Category Archives: KURASA ZA MAISHA

Kila siku mpya kwenye maisha yako ni sawa na ukurasa mpya wa kitabu.
Kwa kila siku mpya unachagua ufanye nini na maisha yako.
Kupitia makala hizi za KURASA ZA MAISHA, utajifunza mambo muhimu ya kufanya ili uwe namaisha bora zaidi.
Makala hizi za kurasa zinakujia kila siku.

2070; Je Umeweka Kazi?

By | August 31, 2020

Nimekuwa nasema, moja ya vitu tunavyopaswa kujifunza kutoka kwenye hadithi za waliofanikiwa ni mchakato waliopitia na siyo kile ambacho wamefanya. Wale waliofanikiwa, kama wangeanza tena kufanya walichofanya, wasingeweza kupata matokeo waliyopata sasa, lakini bado wangefanikiwa kwa kupata matokeo tofauti kwa sababu wana mchakato wanaoutumia. Unaposikia kwamba Thomas Edison alishindwa mara (more…)

2069; Gharama Ya Umaarufu…

By | August 30, 2020

Kila mtu huwa anapenda kuwa maarufu, lakini wengi huwa hawajui gharama kubwa ambayo umaarufu inakuja nayo. Wengi hukazana kufikia umaarufu na wanapoufikia wanajuta kwa nini walikuwa wanautafuta. Hasa pale wanapokuwa maarufu kwa sababu walikuwa wanatafuta umaarufu na siyo kwa sababu kuna kitu kikubwa wamefanya. Gharama kubwa ya umaarufu ni kukosa (more…)

2067; Kitendawili Kilichopo Kwenye Maamuzi…

By | August 28, 2020

Zipo changamoto nyingi ambazo wengi wamekuwa wanakutana nazo wakati wa kufanya maamuzi na hizo kuwa kikwazo kwao kupiga hatua kwenye maisha yao. Kuna changamoto ya kuwahi kufanya maamuzi, hasa pale mtu anapokuwa anaendeshwa na hisia kali za furaha au hasira. Aina hii ya maamuzi huwa siyo sahihi na baadaye huwa (more…)

2066; Kujikweza Na Kujiamini, Ushahidi Na Kuamini, Ukweli Na Maoni…

By | August 27, 2020

Kuna vitu ambavyo huwa vinakaribiana sana, ambapo mstari wa kuvitofautisha ni mwembamba sana kiasi kwamba usipokuwa makini unaweza kwenda upande usio sahihi. Tukianza na kujikweza na kujiamini, hivi ni vitu vinavyokaribiana sana. Kujiamini ni kuzuri, kunakusaidia kufanya makubwa kwenye maisha yako. Lakini pale kujiamini huko kunapozidi na ukaona hakuna aliye (more…)

2064; Ukweli Ni Sasa…

By | August 25, 2020

Kwenye kitabu cha Thinking, Fast and Slow mwandishi ametushirikisha tafiti ambazo ukizitafakari kwa kina, utashangazwa sana na jinsi akili zetu zinavyofanya kazi. Kwenye moja ya tafiti hizo ameonesha kwamba, tunachokumbuka kuhusu siku za nyuma siyo uhalisia wa tukio zima, bali jinsi tukio lilivyoisha. Kwa maana hii basi, sehemu kubwa ya (more…)

2063; Mtego Uliopo Kwenye Furaha…

By | August 24, 2020

Kinachowafanya wasanii au watu wengine maarufu kuingia kwenye madawa ya kulevya ni hiki. Kazi zao zinahusisha kutoa burudani au huduma kwa watu wengi kwa wakati mmoja. Pale wanapokuwa wanafanya kazi yao, wanakuwa kwenye furaha ya hali ya juu sana. Fikiria msanii anafanya tamasha linalohudhuriwa na watu zaidi ya elfu 10 (more…)

2062; Ubobezi Uko Kwenye Vitu Vidogo Vidogo…

By | August 23, 2020

Ukitapa kufikia ubobezi na mafanikio kwenye eneo lolote la maisha yako, unapaswa kuweka juhudi zako kwenye vitu vidogo vidogo, ambavyo ndiyo msingi mkuu wa eneo hilo. Na siyo tu kuvijua, maana tayari unavijua, bali kuvifanya. Angalia eneo la fedha, msingi mkuu uko kwenye kupunguza matumizi, kuongeza kipato na kuwekeza. Hakuna (more…)