Author Archives: Dr. Makirita Amani

About Dr. Makirita Amani

Dr. Makirita Amani ni daktari wa binadamu, mwandishi, mhamasishaji na mjasiriamali. Dhumuni lake kubwa kwenye maisha ni KUWASAIDA WATU KUBORESHA MAISHA YAO NA KUFIKIA MAFANIKIO MAKUBWA KUPITIA KAZI ANAZOFANYA. Mawasiliano 0717396253 email makirita@kisimachamaarifa.co.tz

2629; Hawataki ushauri wako.

By | March 13, 2022

2629; Hawataki ushauri wako. Nimewahi kuandika mara kadhaa kuhusu ushauri wa bure. Nikisisitiza usimpe mtu ushauri kama hajakuomba na usipokee ushauri kwa mtu kama hujamuomba akushauri. Pia nikaeleza jinsi ushauri wa bure ulivyo na gharama pale unapoufanyia kazi, kwa sababu unakuwa haujatolewa kulingana na uhitaji uliopo. Leo nakwenda kukupa sababu (more…)

#SheriaYaLeo (133/366); Kuwa makini na wema unaoonyeshwa.

By | March 13, 2022

#SheriaYaLeo (133/366); Kuwa makini na wema unaoonyeshwa. Mara nyingi watu hukazana kuonyesha wema fulani kwa nje ili waonekane wanafanya kwa manufaa ya wengine. Lakini ndani yao wanakuwa wameficha sababu halisi ambayo ni kujinufaisha wao wenyewe zaidi. Kuwa makini sana na wema unaoonyeshwa kwa nguvu kubwa, kwa sababu unakuwa umeficha ulaghai (more…)

2628; Ndiyo biashara yenyewe.

By | March 12, 2022

2628; Ndiyo biashara yenyewe. Sisi binadamu huwa tunafanya vitu kwa misukumo ya hisia mbili; tamaa na hofu. Huwa tunafanya kitu kama kuna kitu kizuri tunapata (tamaa) au kama hatutaki kupoteza tulichonacho (hofu). Kwa kujua hili, inakusaidia sana kuelewa kwa nini baadhi ya watu huwa wanafanya vitu ambavyo hukutegemea wafanye. Unaweza (more…)

#SheriaYaLeo (132/366); Angalia tabia wanazoficha.

By | March 12, 2022

#SheriaYaLeo (132/366); Angalia tabia wanazoficha. Katika kuchagua watu wa kushirikiana nao, huwa tunaamini haraka kile ambacho tunasikia na kuona kwao. Tunaamini hivyo ndivyo watu walivyo na yale wanayotuambia na kutuonyesha ndiyo uhalisia wao. Tunachosahau ni kila mtu kuna tabia anazo ambazo huwa hapendi kuziweka wazi. Huenda hata yeye mwenyewe hajui (more…)

#SheriaYaLeo (131/366); Usichanganye kujiamini kulikopitiliza na ukweli.

By | March 11, 2022

#SheriaYaLeo (131/366); Usichanganye kujiamini kulikopitiliza na ukweli. Sisi binadamu huwa tunadanganyika kirahisi sana. Pale mtu anapotueleza kitu kwa kujiamini sana, huwa tunaona ni ukweli, kwamba kama isingekuwa kweli basi wasingejiamini. Hii ndiyo njia wanayotumia matapeli na watu wengine wenye lengo la kudanganya na kuhadaa kwa manufaa yao. Huwa wanaeleza jambo (more…)

#SheriaYaLeo (130/366); Tambua mlipuko wa kihisia.

By | March 10, 2022

#SheriaYaLeo (130/366); Tambua mlipuko wa kihisia. Pale mtu anapopata mlipuko mkali wa kihisia dhidi yako, mfano hasira ambayo haiendani na kile ulichofanya, tambua ni mbinu ya kutaka kukutawala kihisia. Wapo watu ambao hutumia mlipuko wa hisia kuibua hisia kali ndani yako ili waweze kukutawala. Wanajua ukishakuwa na hisia kali, huwezi (more…)

2625; Usife.

By | March 9, 2022

2625; Usife. Katika safari ya mafanikio ya mtu yeyote yule, bahati ina mchango wake. Kila historia ya aliyefanikiwa, kuna mahali alikutana na bahati au fursa ya kipekee na ikampa manufaa makubwa. Kinachowatofautisha wanaokutana na bahati na ambao hawakutani nazo siyo bahati yenyewe, bali muda. Yaani siyo kwamba kuna watu wana (more…)

#SheriaYaLeo (129/366); Angalia mapito yao.

By | March 9, 2022

#SheriaYaLeo (129/366); Angalia mapito yao. Kiashiria kizuri cha tabia za watu ni mapito yao. Kwa kuangalia historia zao na yale ambayo wamefanya huko nyuma, unaweza kupata picha ni watu wa aina gani. Watu wanaweza kusema wamejifunza na kubadilika kutokana na yale waliyopitia, lakini siyo rahisi hivyo. Kuna tabia huwa zinaendelea (more…)