Category Archives: KURASA ZA MAISHA

Kila siku mpya kwenye maisha yako ni sawa na ukurasa mpya wa kitabu.
Kwa kila siku mpya unachagua ufanye nini na maisha yako.
Kupitia makala hizi za KURASA ZA MAISHA, utajifunza mambo muhimu ya kufanya ili uwe namaisha bora zaidi.
Makala hizi za kurasa zinakujia kila siku.

2199; Aina Mbili Za Ushauri…

By | January 7, 2021

Kuna aina mbili za ushauri, unazopaswa kuzijua na jinsi unavyoweza kutumia kwenye kile unachopitia. Aina ya kwanza ni ushauri wa wazi, huu ni ule ushauri unaotolewa kwa wazi na unaoweza kumlenga kila mtu. Mfano unaposoma makala yenye ushauri kuhusu biashara, kazi au fedha, inaweza kuwa na mambo mazuri, lakini mengi (more…)

2198; Unachopaswa Kujua Unapoamua Kuyaishi Maisha Yako…

By | January 6, 2021

Asilimia zaidi ya 90 ya watu kwenye jamii hawaishi maisha yao. Badala yake wanaishi maisha ya maigizo, maisha ya kufuata mkumbo. Wengi wanaishi maisha ya kufanya kile kinachofanywa na wengine. Kuishi hivyo ni rahisi, hakuna atakayekusumbua, kwa sababu unafikiri, kusema na kufanya kama wengine wanavyokubali. Lakini ukichagua kuyaishi maisha yako, (more…)

2197; Mabishano Yasiyo Na Mwisho…

By | January 5, 2021

Mijadala inayohusu dini, siasa, michezo na mapenzi, huwa haina mwisho au watu kufikia muafaka. Hiyo ni kwa sababu watu huingia kwenye mijadala hiyo wakiwa tayari wana upande, na upande waliopo umebeba sehemu ya utu na maisha yao. Mtu anapoingia kwenye mjadala au mabishano yanayohusu dini, tayari anakuwa upande fulani wa (more…)

2196; Njia Bora Ya Kuuza…

By | January 4, 2021

Tasnia ya mauzo imekuwa inachukuliwa kama isiyo ya uaminifu, ambapo wauzaji hutumia kila mbinu kumshawishi mtu kununua kitu ambacho hakihitaji. Ni kweli kuna wauzaji wengi wenye mtazamo huo, ambao kwao wanachojali ni kuuza na kupata fedha, bila kujali anayenunua kitu hicho kina manufaa kwao au la. Wauzaji hawa huwa wanajisifia (more…)

2195; Fanya Kwa Muda Mfupi…

By | January 3, 2021

Kuna majukumu ambayo unapenda kuyafanya, ambayo upo tayari kuyafanya kwa muda mrefu iwezekanavyo, haya siyo shinda kwako kama ni majukumu muhimu. Ila kuna majukumu ambayo hupendi kuyafanya kabisa, kila ukifikiria kuyafanya unajikuta ukiahirisha na kupanga kufanya mambo mengine. Tatizo la majukumu haya yanakuwa ni muhimu sana, kiasi kwamba usipoyafanya basi (more…)

2194; Utakapokuwa Unavuta Pumzi Yako Ya Mwisho…

By | January 2, 2021

Siku utakayokuwa unavuta pumzi yako ya mwisho hapa duniani, kuna mambo utajivunia kwa kuyafanya na kuna mambo utajutia kuyafanya. Hiki ni kitu ambacho wengi huwa hawakifikirii mapema, lakini wanapofika ukingo wa maisha yao ndiyo wanapata nafasi ya kuyatafakari maisha yao, huku wakiwa hawana cha kubadili. Lengo lako kwenye maisha ni (more…)

2193; Kuacha Alama Duniani…

By | January 1, 2021

Watu wote ambao wamewahi kupita hapa duniani na mpaka leo bado tunawakumbuka wana sifa moja. Kuna wakati walipinga kile ambacho kila mtu aliamini na kuja na ambacho ni sahihi. Wakati wanafanya hivyo haikuwa rahisi kwao, walikutana na ugumu, walikatishwa tamaa na hata kuhujumiwa, wapo ambao walifungwa na wengine kuuawa. Lakini (more…)

2192; Kutokufanya Ambacho Hutaki Kufanya…

By | December 31, 2020

Huo unaweza kuwa uhuru wa juu kabisa kwenye maisha yako. Uhuru huu huwa hautokei tu, bali unatengenezwa. Na njia kuu ya kuutengeneza ni kufikia uhuru wa kifedha kwanza. Iko hivi rafiki, kitu kinachopelekea ufanye usichotaka kufanya ni kwa sababu ya fedha. Umewahi kufanyika utafiti fulani, ambapo matapeli maarufu waliulizwa iwapo (more…)

2191; Familia Yako Imekushinda, Unahangaika Na Dunia!

By | December 30, 2020

Sisi binadamu huwa tunachekesha na kuhuzunisha kwa wakati mmoja. Mambo yaliyo ndani ya uwezo wetu kufanya huwa hatuyafanyi, bali yaliyo nje ya uwezo wetu ndiyo tunahangaika nayo. Mambo yaliyo muhimu na yenye manufaa kwetu huwa hatuhangaiki nayo, ila yale yasiyo muhimu na yasiyo na manufaa kwetu ndiyo yanatuhangaisha. Huwa tunakazana (more…)