Category Archives: KURASA ZA MAISHA

Kila siku mpya kwenye maisha yako ni sawa na ukurasa mpya wa kitabu.
Kwa kila siku mpya unachagua ufanye nini na maisha yako.
Kupitia makala hizi za KURASA ZA MAISHA, utajifunza mambo muhimu ya kufanya ili uwe namaisha bora zaidi.
Makala hizi za kurasa zinakujia kila siku.

2099; Lakini Mbona Hawakamatwi?

By | September 29, 2020

Kuna wakati unaweza kuona watu wanahangaika na kitu kisichokuwa sahihi, na unajua kabisa siyo sahihi lakini unaona kikiendelea tu, hakikatazwi na wala wanaofanya hawakamatwi. Kwa vile kitu hicho kinaendelea, watu wananufaika kweli kweli, na wanakuonesha wazi kwamba kitu hicho kinawanufaisha. Mwanzo ulikuwa na msimamo kwamba hutajihusisha na kitu hicho, kwa (more…)

2098; Tabia Ni Kama Akiba…

By | September 28, 2020

Akiba ni kitu unachoweka wakati mambo yako yanakwenda vizuri, ili kikusaidie pale mambo yatakavyokwenda vibaya. Unapozingatia hilo, unaepuka usumbufu na gharama zisizo na ulazima. Mfano unapojikuta kwenye changamoto za kifedha, ukiwa na akiba unazitatua, ukiwa huna, unaingia kwenye mkopo ambao utakuumiza zaidi. Unanunua mwavuli wakati wa kiangazi, ili wakati wa (more…)

2097; Yote Huanza Kwa Nia Njema…

By | September 27, 2020

Ni watu wachache sana ambao huwa wanafanya makosa kwa kusudia. Wengi huwa wanaanza na nia njema kabisa, lakini matokeo yanakuja kuwa makosa makubwa na yenye madhara. Mara nyingi tunapofanya maamuzi ya kufanya kitu, huwa tunaamini hatua tunazokwenda kuchukua zitarahisisha zaidi hali kuliko ilivyo sasa. Mfano mtu anapochukua hatua ya kudanganya, (more…)

2096; Huo Muda Zaidi Umeutumia Kufanya Nini?

By | September 26, 2020

Muda ni changamoto kwa kila mtu, kila mtu hana muda na kila mtu anapoteza muda. Yaani ni sawa na kumkuta mtu anakulalamikia hana fedha, lakini wakati huo huo anachukua fedha na kuzitupa. Kwenye fedha inaonekana haraka, lakini kwenye muda haionekani, kwa sababu muda huwa unatuponyoka. Mtu anaweza kupambana apate muda (more…)

2095; Kitu Pekee Anachujua Guru Na Usichojua…

By | September 25, 2020

Wahamasishaji, washauri, viongozi wa dini na watu wengine ambao watu wanawaamini na kuwatumia kama mwongozo kwao katika kufanya maamuzi mbalimbali, wamekuwa wanaonekana ni watu wenye uwezo fulani wa juu kuliko wengine. Kuonesha hilo, wale wenye mafanikio makubwa kwenye kuwashawishi wengi wafuate kile wanachowaambia, wamepewa jina la guru, ikiwa ni neno (more…)

2094; Fanya Yako Na Iache Dunia Ifanye Yake…

By | September 24, 2020

Fanya kazi kwa juhudi na maarifa na utafika kwenye mafanikio makubwa. Huu ni ushauri ambao kila mtu anayetaka mafanikio ya uhakika huwa anapewa. Lakini wengi huwa hawauelewi ushauri huu na hivyo kuishia kuumia. Ushauri unaeleza wazi kwamba fanya kazi kwa juhudi na maarifa, ukisisitiza upande wako wewe ni kuweka kazi. (more…)

2093; Thamani Ni Kubwa Kuliko Bei…

By | September 23, 2020

Unaweza kujipa sababu nyingi kwa nini umenunua kitu, kwamba unakipenda, kwamba unakithamini lakini zote hizo ni sababu za juu juu tu. Sababu halisi kwa nini umenunua kitu, ni kwa sababu thamani unayoipata ni kubwa kuliko gharama unazolipia. Yaani thamani yake ni kubwa kuliko bei. Chukua mfano, unataka kununua gari, ukaenda (more…)

2091; Jiwekee Ukomo Wa Matumizi Ya Muda Wako…

By | September 21, 2020

Kinachotufanya tuahirishe yale tunayopanga kufanya, ni kwa sababu tuna machaguo mengi ya nini tunaweza kufanya na muda tulionao. Hivyo kile tulichopanga kufanya kinapoonekana kigumu au chenye changamoto, ni rahisi kukimbilia kwenye kingine kinachoonekana rahisi zaidi. Kwa njia hii, unajikuta ukitoroka yale uliyopanga kufanya, ukijipa sababu nyingi unazoweza kuona ni za (more…)