Category Archives: KURASA ZA MAISHA

Kila siku mpya kwenye maisha yako ni sawa na ukurasa mpya wa kitabu.
Kwa kila siku mpya unachagua ufanye nini na maisha yako.
Kupitia makala hizi za KURASA ZA MAISHA, utajifunza mambo muhimu ya kufanya ili uwe namaisha bora zaidi.
Makala hizi za kurasa zinakujia kila siku.

2210; Kila Mtu Anaishi Kwa Matumaini…

By | January 18, 2021

Wakati vifo vya ugonjwa wa Ukimwi vilipokuwa vinapamba moto, kipindi ambacho dawa za kupunguza makali ya virusi hivyo zilikuwa hazipatikani kwa urahisi na kwa wote wenye maambukizi, mtu aliyepata maambukizi aliitwa anaishi kwa matumaini. Ni kama vile mtu akishapata virusi hivyo basi ana tiketi ya uhakika ya kifo na hivyo (more…)

2209; Ingia Na Ukae Kwenye Mstari…

By | January 17, 2021

Nakumbuka sherehe za zamani ambapo watu walikuwa wanapakuliwa na kupelekewa chakula pale walipokaa. Haikujalisha unapenda au hupendi nini, chakula kilipakuliwa sawa kwa wote na kisha kusambazwa kuwapelekea walipo. Lakini sherehe za siku hizi zimebadilika kabisa, hakuna tena wa kukupakulia chakula na kukuletea ulipo, bali unapaswa kwenda eneo la chakula na (more…)

2208; Jehanamu Unaishi Nayo…

By | January 16, 2021

Watu wengi wamekuwa hawaielewi vizuri dhana ya jehanamu. Wanachoelewa ni kwamba kama utafanya uovu au dhambi, utakapofika mwisho wa dunia basi utahukumiwa kwenda jehanamu na kuteseka milele. Mateso ya huko yameelezewa kuwa mengi na makali, ikiwepo kuchomwa moto. Dhana ya jehanamu ni adhabu ambayo mtu unaipata pale unapokuwa umefanya uovu (more…)

2207; Hujateleza, Ndiyo Uhalisia Wako…

By | January 15, 2021

Viumbe hai wengine wote ukiacha binadamu, huwa wanazaliwa wakiwa tayari wana njia ya kuyaendesha maisha yao. Wanakuwa tayari kukabiliana na mazingira yao pale wanapokuwa wamezaliwa na wanayaendesha hivyo maisha yao. Binadamu ndiye kiumbe hai pekee anayezaliwa akiwa hana maandalizi kamili ya kukabiliana na maisha yake, ndiyo maana anachukua muda mrefu (more…)

2206; Mambo Muhimu Kujikumbusha Kuhusu Fedha…

By | January 14, 2021

Nimekuwa naandika mara nyingi kuhusu fedha na hapa nimekusanya yale muhimu unayopaswa kuyajua kila wakati kuhusu fedha. Siyo mapya, ila ni ya kujisisitizia uyaelewe kwa undani. Ongeza kipato chako, kila wakati pambana kukiongeza. Dhibiti matumizi yako, yasikue kuzidi kipato. Kuwa na akiba ya dharura angalau miezi 6 mpaka 12 ya (more…)

2205; Njia Sahihi Ya Kuzitumia Hisia…

By | January 13, 2021

Matatizo mengi tunayokutana nayo kwenye maisha, kwetu wenyewe na kwa wengine huwa yanaanzia kwenye hisia. Tunafanya maamuzi fulani kwa kusukumwa na hisia na baadaye tunagundua hayakuwa maamuzi sahihi kitu kinachofanya tuingie kwenye matatizo. Tunaweza kuzichukia hisia, lakini bila ya hizo, hatuwezi kufanya maamuzi yoyote, tunaweza kufikiri tutakavyo, lakini ili kufanya (more…)

2204; Wasaidie Wengine Kushinda…

By | January 12, 2021

Kama unataka ushindi kwenye maisha, basi wasaidie wengine kushinda. Kwa wengine kushinda, watakufanya na wewe upate ushindi pia, tena ushindi ambao utadumu. Kwa chochote unachofanya, angalia ni kwa namna gani wengine wananufaika kwanza kabla hujaangalia wewe unanufaikaje. Weka maslahi ya wengine mbele kama unavyoweka yao, lakini anza kwa kuangalia maslahi (more…)

2203; Fanya Chochote Ili Kujua Cha Kufanya…

By | January 11, 2021

Kanuni za kisayansi, hasa kanuni za fizikia, ni kanuni ambazo zinatokana na asili. Hiyo ina maana kwamba kanuni hizo zinafanya kazi kila mahali na kwa kila hali. Moja ya kanuni hizo ni kuhusu mwendo, ambayo inasema kitu kilichosimama kitaendelea kusimama na kilicho kwenye mwendo kitaendelea na mwendo mpaka nguvu ya (more…)

2202; Umaarufu Feki Na Halisi…

By | January 10, 2021

Watu wengi wanapenda umaarufu, ila huwa hawajali ni umaarufu wa aina gani, una manufaa gani na changamoto zipi zinakuja na umaarufu. Umaarufu tunaweza kuugawa kwenye makundi mawili, feki na halisi. Umaarufu halisi ni ule unaotokana na ubobezi ambao mtu amefikia katika kile anachofanya, na ambacho kina manufaa makubwa kwa wengine. (more…)