Category Archives: KURASA ZA MAISHA

Kila siku mpya kwenye maisha yako ni sawa na ukurasa mpya wa kitabu.
Kwa kila siku mpya unachagua ufanye nini na maisha yako.
Kupitia makala hizi za KURASA ZA MAISHA, utajifunza mambo muhimu ya kufanya ili uwe namaisha bora zaidi.
Makala hizi za kurasa zinakujia kila siku.

2160; Anza Na Wewe, Kisha Soko, Kisha Biashara…

By | November 29, 2020

Kuna njia kuu mbili ambazo zimekuwa zinatumiwa na wengi kuingia kwenye biashara. Njia ya kwanza ni mtu anapata wazo fulani la biashara, anaona ni wazo jipya ambalo halijawahi kufanyiwa kazi, anasukumwa kuanza kulifanyia kazi. Changamoto kubwa ya njia hii ni mara nyingi mawazo mapya huwa hayana soko, unaweza kuwa na (more…)

2159; Kutaka Kuibadili Dunia…

By | November 28, 2020

Kutaka kuibadili dunia ni kauli ambayo imekuwa inatumiwa na watu wengi. Wengi hujiambia ndoto yao ni kutaka kuibadili dunia, kupitia kile wanachofanya. Lakini wengi siyo tu huwa wanashindwa, bali wanaishia kuiharibu dunia. Dunia haihitaji kubadilishwa, dunia imekuwepo, ipo na itaendelea kuwepo. Wajibu wetu sisi ni kuielewa dunia na kisha kuyafanya (more…)

2157; Ni Vyote Kwa Pamoja, Kipato Na Matumizi…

By | November 26, 2020

Kwenye SEMINA YA KISIMA CHA MAARIFA 2020 mwanamafanikio mwenzetu Simeon Shimbe aliuliza; walimu wengi wa mambo ya fedha wanasisitiza zaidi mtu kuongeza kipato na siyo kupunguza matumizi, lakini kwenye kitabu cha ELIMU YA MSINGI YA FEDHA umesisitiza zaidi kupunguza matumizi, hiyo ikoje? Nilimjibu ni kweli kuongeza kipato ni msingi muhimu (more…)

2156; Ya Kila Mtu, Haina Mtu…

By | November 25, 2020

Moja ya sababu zinazopelekea mifumo ya kijamaa kushindwa ni kukosekana kwa uwajibikaji kwenye maeneo yanayotumia mfumo huo. Kwa kuwa kila kitu ni mali ya kila mtu, inakuwa vigumu kuwajibisha watu. Mtu anakuwa na uchungu pale kitu kinapokuwa chake, kuliko kinapokuwa cha wengine. Kwa kuwa kwenye mifumo ya ujamaa kila kitu (more…)

2155; Fanya Kama Unatoa Zawadi…

By | November 24, 2020

Safari ya mafanikio, kama ambavyo nimekuwa nakushirikisha mara kwa mara, ni ya muda mrefu, inahitaji msimamo na uvumilivu mkubwa. Hali hiyo inakaribisha uchovu, kwa sababu siyo kawaida kwetu binadamu kufanya kitu kwa muda mrefu, hasa pale unapohitajika kukazana kuwa bora kila wakati. Tumekuwa tunashirikishana njia nyingi za kukabiliana na uchovu (more…)

2154; Ni Kurudia Rudia…

By | November 23, 2020

Nguvu ya asili ipo kwenye msimamo na kurudia rudia. Hakuna chochote ambacho asili inafanya mara moja na kuacha, bali hurudia kwa muda mrefu na hapo ndipo matokeo makubwa hutengenezwa. Chukua mfano wa tone la maji, moja pekee haliwezi kuleta madhara yoyote, lakini tone hilo linapojirudia mara nyingi, linaweza kuvunja mwamba (more…)

2153; Ni Msukumo Kutoka Ndani Au Wivu?

By | November 22, 2020

Kikwazo kikubwa kinachowazuia watu kufanikiwa kwenye jambo lolote lile wanalofanya, ni kuanza kwa sababu zisizo sahihi. Iwe ni kazi ambayo mtu amechagua kufanya au biashara, kuna sababu kuu mbili za mtu kuingia kwenye kitu hicho. Sababu ya kwanza ni mtu kupenda kitu hicho kutoka ndani yake au kukichagua na kuwa (more…)

2152; Unalipa Sasa Au Utalipa Baadaye?

By | November 21, 2020

Kwenye maeneo mbalimbali yanayotoa huduma hasa za starehe, huwa yana taratibu zinazotofautiana za malipo. Kuna eneo ukienda unalipa kwanza ndiyo upewe huduma, wakati eneo jingine unapata huduma kwanza halafu unalipa mwisho. Kwa vyovyote vile huduma utapata, lakini lazima utalipia. Hivyo pia ndivyo ilivyo kwenye maisha yetu, kuna gharama za kulipa (more…)

2151; Kukubali Kutokukubaliana…

By | November 20, 2020

Mara nyingi watu wamekuwa wanashangaa nawezaje kukubaliana na kila mtu, hata kama anaamini na kusimamia kile ambacho ni tofauti kabisa na mimi. Nina mifano mingi ya namna ambavyo watu wamekuwa wanashangazwa na hilo na hata wengine kukasirishwa. Mfano tunaweza kuwa tunajadiliana jambo, ambapo niko upande fulani, halafu baada ya muda (more…)