Category Archives: KURASA ZA MAISHA

Kila siku mpya kwenye maisha yako ni sawa na ukurasa mpya wa kitabu.
Kwa kila siku mpya unachagua ufanye nini na maisha yako.
Kupitia makala hizi za KURASA ZA MAISHA, utajifunza mambo muhimu ya kufanya ili uwe namaisha bora zaidi.
Makala hizi za kurasa zinakujia kila siku.

2090; Angalia Umri Wako Usiwe Kikwazo Kwako…

By | September 20, 2020

Moja ya vikwazo ambavyo vimekuwa vinawazuia watu kufanikiwa lakini hawavijui ni umri. Wengi hawajawahi kukaa chini na kutafakari jinsi umri unaathiri hatua wanazochukua, wanadhani wanachofanya ndiyo wanachotaka, kumbe umri wao umekuwa na ushawishi. Kwa vijana, wengi huwa hawaridhiki na kile walichonacho, wanapenda mabadiliko ya haraka, wapo tayari kujaribu vitu vipya (more…)

2089; Unasikiliza Watu Wa Aina Gani?

By | September 19, 2020

Hatua unazopiga na matokeo unayopata, vinategemea sana aina ya watu waliokuzunguka. Watu hao wanagawanyika kwenye makundi mawili na ndani ya kila kundi wanagawanyika mara mbili. Kundi la kwanza ni wale wanaokutia moyo na kukushauri upige hatua zaidi. Hawa wanakubaliana na kile unachofanya na wanakupa sababu ya kuendelea. Ni rahisi kuwapenda (more…)

2088; Hasira Zako Haziwezi Kubadili Kanuni Za Asili…

By | September 18, 2020

Umeamka asubuhi, unataka kuwahi mahali, unajua kabisa usafiri wako uko vizuri, ila asubuhi hiyo unajaribu kuuwasha na hauwaki. Ulishapanga kabisa muda uliozoea kufika eneo husika na sasa usafiri ambao umekuwa unatumia kila siku hauwaki. Unaweza kupata hasira, ukakazana kuendelea kuwasha ukitegemea uwake kwa haraka kama ulivyo na haraka wewe, lakini (more…)

2087; Kinachofanya Upate Muda Wa Kuhangaika Na Mambo Madogo Madogo…

By | September 17, 2020

Kuhangaika na mambo madogo madogo kwenye maisha yako ndiyo kikwazo kwako kuhangaika na mambo makubwa na yatakayokuwezesha kupiga hatua kubwa kwenye maisha yako. Unaweza kujishangaa, iweje upoteze muda, nguvu na umakini wako kwa mambo yasiyo na tija, huku kukiwa na mambo mengine yenye tija. Kuna mambo matatu yanayopelekea hali hiyo. (more…)

2086; Kauli Ya Kishujaa Na Inayokupa Uhuru…

By | September 16, 2020

Kwenye moja ya mahojiano yake na watu mbalimbali waliofanikiwa, mwandishi James Altucher alikuwa anamhoji mchekeshaji na mfanyabiashara Bryon Allen ambaye alianza ujasiriamali akiwa na umri wa miaka 12. Alipokutana na wachekeshaji maarufu, aliona hicho ndiyo kitu anachotaka kufanya kwenye maisha yake na hapo alijipa kauli ya kishujaa na iliyompa msukumo (more…)

2085; Kusimamia Ukweli Kuna Gharama…

By | September 15, 2020

Kila kitu chenye thamani kwenye maisha, kina gharama, mafanikio yana gharama yake kubwa sana na ndiyo maana katika kila watu 100, ni mmoja pekee ambaye anakuwa na mafanikio makubwa. Moja ya gharama kubwa ambayo mtu unapaswa kulipa kwenye mafanikio, ni kusimama kwenye ukweli. Kinachofanya mmoja kati ya 100 ndiyo afanikiwe, (more…)

2084; Kukuza Hofu Au Kuchukua Hatua…

By | September 14, 2020

Kwa kila jambo unalopanga kufanya, kuna hatari ya kupata matokeo mabaya na hivyo kushindwa. Kila kitu kina hatari hiyo, hata uwe na uhakika kiasi gani. Hatari hiyo huwa inazalisha hofu ndani yetu, lakini kiwango cha hofu tunayokuwa nayo, huwa hakilingani na kiwango cha hatari. Hofu tunayokuwa nayo hua inakua kadiri (more…)

2083; Tunakuangalia Wewe Wa Leo…

By | September 13, 2020

Umekuwa unayatoroka maisha, kwa kuepuka kuishi leo na kukimbilia kuishi jana na kesho. Kwa kuwa ugumu wote wa maisha yako unakabiliana nao leo, ni rahisi kujikumbusha mazuri yaliyopita au kujiliwaza kwa mazuri unayotegemea yawe. Lakini hilo halitatui ugumu unaokabiliana nao. Unakuwa unajidanganya tu, kwa sababu jana haitajirudia na hiyo kesho (more…)

2082; Mbwa Anayetembea Kwa Miguu Miwili…

By | September 12, 2020

Seth Godin ni mmoja wa watu bora wa masoko hapa duniani. Msingi wake mkuu wa masoko umebebwa kwenye moja ya vitabu vyake ambacho kimekuwa maarufu sana, alikiita kitabu hicho Purple Cow, yaani ng’ombe wa zambarau. Anasema tumezoea kuwaona ng’ombe weusi, weupe na kahawia, hivyo huwezi kumkuta mtu anashangaa ona yule (more…)

2081; Kanuni Ya Maisha Rahisi Kutoka Kwa Epictetus…

By | September 11, 2020

Maisha ni magumu, lakini huwa tunayafanya kuwa magumu zaidi kwa baadhi ya mambo tunayohangaika nayo. Wastoa, hasa mwanafalsafa Epictetus alikuwa akisisitiza sana kujua mambo yaliyo ndani ya uwezo wako na kujishughulisha nayo na kujua yale yaliyo nje ya uwezo wako na yasikusumbue. Katika mwendelezo wa hilo, Epictetus anatushirikisha kanuni ya (more…)