Category Archives: KURASA ZA MAISHA

Kila siku mpya kwenye maisha yako ni sawa na ukurasa mpya wa kitabu.
Kwa kila siku mpya unachagua ufanye nini na maisha yako.
Kupitia makala hizi za KURASA ZA MAISHA, utajifunza mambo muhimu ya kufanya ili uwe namaisha bora zaidi.
Makala hizi za kurasa zinakujia kila siku.

2190; Maeneo Manne Muhimu Ya Kushinda…

By | December 29, 2020

Mafanikio yana maana tofauti kwa watu tofauti, lakini watu waliofanikiwa wanafanana kwa mengi, hata kama siyo kwa fedha na mali walizonazo. Wale waliofanikiwa kuna vitu wanakuwa wameshinda, ambavyo vinayafanya maisha yao kuwa tulivu na hivyo kuweza kupeleka umakini mkubwa kwenye kile wanachofanya badala ya kuhangaika na yasiyo sahihi. Kuna maeneo (more…)

2188; Vinabaki Na Wewe…

By | December 27, 2020

Ukila chakula, kinameng’enywa tumboni, kisha kufyonzwa mwilini na kwenda kuwa sehemu ya mwili wako. Hivyo kila unachokula, kinaenda kuwa sehemu ya wewe. Kadhalika kwenye yale tunayofanya, huwa yanakuwa sehemu yako, yanakuwa wewe. Kitu chochote unachofanya kwa kujirudia rudia, kinaenda kuwa tabia ambayo inakuwa sehemu yako. Hivyo chochote kile unachofanya, humfanyii (more…)

2186; Jukumu Lako Kuu…

By | December 25, 2020

Kwenye kila unachofanya kwenye maisha yako, kuna jukumu ambalo ni kuu na muhimu kwako kutekeleza, halafu kuna majukumu madogo madogo. Jukumu lililo kuu huwa ni gumu na matokeo yake hayaonekani haraka. Majukumu madogo madogo huwa ni rahisi kufanya na matokeo yake ni ya haraka. Lakini mafanikio makubwa huwa yanatokana na (more…)

2185; Muda Na Nguvu…

By | December 24, 2020

Kuna kauli moja fupi ila yenye maana kubwa sana, kauli hiyo inasema muda huwa ni tiba ya kila kitu. Chochote kinachoshindikana, kipe muda. Muda una nguvu kubwa, hasa unapokuwepo wa kutosha. Lakini wengi huwa hawaweki muda wa kutosha kwenye kitu chochote wanachofanya. Matokeo yake wanalazimika kutumia nguvu kubwa ili kulazimisha (more…)

2184; Ni Kujifunza, Siyo Kuiga…

By | December 23, 2020

Tunaishi kwenye zama ambazo hadithi za mafanikio ni nyingi kuliko mafanikio yenyewe. Kila mtu anapenda kujua hadithi ya wale waliofanikiwa sana. Pamoja na uwepo wa hadithi hizo, bado wanaofanikiwa ni wachache kati ya wengi wanaotaka kufanikiwa. Na tatizo kubwa ni kwamba hadithi hizo zimekuwa haziwasaidii watu, kwa sababu wamekuwa hawajifunzi (more…)

2183; Msongo Wa Mawazo…

By | December 22, 2020

Watoto wadogo na wanyama huwa ni nadra sana kupatwa na msongo wa mawazo. Hiyo ni kwa sababu wanaishi kwenye wakati uliopo, wanakabiliana na kilicho mbele yao. Ni vigumu kumkuta kuku akiwa na msongo kwamba kesho yake utakuwaje au kuhusu jana iliyopita au akihofia kuhusu yale yanayoendelea kwenye dunia. Kuku anakabiliana (more…)

2182; Ni Kwa Sababu Unapenda, Siyo Kwa Sababu Kuna Kitu Unategemea Kupata…

By | December 21, 2020

Chochote unachofanya kwenye maisha kwa mategemeo ya kupata kitu fulani, ukiweka juhudi utapata kile unachotaka kufanya. Lakini ukishakipata, huo ndiyo unakuwa mwisho wako, na wakati mwingine kupata ulichokuwa unatafuta kunaweza kuwa sumu na kikwazo kwako kupiga hatua zaidi. Wale wanaofanikiwa zaidi, wale wanaofanya makubwa kwenye maisha yao, ni wale wanaofanya (more…)

2181; Punguza Maamuzi Unayofanya…

By | December 20, 2020

Kila maamuzi unayofanya, yanapunguza sehemu ya nguvu ya utashi wako wa kiakili. Kadiri unavyofanya maamuzi mengi kwenye siku yako, ndivyo unavyochoka kiakili na kushindwa kufanya maamuzi bora. Na siyo lazima maamuzi yawe makubwa ndiyo yakuchoshe, chochote unachofikiria kwa muda kabla ya kuchukua hatua, kinakula nguvu yako ya akili. Mfano kama (more…)