Category Archives: KURASA ZA MAISHA

Kila siku mpya kwenye maisha yako ni sawa na ukurasa mpya wa kitabu.
Kwa kila siku mpya unachagua ufanye nini na maisha yako.
Kupitia makala hizi za KURASA ZA MAISHA, utajifunza mambo muhimu ya kufanya ili uwe namaisha bora zaidi.
Makala hizi za kurasa zinakujia kila siku.

2330; Nguzo Tano Za Kujijenga Binafsi…

By | May 18, 2021

2330; Nguzo Tano Za Kujijenga Binafsi… Umekuwa unasikia sana ushauri wa kwamba kama unataka kufanikiwa kwenye maisha basi unapaswa kuwa wewe, unapaswa kuwa halisi kwako na siyo kuiga maisha ya wengine. Kwa wengi ushauri huo huwa unaishia kuwachanganya badala ya kuwasaidia. Hapa tunakwenda kujifunza nguzo tano za kujijenga binafsi. Kwa (more…)

2329; Kanuni ya kipato…

By | May 17, 2021

2329; Kanuni ya kipato… Kitapo unachoingiza kinatokaba na kanuni ya kisayansi ambayo ukiielewa na kuifanyia kazi, utaweza kukuza sana kipato chako. Kanuni hiyo ina vitu vinne muhimu sana. Kitu cha kwanza ni uhitaji wa kile ambacho unafanya. Kama unachofanya au kuuza ni hitaji la msingi la watu, watasukumwa kuja kulipata (more…)

2328; Vyanzo viwili vya msongo…

By | May 16, 2021

2328; Vyanzo viwili vya msongo… Huwa tunapatwa na msongo au kwa lugha nyingine kuvurugwa pale nambo yanapokwenda tofauti na tulivyotegemea. Ni rahisi kuona kilichosababisha msongo kwako ni kile kilichotokea. Lakini hiyo siyo kweli. Kinachokusababishia msongo ni namna unavyopokea kile kilichotokea. Kwa wengi hupokea kwa aina mbili na hizo ndiyo huwa (more…)

2327; Hatua tano za masoko…

By | May 15, 2021

2327; Hatua tano za masoko… Masoko ni sehemu muhimu ya biashara yoyote ambayo mtu anafanya. Bila masoko hakuna wateja na bila wateja hakuna mauzo. Bila mauzo hakuna faida na bila faida hakuna biashara. Hivyo unaweza kuona jinsi masoko yalivyo kiuongo muhimu kwenye biashara. Wengi wanashindwa kwenye biashara kwa sababu hawana (more…)

2324; Maarifa Na Hekima…

By | May 12, 2021

2324; Maarifa Na Hekima… Huwezi kuwa na hekima bila ya kuwa na maarifa, lakini unaweza kuwa na maarifa usiwe na hekima. Maarifa ni kujua vitu vingi, hekima ni kujua jinsi ya kutumia maarifa hayo. Maarifa unayapata, ila hekima unaishi. Maarifa yanakusanywa, ila hekima inanolewa. Unaweza kuyapoteza maarifa lakini hekima inadumu (more…)

2323; Mambo ya kuzingatia wakati wa mabadiliko

By | May 11, 2021

2323; Mambo ya kuzingatia wakati wa mabadiliko magumu… Kila mtu huwa anapitia kipindi cha mabadiliko magumu kwenye maisha yake. Ni katika vipindi hivyo ndipo wanaofanikiwa na wanaoshindwa wanapotengana. Wanaofanikiwa wanavitumia vipindi vya mabadiliko vizuri, huku wanaoshindwa wakivitumia vibaya. Haya ni mambo muhimu ya kuzingatia wakati wa mabadiliko magumu ili yakupeleke (more…)

2322; Hekima mpya na upumbavu mpya…

By | May 10, 2021

2322; Hekima mpya na upumbavu mpya… Watu wenye hekima wa vizazi vyote wamekuwa wakisema mambo yale yale. Na hayo ndiyo mambo sahihi ambaye yeyote akiyazingatia anakuwa na maisha bora. Hakuna hekima mpya ni zile zile ila zinaboreshwa kuendana na kizazi husika. Kujijua wewe mwenyewe, kuishi kusudi la maisha yako, kuwatendea (more…)

2321; Usiyazungushe maisha…

By | May 9, 2021

2321; Usiyazungushe maisha… Maisha ni magumu tayari, hivyo usiyafanye kuwa magumu zaidi ya halivyo. Usiyazungushe sana maisha kwa vitu ambavyo viko wazi kabisa. Kama kuna kitu unakitaka, kitake kweli na weka wazi kwamba unakitaka. Usilete michezo au mitego ukitaka wengine waweze kusoma mawazo yako wajue unataka nini. Wewe ndiye wa (more…)