Category Archives: KURASA ZA MAISHA

Kila siku mpya kwenye maisha yako ni sawa na ukurasa mpya wa kitabu.
Kwa kila siku mpya unachagua ufanye nini na maisha yako.
Kupitia makala hizi za KURASA ZA MAISHA, utajifunza mambo muhimu ya kufanya ili uwe namaisha bora zaidi.
Makala hizi za kurasa zinakujia kila siku.

2170; Unacholalamikia, Unakistahili…

By | December 9, 2020

  Kitu chochote unachokilalamikia au kulaumu kwenye maisha yako, unakistahili kabisa. Na kadiri utakavyoendelea na malalamiko na lawama zako, utaendelea kuwa na kitu hicho. Hakuna namna mambo yataenda kama unavyopanga wewe, hivyo kulalamikia watu au hali fulani kuwa kikwazo kwako ni utoto. Na kama hujui hilo, basi unastahili kabisa kile (more…)

2169; Kikiwa Muhimu, Unawekeza Kweli…

By | December 8, 2020

Kitu kinapokuwa muhimu kwa mtu, hufanya uwekezaji wa kutosha kwenye kitu hicho ili apate matokeo mazuri kwenye kitu hicho. Angalia pale mtu anapoumwa, atafanya awezavyo ili apate matibabu sahihi na aweze kupona. Angalia kwenye harusi, hata kama mtu ni masikini kiasi gani, atapambana awezavyo harusi iweze kwenda vizuri. Atahakikisha gharama (more…)

2168; Mtego Wa Mitandao Ya Kijamii Kwenye Umaarufu…

By | December 7, 2020

Mitandao ya kijamii huwa inahitaji kuwa na watumiaji wengi ndiyo iingize faida. Kadiri watu wanavyotumia mtandao kwa muda mrefu, ndivyo mtandao huo unavyonufaika kwa sababu faida yake ni muda wa watu. Kwa kuwa inategemea sana wingi wa watu ndiyo faida iwe kubwa, mitandao hii imekuwa inatumia njia mbalimbali kuwatega na (more…)

2167; Ni Wakati Mambo Yanapokuwa Magumu…

By | December 6, 2020

Wakati mambo ni mazuri, mtu anaweza kuahidi na kufanya kama anavyoahidi. Kama ilivyo kwa bahari tulivu, kila nahodha anaonekana ni mahiri. Au hali ya uchumi inapokuwa nzuri, kila mtu anaonekana anafanya vizuri. Lakini pale mambo yanapokuwa magumu, ndipo tunapata nafasi ya kujua nani kweli yuko vizuri na nani anaigiza. Warren (more…)

2166; Usiwe Mtu Wa Kujaribu, Bali Fanya Mpaka Upate…

By | December 5, 2020

Kuanza kitu kipya ni rahisi, unakuwa na hamasa kubwa na unaona njia ilivyo wazi ya kufanikiwa. Unakuwa unaona upande mmoja tu wa mafanikio, huoni upande wa pili wa changamoto ambazo lazima zipo. Angalia hadithi nyingi za fursa, mfano kilimo cha matikiti maji ambacho kimekuwa kinatumika kuwahadaa wengine. Mtu anaambiwa kilimo (more…)

2165; Nasa Kama Sumaku…

By | December 4, 2020

Sumaku huwa ina tabia ya kunasa, lakini huwa hainasi kila kitu. Sumaku haiwezi kunasa pamba, wala plastiki. Ila sumaku inapokutana na chuma, inakinasa kweli kweli. Kuna kitu kikubwa cha kujifunza kutoka kwenye sumaku, kuhusu kuchagua watu wa kuambatana nao na kuachana na wengine. Tunaitumia sumaku kwenye vitu ambavyo inavivuta na (more…)

2164; Kiburi Na Ujinga…

By | December 3, 2020

Ndiyo vitu pekee vinavyoleta anguko kubwa baada ya mtu kuwa amefanikiwa. Wote ambao waliwahi kufanikiwa na kufika ngazi za juu, lakini baadaye wakaanguka kutoka kwenye mafanikio yao, ni kwa sababu ya vitu hivyo viwili, kiburi na ujinga. Kiburi ni pale mtu anapojua kitu sahihi anachopaswa kufanya, lakini hakifanyi. Mafanikio huwa (more…)

2163; Ukweli Au Hadithi?

By | December 2, 2020

Sisi binadamu huwa hatuwezi kutulia kama hatujapata maelezo kuhusu kitu kinachotuhusu. Akili yetu hairuhusu kuwa njia panda bila ya kuwa na maelezo. Hivyo kuna njia mbili za kupata maelezo ya kitu, kupitia ukweli na kupitia hadithi. Ukweli ni jinsi kitu kilivyo, hivyo pale ukweli unapoulikana, watu huchukua huo. Hadithi ni (more…)

2162; Kufyeka Au Kung’oa?

By | December 1, 2020

Wengi wetu tumetokea familia zinazojihusisha na kilimo au tunafanya kilimo. Hivyo tunaelewa vizuri sana kuhusu magugu yanapokuwa shambani. Magugu huwa yanazuia mazao yaliyopandwa yasipate virutubisho na kukua vizuri, kwa sababu yananyonya rasilimali nyingi za ardhi. Ukitaka kuondoa magugu shambani, kuna njia mbili unaweza kutumia. Njia ya kwanza ni kuyafyeka au (more…)

2161; Njaa, Hasira, Upweke Na Uchovu…

By | November 30, 2020

Kamwe usifanye maamuzi ukiwa kwenye hali hizo nne. Kwani maamuzi utakayoyafanya ukiwa kwenye hali hizo, huishia kuwa maamuzi mabovu na yatakayokugharimu mno. Hali hizo huwa zinaondoa kabisa uwezo wa akili kufikiri kwa umakini na kufikia maamuzi sahihi. Unapofanya maamuzi kwenye hali hizo, unakuwa umesukumwa zaidi na hisia kuliko kufikiri. Kila (more…)