Category Archives: KURASA ZA MAISHA

Kila siku mpya kwenye maisha yako ni sawa na ukurasa mpya wa kitabu.
Kwa kila siku mpya unachagua ufanye nini na maisha yako.
Kupitia makala hizi za KURASA ZA MAISHA, utajifunza mambo muhimu ya kufanya ili uwe namaisha bora zaidi.
Makala hizi za kurasa zinakujia kila siku.

2400; Kinachofanya mabadiliko kuwa magumu

By | July 27, 2021

2400; Kinachofanya mabadiliko kuwa magumu kwako… Ni kwa sababu unahangaika na kitu kisichokuwa sahihi. Unaweka juhudi zako eneo ambalo haliwezi kuzalisha mabadiliko. Unahangaika na matokeo badala ya kile kinachozalisha matokeo hayo. Unahangaika na matawi badala ya shina. Kama unataka kuyabadili maisha yako, usihangaike na yale matokeo unayopata sasa, bali hangaika (more…)

2399; Jenga nguvu ya ushindani…

By | July 26, 2021

2399; Jenga nguvu ya ushindani… Kama kuna vitu viwili vinavyofanana na ambavyo vipo sehemu moja, kimoja hakina umuhimu. Hivyo pia ndivyo ilivyo kwenye biashara. Kama kuna biashara mbili zinazofanana kwa kila kitu, moja siyo muhimu. Na kama biashara zinazofanana ni nyingi, nyingi pia zinakuwa siyo muhimu. Inakwenda hata kwenye kazi. (more…)

2398; Usibadili Maamuzi, Badili Mikakati…

By | July 25, 2021

2398; Usibadili Maamuzi, Badili Mikakati… Umeamua kwamba ni sahihi kwako kuingia kwenye biashara. Ni kitu ambacho umeona kinatoka ndani yako kweli. Umeiona fursa nzuri, Na unaona ndiyo njia ya uhakika ya kuishi kusudi lako na kuzifikia ndoto zako kubwa. Unaingia kwenye biashara ukiwa na hamasa kubwa. Unaona jinsi unakwenda kufanya (more…)

2397; Mambo ya kuzingatia unapokuwa juu…

By | July 24, 2021

2397; Mambo ya kuzingatia unapokuwa juu… Kila mtu anapenda kwenda juu, kufika kwenye kilele cha juu kabisa cha mafanikio. Lakini wengi huangalia upande mmoja tu wa kuwa juu, upande wa mazuri. Kuwa juu kuna upande wa mabaya yake, ambao unaambatana na changamoto mbalimbali. Ipo kauli inayosema kadiri unavyokwenda juu, ndivyo (more…)

2396; Mambo ya kufanya unapokuwa chini kabisa…

By | July 23, 2021

2396; Mambo ya kufanya unapokuwa chini kabisa… Safari ya maisha siyo barabara iliyonyooka. Ni njia yenye vilima, mabonde na kona nyingi. Kuna kupanda na kushuka, kwenda mbele na kurudi nyuma. Kila mtu anayapitia haya kwenye maisha kwa wakati wake na kwa viwango vinavyotofautiana. Mambo yanapokuwa mazuri, huwa tunajisahau na kudhani (more…)

2395; Tayari Una Taarifa Za Kutosha, Anza…

By | July 22, 2021

2395; Tayari Una Taarifa Za Kutosha, Anza… Kama kuna kitu unataka kuanza lakini unajiambia bado hujawa na taarifa za kutosha, jua unajidanganya tu. Hakuna sehemu rahisi kujificha kama kwenye kukusanya taarifa zaidi na kufanya tafiti. Kwa zama za mafuriko ya taarifa tunazoishi sasa, ni rahisi kuzama na kupotelea kwenye kutafuta (more…)

2394; Siyo Kweli…

By | July 21, 2021

2394; Siyo Kweli… Zoezi rahisi la kufanya leo. Andika kile unachokitaka sana kwenye maisha yako lakini bado hujakipata. Kisha orodhesha sababu zote kwa nini mpaka sasa hujakipata. Mbele ya kila sababu, andika ni uongo. Halafu tafuta walioweza kupata kitu hicho wakiwa na sababu unazojipa wewe. Kama unajiambia hujaanzisha biashara kwa (more…)

2393; Sifuri, Moja, Kumi, Mia na kuendelea…

By | July 20, 2021

2393; Sifuri, Moja, Kumi, Mia na kuendelea… Safari ya maili elfu moja huwa inaanza na hatua moja. Hii ni kauli maarufu sana kwenye mafunzo ya hamasa na mafanikio. Lakini imekuwa kauli rahisu kusema kuliko kuweka kwenye vitendo. Watu wengi hawana subira wanapoianza safari ya mafanikio. Wakiwaangalia waliofanikiwa, wanataka wawe kama (more…)

2392; Unavyojitengenezea Maumivu…

By | July 19, 2021

2392; Unavyojitengenezea Maumivu… Sehemu kubwa ya maumivu unayopitia kwenye maisha yako, huwa unayatengeneza wewe mwenyewe. Unafanya hivyo bila ya kujua. Hapa ni baadhi ya mambo ambayo umezoea kufanya ambayo yanakuweka kwenye hatari ya kupata maumivu. Kuwa na matarajio makubwa kwenye vitu usivyokuwa na udhibiti navyo. Kulazimisha matokeo ya aina fulani. (more…)

2391; Kutaka kupenda na kila mtu…

By | July 18, 2021

2391; Kutaka kupenda na kila mtu… Hakuna maisha magumu hapa duniani kama kutaka kila mtu akupende. Ni maisha magumu kwa sababu hata ujaribu kwa namna gani, huwezi kufanikiwa. Haijalishi unafanya nini, kuna watu wanachagua tu kukuchukia. Na hata kama unachofanya ni kizuri na chenye manufaa, bado wapo ambao hawatapenda namna (more…)