na usivyokuwa na mapungufu, ndivyo wengi wanavyojenga wivu na chuki juu yako. Unaweza kudhani kuonyesha uwezo na ukamilifu wako (more…)

ONGEA NA KOCHA; Instant Cashflow Sehemu Ya Pili.

By | February 28, 2022

Habari Mwanamafanikio? Karibu kwenye kipindi cha ONGEA NA KOCHA ambapo tunapata uchambuzi wa kitabu cha INSTANT CASHFLOW sehemu ya pili. Kwenye sehemu hii ya pili tunaangalia maeneo mawili kati ya matano ya kukuza biashara. Eneo la kwanza ni kutengeneza wateja tarajiwa kupitia masoko. Hapa tunaziangalia njia mbalimbali za masoko unazoweza (more…)

2616; Ni rahisi kwa wengine.

By | February 28, 2022

2616; Ni rahisi kwa wengine. Ukiwa unaona watu wengine wanafanya vitu, unaweza kuona ni rahisi. Ni mpaka pale unapoingia mwenyewe kufanya ndiyo unajua ni vigumu kiasi gani kufanya. Unapoona mwingine anakwama kufanya maamuzi au kuchukua hatua fulani unaweza kuona ni rahisi na wanajiendekeza, lakini unapokuwa kwenye nafasi hiyo unaona ilivyo (more…)

#SheriaYaLeo (120/366); Usitabirike.

By | February 28, 2022

#SheriaYaLeo (120/366); Usitabirike. Watu huwa wanajaribu kusoma sababu iliyo nyuma ya kila hatua unayochukua. Ukiwa mtu wa kuchukua hatua kwa namna fulani na sababu zinazoeleweka, unatabirika kirahisi. Na watu wakishaweza kukutabiri, wanakutawala kirahisi. Sisi binadamu ni viumbe wa kitabia, huwa tunafanya yale tuliyozoea kufanya na hilo linapelekea tutabirike kirahisi. Mara (more…)