Category Archives: KURASA ZA MAISHA

Kila siku mpya kwenye maisha yako ni sawa na ukurasa mpya wa kitabu.
Kwa kila siku mpya unachagua ufanye nini na maisha yako.
Kupitia makala hizi za KURASA ZA MAISHA, utajifunza mambo muhimu ya kufanya ili uwe namaisha bora zaidi.
Makala hizi za kurasa zinakujia kila siku.

2080; Mambo Matatu Yatakayokujengea Heshima…

By | September 10, 2020

Sifa ambayo mtu unajijengea, ina mchango mkubwa sana kwenye mafanikio au kushindwa kwako. Kuna watu wanashangaa kwa nini mambo yao hayaendi sasa, lakini wamesahau ambayo wamewahi kufanya huko nyuma na sasa ni kikwazo kwao. Ili kuhakikisha hujijengei sifa mbaya inayokuwa kikwazo kwa mafanikio yako, hapa kuna mambo matatu muhimu ya (more…)

2079; Hadithi Za Mafanikio Zisiwe Kikwazo Kwako…

By | September 9, 2020

Hadithi za mafanikio zimekuwa kikwazo cha mafanikio kwa walio wengi. Na wengi wanaokwamishwa na hadithi hizo ni wale ambao hawajajua nini hasa wanachotaka kwenye maisha yao. Hivyo wakisoma hadithi moja ya mtu aliyefanikiwa kwenye kulima mpunga, wanapanga kwenda kulima mpunga. Kesho wakisoma hadithi ya mtu mwingine aliyefanikiwa kwenye kufuga kuku, (more…)

2078; Akili Za Kushikiwa…

By | September 8, 2020

Umeamka asubuhi, hujapangilia siku yako itakwendaje, unaona uingie mtandaoni kidogo au ufuatilie habari. Huko unakutana na habari moto moto, kuhusu msanii aliyefanya jambo la ajabu au mwanasiasa aliyetoa kauli ya hovyo au habari mpasuko za kusisimua. Siku yako nzima inaendeshwa na habari ulizosikia, unabishana, kupinga au kukubaliana na habari husika (more…)

2077; Umaarufu Au Uaminifu?

By | September 7, 2020

Kwa zama tunazoishi sasa, wengi wanaona njia rahisi ya kufikia mafanikio makubwa ni umaarufu. Kwamba kadiri watu wengi zaidi wanavyokujua ndivyo unavyopata mafanikio makubwa. Ni rahisi kufikiria hivyo kabla mtu hujafika kwenye ngazi hiyo ya umaarufu. Lakini wale waliofika kwenye ngazi hiyo, hugundua haiwapi uhuru. Wakishakuwa maarufu maisha yanaacha kuwa (more…)

2076; Magugu Yasiyoisha…

By | September 6, 2020

Kama umewahi kulima hata bustani ya mboga au maua, unajua kwamba kuondoa magumu kwenye eneo unalolima ni zoezi lisilo na ukomo. Huondoi mara moja na shamba likawa safi milele. Kila wakati unapaswa kurudia zoezi la kuondoa magugu. Kadhalika kwenye kusafisha miili yetu, mtu unaoga kila siku kwa sababu uchafu unajirudia (more…)

2075; Magumu Matatu Ya Kiroho…

By | September 5, 2020

Utulivu umekuwa ni kitu kigumu kwenye zama tunazoishi sasa. Maelewano pia yamekuwa siyo mazuri. Hali hizi zinachochewa na magumu matatu ya kiroho ambayo wengi wanayapitia kwenye zama tunazoishi sasa. Ugumu wa kwanza ni kuwapenda wale wanaokuchukia. Ni rahisi kusema adui mpende, lakini inapotokea mtu amefanya jambo linalokukwaza, kukuumiza au kukuangusha, (more…)

2074; Kama Unataka Mafanikio Ya Haraka, Tumia Mbinu Hizi Nne…

By | September 4, 2020

Mbinu zote za mafanikio ya haraka ambazo watu wamekuwa wanajifunza zimekuwa hazifanyi kazi kwao kwa sababu zinaondoa kiungo kimoja muhimu, kazi. Hakuna mafanikio ambayo hayahitaji kazi, kufikia mafanikio makubwa kwa haraka bila ya kuweka kazi ni kitu ambacho hakipo. Hivyo usije ukadanganyika hata kidogo. Kama unachotaka ni kupata mafanikio ya (more…)

2073; Sharti Na Chaguo…

By | September 3, 2020

Kama kuna kitu ambacho ni sharti ukifanye, basi huna uhuru wa kuchagua, unapaswa kufanya. Kuigiza kama vile una uhuru wa kuchagua ni kujidanganya na kujitengenezea msongo zaidi. Kama una uhuru wa kuchagua kile unachofanya basi hilo siyo sharti, unachagua nini ufanye. Kuigiza kama vile ni sharti kufanya ni kujinyima uhuru (more…)

2072; Usijilinganishe Na Kiwanda Au Taasisi…

By | September 2, 2020

Kabla ya mapinduzi ya viwanda, watu wengi walikuwa wanafanya kazi zao binafsi na kila mtu alilenga aina fulani ya wateja ambao atawafanyia kazi. Hivyo mtu alipokuwa na uhitaji, alijua ni mtu gani anayemfaa kwa kazi aliyonayo. Mapinduzi ya viwanda yalileta mabadiliko mengi, kubwa kabisa likawa kuzalisha bidhaa kwa wingi na (more…)

2071; Umekokotoa Gharama Ambatanishi?

By | September 1, 2020

Tunaponunua kitu, huwa tunaangalia gharama tunayoingia kwenye kununua kitu hicho wakati wa matumizi. Hivyo kama gharama tunaweza kuimudu, tunanunua. Kuna gharama za msingi na muhimu zaidi kuangalia kuliko ile tu ya kununua. Gharama hizo ni zile endelevu, ambazo zinaambatana na kitu ulichonunua. Kwa vitu vilivyo wazi kwa gharama zake, huwa (more…)