Category Archives: KURASA ZA MAISHA

Kila siku mpya kwenye maisha yako ni sawa na ukurasa mpya wa kitabu.
Kwa kila siku mpya unachagua ufanye nini na maisha yako.
Kupitia makala hizi za KURASA ZA MAISHA, utajifunza mambo muhimu ya kufanya ili uwe namaisha bora zaidi.
Makala hizi za kurasa zinakujia kila siku.

2110; Msimamo Na Ung’ang’anizi Kwenye Kuchukua Hatua…

By | October 10, 2020

Kuwa na nidhamu kubwa ya msimamo na ung’ang’anizi kwenye kuchukua hatua ndiyo kinachowatofautisha wale wanaofanikiwa sana na wanaobaki kuwa kawaida. Chukua mfano wa watu wawili, mmoja ana wazo la kawaida tu, labda ufugaji au biashara au kilimo, anaamua kuchukua wazo hilo kwa miaka kumi bila kuacha. Mwingine kwa miaka hiyo (more…)

2109; Kama Fedha Inaweza Kutatua, Huna Tatizo…

By | October 9, 2020

Sehemu kubwa ya matatizo yanayowasumbua wengi kwenye maisha siyo matatizo halisi, bali tatizo la msingi linakuwa ni fedha. Kama una tatizo lolote linalokusumbua na unaweza kulitatua kwa fedha, basi jua huna tatizo, bali unachokosa ni fedha. Kwa kujua hili, inakupunguzia mzigo wa mawazo na msongo ambao umekuwa unajipa kwa matatizo (more…)

2108; Jiandae Kwa Mchakato…

By | October 8, 2020

Kinachowaangusha wengi kwenye hadithi za mafanikio ni hiki; kuangalia pale waliofanikiwa wapo sasa na kutaka kufika hapo,  bila kupitia mchakato wa kufika pale. Yeyote unayemuona amefanikiwa leo, hakuamka na kujikuta kwenye mafanikio hayo, na wala hakupita njia ya mkato isiyohitaji kazi. Alipitia kwenye mchakato mrefu ambao huwa haupewi uzito sana (more…)

2107; Kimbilia  Kwenye Vitabu…

By | October 7, 2020

Maisha yana changamoto, hakuna chochote kitakachokwenda kama ulivyopanga kwa asilimia 100. Utaweka mipango yako vizuri na kuanza kuitekeleza, lakini baadaye utakutana na vikwazo na changamoto ambazo zinakuzuia kupata kile unachotaka. Hapo ndipo wengi hukwama, kukata tamaa na kuachana na safari waliyokuwa wameianza. Lakini haipaswi kuwa hivyo, kama kweli umejitoa kupata (more…)

2106; Unakosa Muda Na Kuchoka Sana Kwa Sababu…

By | October 6, 2020

Unahangaika na mambo mengi ambayo hayana mchango wowote kukufikisha kule unakotaka kwenda. Kila siku unapata mawazo ya kuanza na kujaribu vitu vipya, ambavyo unaviona vitakuwa bora zaidi. Lakini ambacho hufikirii kabla hujaanza kitu kipya ni kwamba muda na nguvu zako vina ukomo. Kwa siku una saa 24 tu na haziongezeki, (more…)

2105; Kauli Ya Kukujengea Imani Ya Kupata Unachotaka…

By | October 5, 2020

“Nguvu kubwa inayouendesha ulimwengu ipo ndani yangu. Chochote ninachotaka kwa imani hai, mategemeo chanya na nia thabiti kiko njiani kuja kwangu. Na kama kile ninachotaka hakijaja, basi ni kwa sababu kuna kikubwa na bora zaidi kipo njiani kuja kwangu. Ninajua imani hii ni ya kweli na nitaisimamia mara zote.” Kauli (more…)

2104; Wanasambaza Walichonacho…

By | October 4, 2020

Kila mtu huwa anasambaza kile kilicho ndani yake, hakuna anayependa kukaa na kitu ndani yake. Hivyo wale wenye hofu, huwa wanasambaza hofu hiyo kwa wengi zaidi. Na wenye maumivu huwa wanahakikisha wanawapa watu wengi maumivu hayo. Kadhalika wanaoteseka, huwa wanahakikisha kuwatesa wengine. Na wale wenye upendo, huwa wanawapenda zaidi wengine. (more…)

2103; Adui Mmoja Ni Maadui Wengi…

By | October 3, 2020

Pita kwenye haya maisha kwa amani kadiri uwezavyo. Enenda na wengine kwa mapatano na jitahidi kadiri uwezavyo kutokuingia kwenye migogoro na wengine. Mara zote fanya kile kilicho sahihi na simama kwenye ukweli na haki. Kuna watu watachukizwa na wewe kuishi kwenye misingi hiyo, watajenga uadui na wewe, usijisumbue nao wala (more…)

2102; Kwa Wengine Ni Mambo Ya Kawaida…

By | October 2, 2020

Ni rahisi kutoa ushauri kwa wengine, lakini ni vigumu wewe mwenyewe kuuishi ushauri unaowapa wengine. Hata pale mambo yanapowatokea watu wengine, ni rahisi kwetu kuwashauri na kuwapa moyo, lakini mambo hayo hayo yanapotutokea sisi wenyewe hatuwezi kutumia ushauri ambao tumekuwa tunawapa wengine. Kinacholeta hali hizi za tofauti ni hisia ambazo (more…)

2101; Siyo Asilimia 10, Bali Mara 10…

By | October 1, 2020

Watu wengi wamekuwa wanajiambia wanaanzisha biashara mpya kwa sababu wameona fursa fulani mahali. Lakini ukweli siyo wanaanzisha biashara mpya, bali wanakwenda kuiga biashara nyingine inayofanyika eneo hilo au kuhamisha biashara kutoka eneo jingine kwenda hapo. Hivyo biashara wanayokwenda kuanzisha siyo ya tofauti wala ya kipekee sana. Na hapo wanakuwa wamejipeleka (more…)