Category Archives: KURASA ZA MAISHA

Kila siku mpya kwenye maisha yako ni sawa na ukurasa mpya wa kitabu.
Kwa kila siku mpya unachagua ufanye nini na maisha yako.
Kupitia makala hizi za KURASA ZA MAISHA, utajifunza mambo muhimu ya kufanya ili uwe namaisha bora zaidi.
Makala hizi za kurasa zinakujia kila siku.

2150; Nguvu Unazozitawanya Hovyo…

By | November 19, 2020

Nguvu, muda na pesa ni rasilimali muhimu sana kwenye safari ya mafanikio. Muda tumekuwa tunauzungumzia sana, jinsi ambavyo unapaswa kutumia fedha kuokoa muda badala ya kutumia muda kuokoa fedha. Tumejifunza sana kuhusu ukomo wa muda, kwamba ukishapotea haurudi tena, hivyo tunapaswa kuwa na ubahili nao kuliko tunavyokuwa na ubahili na (more…)

2149; Rahisi, Haraka, Bora Chagua Mbili…

By | November 18, 2020

Upo usemi maarufu kwenye biashara kwamba unaweza kuwa rahisi au haraka au bora, lakini unaweza kufanya viwili tu kwa wakati mmoja na siyo vyote vitatu. Hivyo unapaswa kuchagua viwili ambavyo utapambana navyo kwenye biashara yako. Hivyo pia ndivyo ilivyo kwenye mafanikio kwenye kila eneo la maisha, kupitia chochote unachokifanya. Unaweza (more…)

2148; Haikuwa Rahisi Kwao, Haitakuwa Rahisi Kwako…

By | November 17, 2020

Watu wote ambao walileta mapinduzi na mabadiliko makubwa kwenye kila eneo la maisha, ambayo tunayafurahia sasa, hawakukubalika kirahisi. Walipingwa, wakateswa na wengine kuuawa kwa sababu tu walifikiri tofauti na kundi kubwa lilivyokuwa linafikiri. Kwa upande wa falsafa, Socrates alikuja na njia mpya ya kuwajengea watu uwezo wa kufikiri, kuhoji na (more…)

2147; Msongo Ni Pale Ambapo Huwezi Kujidanganya Tena…

By | November 16, 2020

Watu wengi wamekuwa wanapitia msongo wa mawazo kwenye maisha yao na wasijue nini chanzo. Wanajikuta wamezama kwenye msongo huo na kushindwa kuondokana nao kwa sababu hawajui chanzo. Kuna sababu kubwa mbili, ya kwanza ni kulazimisha mambo, kutaka mambo yawe tofauti na yalivyo au nje ya uwezo wako, sababu hii hatutaijadili (more…)

2146; Unaweza Kwenda Kwa Muda Gani?

By | November 15, 2020

Watu huwa wanalalamikia hamasa wanazopata kutoka kwa wengine zimekuwa hazidumu. Mfano mtu anahudhuria semina au kusoma kitabu na kuhamasika sana, anatoka akiwa na mipango mikubwa ya kwenda kubadili kabisa maisha yake. Lakini siku chache baadaye hamasa ile inakuwa imeisha kabisa na kurudi kwenye mazoea. Wengi hufikiri tatizo liko kwenye hamasa (more…)

2145; Njia Ya Uhakika Ya Kufika Na Kubaki Kwenye Utajiri…

By | November 14, 2020

Watu waliopo kwenye safari ya kuelekea kwenye utajiri ni wengi, lakini kati yao, wachache ndiyo wanaofika kwenye utajiri. Na katika kundi la wale wanaofika kwenye utajiri, ni wachache ambao hudumu na utajiri huo. Wengi huupata utajiri na baadaye kuwapotea, kuanguka kutoka kwenye utajiri. Wale wanaoshindwa kufika kwenye utajiri ni kwa (more…)

2142; Wakati Gani Wa Kuyaamini Machale…

By | November 11, 2020

Kuna wakati unafanya maamuzi bila ya kujua kwa nini unayafanya na yanaishia kuwa maamuzi sahihi. Hapo unajiambia kwamba machale yamekucheza na ukaona kitu ambacho huwezi kukielezea lakini ni sahihi. Lakini pia kuwa wakati machale hayo hayo yanakupoteza, yanapelekea ufanye maamuzi ambayo siyo sahihi na yanayokugharimu. Machale ni zile hisia unazozipata (more…)

2141; Hakuna Kinachofanywa Mara Moja…

By | November 10, 2020

Simu ya Iphone iko kwenye toleo la 12, wakati toleo la kwanza linatoka, ilikuwa ni mapinduzi makubwa mno kwenye ulimwengu wa teknolojia na mawasiliano. Ilikuwa ni kitu ambacho hakijawahi kuonekana wala kudhaniwa na ilibadili kabisa maisha ya watu. Ingetosha kwa kampuni ya Apple kusema wamemaliza, wameweza kuleta mapinduzi makubwa na (more…)