Category Archives: KURASA ZA MAISHA

Kila siku mpya kwenye maisha yako ni sawa na ukurasa mpya wa kitabu.
Kwa kila siku mpya unachagua ufanye nini na maisha yako.
Kupitia makala hizi za KURASA ZA MAISHA, utajifunza mambo muhimu ya kufanya ili uwe namaisha bora zaidi.
Makala hizi za kurasa zinakujia kila siku.

2120; Kazi Na Mbwembwe…

By | October 20, 2020

Watu wamekuwa wanatumia nguvu nyingi kwenye mbwembwe kuliko kwenye kazi. Kwenye maonesho kwamba wanafanya kazi kuliko kazi yenyewe wanayoifanya. Wengi wanakazana ili waonekane wanafanya kazi, ili waonekane wako ‘bize’ lakini hakuna chochote kikubwa wanachozalisha. Na haya yote yamechochewa na ukuaji wa mitandao ya kijamii, maana hiyo inampa kila mtu nafasi (more…)

2119; Kuna Gharama Zaidi Utakayoilipa…

By | October 19, 2020

Kila unapoendelea kusubiri na usianze kufanya kile ulichopanga kufanya, kuna gharama ya zaidi ambayo utalazimika kuilipa. Kila unaposubiri mpaka tarehe ya mwisho ya kufanya kitu ikaribie ndiyo ufanye, utakifanya kwa haraka na ubora utakuwa hafifu kitu ambacho kitakugharimu zaidi au kukupunguzia manufaa ambayo ungeyapata kama ungekifanya mapema. Kila unaposubiri mpaka (more…)

2118; Kujikana Wewe Mwenyewe…

By | October 18, 2020

Wanaotaka mafanikio makubwa ni wengi, Wanaotaka kuwa na utajiri ni wengi, Wanaotaka umaarufu ni wengi, Lakini ni wachache sana wanaopata kile wanachotaka, katika watu 100 ni mmoja pekee anayefikia kile hasa anachotaka. Siyo kwa sababu watu hao ni wa tofauti sana, ila watu hao wamejitoa zaidi ya wale ambao hawafikii. (more…)

2117; Uhuru Wa Kweli Ni Ule Unaoujenga Mwenyewe…

By | October 17, 2020

Hakuna uhuru unaopatikana kwa kutegemea wengine, unaweza kuona kuna uhuru kwenye hilo lakini ni swala la muda tu kabla watu hao unaowategemea hawajaja na masharti yao, ambayo yanaweza kuwa kikwazo kwako. Tuchukue mfano mzuri wa mitandao ya kijamii, wakati inakuja kila mtu alishangilia kwamba sasa mawasiliano yana uhuru kamili. Huhitaji (more…)

2116; Kizazi Laini Laini…

By | October 16, 2020

Mtu mmoja amewahi kusema kama watu wanaoishi sasa watachukuliwa na kurudishwa kwenye aina ya maisha ambayo watu waliishi kwenye karne ya kwanza, basi karibu wote watafariki kwa haraka sana. Hii ni kwa sababu mazingira ya sasa ni rahisi sana ukilinganisha na mazingira ya kipindi hicho. Mazingira hayo rahisi yamefanya sehemu (more…)

2115; Unapokuwa Njia Panda, Iangalie Asili…

By | October 15, 2020

Asili huwa inajiendesha kwa kanuni zake yenyewe na haijawahi kushindwa kwenye hilo. Kila kitu kinaenda kwa taratibu zake na asili haina uonevu wala upendeleo. Asili haina wema wala ubaya, bali inaenda kwa namna ambayo ni bora kwa asili kwa ujumla. Simba kumla swala inaweza kuonekana ni uonevu kwa swala, lakini (more…)

2114; Linda Rasilimali Hizi Tano…

By | October 14, 2020

Wale wanaofanya makubwa kwenye maisha yao siyo kwamba wana tofauti kubwa sana na wanaoshindwa kufanya makubwa. Bali wanajitambua zaidi kuliko wengine. Na katika kujitambua kwao, wanazijua rasilimali muhimu za kulinda ili waweze kufanya makubwa. Hizo ni rasilimali ambazo zikipotea huwa zina madhara makubwa ya kumzuia mtu asipige hatua. Rasilimali hizi (more…)

2113; Fanya Kitu Kuwa Bora Zaidi Ya Kilivyo Sasa…

By | October 13, 2020

Kuna watu wanaamini ushindani ndiyo njia nzuri wa kuwasukuma kufanya makubwa zaidi. Lakini hilo siyo kweli, ushindani huwa unamfanya mtu asahau kule anakotaka kufika na kuanza kuangalia wengine wanafanya nini ili kuwazidi. Kinachotokea, hata kama umewashinda wale unaoshindana nao, unakuwa umepoteza, kwa sababu hujawa wewe. Mafanikio ya kweli hayaletwi na (more…)

2112; Kwa Nini Usianze Kuishi Hivyo Sasa…

By | October 12, 2020

Siku moja nikiwa kliniki, niliona kwenye orodha ya wagonjwa wanaosubiri kuingia kwangu kutibiwa kukiwa na mgonjwa mwenye miaka 93. Kwa haraka nilipata picha atakuwa ni mzee sana, ambaye atakuwa kwenye kiti cha kuendeshwa na atakuwa hawezi kutembea. Lakini nilipoita mgonjwa huyo, alikuja akiwa anatembea mwenyewe na alionekana kuwa na nguvu (more…)

2111; Sababu Pekee Ya Kufanya Kilicho Sahihi…

By | October 11, 2020

Watu wengi hufanya kilicho sahihi kwa sababu wana ajenda fulani, kuna kitu wanategemea kukipata kwa kufanya kilicho sahihi. Hivyo wengi hufanya kilicho sahihi kama maigizo, haitoki kweli ndani yao, bali wanafanya kwa mategemeo fulani. Lakini Mstoa Marcus Aurelius alituasa vyema, sababu pekee ya kufanya kilicho sahihi ni kwa kuwa ndiyo (more…)