Category Archives: KURASA ZA MAISHA

Kila siku mpya kwenye maisha yako ni sawa na ukurasa mpya wa kitabu.
Kwa kila siku mpya unachagua ufanye nini na maisha yako.
Kupitia makala hizi za KURASA ZA MAISHA, utajifunza mambo muhimu ya kufanya ili uwe namaisha bora zaidi.
Makala hizi za kurasa zinakujia kila siku.

2060; Mipango Ni Kama Ramani…

By | August 21, 2020

Kama umewahi kutumia ramani kufika mahali au kukamilisha jambo, unajua wazi kabisa uhalisia huwa hauendi kama ramani kwa asilimia 100. Hata kama ni ramani ya nyumba umechorewa vizuri, ukaipenda kweli kweli na ukawa na kiasi cha fedha cha kutosha kutekeleza kila kilichopo kwenye ramani, bado nyumba iliyokamilika haitafanana na ramani (more…)

2059; Ndoano Ya Kunasa Umakini…

By | August 20, 2020

Ukitaka kuvua samaki, unakuwa na ndoano ambayo unaiwekea chambo na kisha kuweka kwenye maji yenye samaki. Samaki akiwa kwenye pita pita zake za kutafuta chakula, anaona chakula kizuri, anakifuata, anakula na kujikuta amenasa kwenye ndoano na hapo anavuliwa. Ni kwa njia hiyo pia umakini wa watu umekuwa unashikwa, hasa mtandaoni. (more…)

2058; Siyo Ilivyo, Bali Ulivyo…

By | August 19, 2020

Kila mmoja wetu ni kama amevaa miwani ya rangi ambayo anaitumia kuiangalia dunia. Kama umewahi kuvaa miwani yenye rangi, unajua kila unachoangalia kitakuwa na rangi ya miwani hiyo. Hivyo siyo kwamba vitu hivyo vimebadilika rangi, bali miwani imekufanya uvione kwa rangi hiyo. Kila mmoja wetu ana miwani anayoitumia kuiangalia dunia, (more…)

2057; Vigezo Vitano Vya Kuzingatia Kwenye Kazi Au Biashara Unayotaka Kufanya Kwa Muda Mrefu…

By | August 18, 2020

Kuna biashara au kazi ambazo mtu unaweza kufanya kwa muda mfupi, ndani ya mwaka mmoja na kuachana nayo kwenda kwenye biashara nyingine. Biashara za aina hiyo huwa hazihitaji vigezo vingi, hapo unaangalia tu faida unayokwenda kupata. Halafu kuna biashara au kazi ambazo mtu unataka kufanya kwa muda mrefu, unapanga kufanya (more…)

2056; Linda Uhuru Wako Wa Mbeleni…

By | August 17, 2020

Kuna vitu unaweza kufanya sasa na usione madhara yake, lakini baadaye vinakuja kuwa kikwazo kikubwa kwako. Hivyo kwa kila unachotaka kufanya, angalia kwanza mbeleni kitakuathiri kiasi gani, angalia miaka 10, 20 mpaka 50 ijayo kisha ona kitakuwa na athari gani. Mambo mengi yanayokukwamisha sasa, ni matokeo ya kile ulichofanya kipindi (more…)

2055; Hakikisha Hukosi Hivi Viwili…

By | August 16, 2020

  Watu wengi hawajafanikiwa na wengi zaidi hawatafanikiwa kwa sababu wanakosa viungo viwili muhimu sana kwenye mafanikio ya aina yoyote ile. Kiungo cha kwanza ni msimamo, kufanya jambo kwa kurudia rudia bila ya kuacha. Hili linaonekana wazi, ukiangalia waliofanikiwa, huwa wamefanya kitu hicho kwa muda mrefu. Lakini waangalie walioshindwa, katika (more…)

2054; Watatuangalia Na Kucheka…

By | August 15, 2020

Mtu mmoja amewahi kusema kwamba kitu pekee tunachojifunza kwenye historia ni kwamba hatujifunzi kupitia historia. Ukiangalia hapa duniani, mambo ni yale yale, yamekuwa yanakuja kwa njia tofauti. Hivyo kama tungekuwa tunajifunza kupitia historia, tungeepuka kurudia makosa yanayotugharimu. Lakini hatujifunzi kupitia historia, ndiyo maana tunarudia makosa yale yale na yanatugharimu sana. (more…)

2053; Hatima Yako Haijapangwa, Unaipanga Mwenyewe Kila Siku…

By | August 14, 2020

Ukichukua mahindi na kuyaweka kwenye mashine ya kukoboa, yanatoka makande. Ukichukua mahindi hayo hayo na kuyaweka kwenye mashine ya kusaga, unapata unga. Umeanza na kitu kimoja lakini matokeo ni tofauti kwa sababu ya utofauti wa mashine. Hivyo pia ndivyo ilivyo kwenye maisha yetu, Kesho yako inategemea zaidi jinsi ulivyo leo. (more…)

2052; Unawafanyia Wengine, Kwa Ajili Yako…

By | August 13, 2020

Moja ya faida ya uandishi na ualimu ni moja, unaweza kufanya kwa ajili ya wengine, lakini wewe mwenyewe ukanufaika sana na kile unachowafanyia wengine. Unaandika kitu kwa ajili ya watu wengine, lakini katika uandishi wako, unapata njia za kukabiliana na hali fulani kwenye maisha yako mwenyewe. Au unajiandaa kwa ajili (more…)