Category Archives: KURASA ZA MAISHA

Kila siku mpya kwenye maisha yako ni sawa na ukurasa mpya wa kitabu.
Kwa kila siku mpya unachagua ufanye nini na maisha yako.
Kupitia makala hizi za KURASA ZA MAISHA, utajifunza mambo muhimu ya kufanya ili uwe namaisha bora zaidi.
Makala hizi za kurasa zinakujia kila siku.

2390; Kipi Kibaya Zaidi Kinaweza Kutokea?

By | July 17, 2021

2390; Kipi Kibaya Zaidi Kinaweza Kutokea? Unapoweka mipango yako, huwa unaangalia mambo yakienda vizuri tu. Kama ni biashara, unangalia upande wa faida tu. Kama ni tabia unajijengea, unaangalia manufaa yake tu. Tunapenda sana mambo yaende vizuri, lakini hilo liko nje ya uwezo wetu. Kitu pekee tunachoweza kudhibiti ni juhudi unazoweka (more…)

2389; Usimwamini Yeyote Bila Ya Kitu Hiki…

By | July 16, 2021

2389; Usimwamini Yeyote Bila Ya Kitu Hiki… Edward Deming amewahi kunukuliwa akisema; “In God we trust, all others must bring data.” Akimaanisha Mungu pekee ndiye wa kumwamini, wengine wote lazima walete data. Ni kauli rahisi hii, lakini kama ukiielewa na kuiishi, lazima utapiga hatua kubwa kwenye maisha na kile unachofanya. (more…)

2388; Kwa nini ushauri mwingi wa mafanikio haufanyi kazi…

By | July 15, 2021

2388; Kwa nini ushauri mwingi wa mafanikio haufanyi kazi… Vitabu vilivyoandikwa kuhusu siri za mafanikio ni vingi sana. Hadithi za watu waliofanikiwa ni nyingi. Na mafunzo pamoja na ushauri wa mafanikio vimejaa kila kona. Lakini cha kushangaza, idadi ya wanaofanikiwa inabaki kuwa ni ndogo sana. Sababu kubwa ni moja, mafunzo (more…)

2386; Kama bado unajiuliza, jibu ni hapana…

By | July 13, 2021

2386; Kama bado unajiuliza, jibu ni hapana… Hakuna siku unaamka asubuhi na kujiuliza kama uko hai au la, kama uko hai unajua uko hai. Vitu unavyojua kwa hakika kwenye maisha yako huwa hujiulizi ulizi kila wakati, tayari majibu unayo. Hilo lipeleke kwenye kila eneo la maisha yako, ukiona bado unajiuliza (more…)

2385; Kula na Kumeng’enya…

By | July 12, 2021

2385; Kula na Kumeng’enya… Unapokula chakula, hakiingii moja kwa moja kwenye mwili wako kama ulivyokila. Badala yake kinameng’enywa kwanza, kinavunjwa kwenye vipande vidogo vidogo na kisha kufyonzwa kwenye mwili. Hivyo pia ndivyo ilivyo kwenye kusoma. Kusoma ni kama kula, unachosoma siyo kinachoingia kwenye akili yako, bali kile unachochakata. Hivyo usifurahie (more…)

2384; Sababu na visingizio…

By | July 11, 2021

2384; Sababu na visingizio… Kuna vitu huwa unapanga au kupenda kufanya, lakini unashindwa kukamilisha kama ulivyopanga. Huwa unatoa sababu mbalimbali kwa nini umeshindwa kufanya au kupata unachotaka. Lakini kiukweli kabisa nyingi unazotoa siyo sababu, bali ni visingizio. Sababu ni vile vikwazo au changamoto za kweli kabisa, ambazo zinamzuia kila mtu. (more…)

2383; Furahia Kupitwa…

By | July 10, 2021

2383; Furahia Kupitwa… Mitandao ya kijamii imekuwa inakunasa kwenye uraibu kwa kukufanya uone kama unapitwa. Sisi binadamu tunahofia sana kupitwa na yale muhimu, maana kutokupitwa ndiyo kuliwawezesha watangulizi wetu kuepuka hatari mbalimbali na kuweza kuendeleza kizazi cha binadamu hapa duniani. Kipindi cha nyuma ilikuwa hatari sana kwa mtu kukaa na (more…)

2381; Ubahili ulio sahihi…

By | July 8, 2021

2381; Ubahili ulio sahihi… Siri ya utajiri ni ubahili, hiyo iko wazi na inajulikana na wengi. Lakini ubahili umekuwa unachukuliwa kwa mtazamo hasi, kama kujinyima na kuyafanya maisha kuwa magumu. Ubahili ni kuhakikisha matumizi yako hayazidi kipato chako. Na zipo njia za kuufanya ubahili kwa usahihi, ambapo maisha yako yatakwenda (more…)