Category Archives: KURASA ZA MAISHA

Kila siku mpya kwenye maisha yako ni sawa na ukurasa mpya wa kitabu.
Kwa kila siku mpya unachagua ufanye nini na maisha yako.
Kupitia makala hizi za KURASA ZA MAISHA, utajifunza mambo muhimu ya kufanya ili uwe namaisha bora zaidi.
Makala hizi za kurasa zinakujia kila siku.

2410; Hupati Muda…

By | August 6, 2021

2410; Hupati Muda… Kama unajiambia ukipata muda utafanya kitu, jua ni njia tu ya kujifanganya. Ukweli unaopaswa kujiambia ni kitu hicho siyo muhimu sana kwako na hivyo hakipaswi kuwa kipaumbele cha kwanza kwako. Maana kitu kinapokuwa muhimu kabisa huwa hatusubiri mpaka tupate muda, badala yake tunatenga muda. Hivyo acha kujidanganya, (more…)

2409; Mwanzo wa mwisho na mwisho wa mwanzo…

By | August 5, 2021

2409; Mwanzo wa mwisho na mwisho wa mwanzo… Rafiki, Nataka kusema na wewe leo kuhusu kuanza. Huwa kuna kauli ya Kiswahili inayosema mwanzo ni mgumu. Lakini kwenye safari ya mafanikio hakuna kitu rahisi kama kuanza. Najua ulishaanza mambo mengi mno, lakini hukuyafanya kwa muda mrefu. Ni pale ulipokutana na ugumu (more…)

2408; Kila kitu ni rasilimali…

By | August 4, 2021

2408; Kila kitu ni rasilimali… Moto mkali unapokuwa unawaka, chochote kitakachowekwa kwenye moto huo hugeuka kuwa nishati ya kuuchochea zaidi. Hata ukimwaga maji kwenye moto ambao ni mkali, unakuwa kama ni mafuta, yanachochea zaidi moto huo. Hivyo ndivyo unapaswa kuyafanya maisha yako kuwa, tumia kila unachopitia au kukutana nacho kama (more…)

2406; Unachoona na usichoona…

By | August 2, 2021

2406; Unachoona na usichoona… Umewahi kuangalia tangazo au mafunzo ya kitu kwenye tv au mtandaoni, ukatoka na kwenda kujaribu kufanya kama ulivyojifunza? Kama ndiyo mara ya kwanza kufanya kitu hicho, utakuwa ulipata matokeo ya tofuati kabisa na uliyoyaona, hata kama umefanya kila ulichoelekezwa. Hiyo ni kwa sababu unachoona ni matokeo (more…)

2404; Nyenzo Muhimu Za Kujijengea Kwenye

By | July 31, 2021

2404; Nyenzo Muhimu Za Kujijengea Kwenye Maisha… Ni Mwanasayansi Archimedes aliyesema nipe mtarimbo mrefu na mahali pa kuuegemeza na nitaweza kuisogeza dunia. Alisema hayo kwa kujua nguvu ya nyezo, ambapo nguvu kidogo inaweza kuleta matokeo makubwa mno. Unatumia nyenzo kwenye shughuli zako za kawaida. Kung’oa msumari kwenye mbao siyo rahisi (more…)

2403; Itumie hiyo nguvu isikuumize…

By | July 30, 2021

2403; Itumie hiyo nguvu isikuumize… Kipindi cha nyuma kidogo huko Moshi kilianzishwa kiwanda cha pombe iliyoitwa Banana. Ni pombe kali iliyotengenezwa na ndizi. Ilikuwa mwenye duka anapoenda kununua, mpaka anafikisha dukani, kwenye kreti chumba mbili mpaka tatu zinapasuka zenyewe. Wakati wa kufungua pombe hiyo ilipaswa kufanywa taratibu la sivyo ilimwagika (more…)

2402; Kuna watu watakuona takataka…

By | July 29, 2021

2402; Kuna watu watakuona takataka… Kitu kimoja muhimu sana unachopaswa kukijua kwenye safari yako ya mafanikio, na ambacho kitapunguza sana makali ya safari hiyo kwako ni hiki; haijalishi unafanya nini, kuna watu watakuona wewe ni takataka kabisa. Wataona ni mtu usiyefaa na dunia ingekuwa bora kama usingekuwepo kabisa. Kwa kuwa (more…)

2401; Hisia, Hadithi, Mantiki…

By | July 28, 2021

2401; Hisia, Hadithi, Mantiki… Hivyo ni vitu vitatu tunavyotumia katika kufanya maamuzi yote kwenye maisha yetu. Huwa tunadhani tunafanya maamuzi kwa mantiki, kisha kuyajengea hadithi na kuwa na hisia nayo. Lakini sivyo tunavyofanya. Huwa tunafanya maamuzi kwa hisia kwanza, kisha tunatengeneza hadithi inayotetea maamuzi hayo na mwisho ndiyo tunatafuta mantiki (more…)