Category Archives: SHERIA ZA SIKU

#SheriaYaLeo (133/366); Kuwa makini na wema unaoonyeshwa.

By | March 13, 2022

#SheriaYaLeo (133/366); Kuwa makini na wema unaoonyeshwa. Mara nyingi watu hukazana kuonyesha wema fulani kwa nje ili waonekane wanafanya kwa manufaa ya wengine. Lakini ndani yao wanakuwa wameficha sababu halisi ambayo ni kujinufaisha wao wenyewe zaidi. Kuwa makini sana na wema unaoonyeshwa kwa nguvu kubwa, kwa sababu unakuwa umeficha ulaghai (more…)

#SheriaYaLeo (132/366); Angalia tabia wanazoficha.

By | March 12, 2022

#SheriaYaLeo (132/366); Angalia tabia wanazoficha. Katika kuchagua watu wa kushirikiana nao, huwa tunaamini haraka kile ambacho tunasikia na kuona kwao. Tunaamini hivyo ndivyo watu walivyo na yale wanayotuambia na kutuonyesha ndiyo uhalisia wao. Tunachosahau ni kila mtu kuna tabia anazo ambazo huwa hapendi kuziweka wazi. Huenda hata yeye mwenyewe hajui (more…)

#SheriaYaLeo (131/366); Usichanganye kujiamini kulikopitiliza na ukweli.

By | March 11, 2022

#SheriaYaLeo (131/366); Usichanganye kujiamini kulikopitiliza na ukweli. Sisi binadamu huwa tunadanganyika kirahisi sana. Pale mtu anapotueleza kitu kwa kujiamini sana, huwa tunaona ni ukweli, kwamba kama isingekuwa kweli basi wasingejiamini. Hii ndiyo njia wanayotumia matapeli na watu wengine wenye lengo la kudanganya na kuhadaa kwa manufaa yao. Huwa wanaeleza jambo (more…)

#SheriaYaLeo (130/366); Tambua mlipuko wa kihisia.

By | March 10, 2022

#SheriaYaLeo (130/366); Tambua mlipuko wa kihisia. Pale mtu anapopata mlipuko mkali wa kihisia dhidi yako, mfano hasira ambayo haiendani na kile ulichofanya, tambua ni mbinu ya kutaka kukutawala kihisia. Wapo watu ambao hutumia mlipuko wa hisia kuibua hisia kali ndani yako ili waweze kukutawala. Wanajua ukishakuwa na hisia kali, huwezi (more…)

#SheriaYaLeo (129/366); Angalia mapito yao.

By | March 9, 2022

#SheriaYaLeo (129/366); Angalia mapito yao. Kiashiria kizuri cha tabia za watu ni mapito yao. Kwa kuangalia historia zao na yale ambayo wamefanya huko nyuma, unaweza kupata picha ni watu wa aina gani. Watu wanaweza kusema wamejifunza na kubadilika kutokana na yale waliyopitia, lakini siyo rahisi hivyo. Kuna tabia huwa zinaendelea (more…)

#SheriaYaLeo (128/366); Wanaotumia udhaifu kukutawala.

By | March 8, 2022

#SheriaYaLeo (128/366); Wanaotumia udhaifu kukutawala. Kuna watu huwa wanatumia udhaifu walionao kukutawala wewe bila ya mwenyewe kujua. Wanakuwa na tabia fulani sugu ambayo inakukwamisha wewe, lakini unapojaribu kuwakabili kwenye tabia hiyo wanajionyesha hawana hatia na wewe ni mtu mbaya na usiyejali. Wanaweza kuwa na tabia sugu ya kuchelewa kila wakati. (more…)

#SheriaZaLeo (127/366); Unachoona siyo uhalisia.

By | March 7, 2022

#SheriaZaLeo (127/366); Unachoona siyo uhalisia. Watu huwa wanatumia mwonekano wa nje kuwahadaa wengine. Pale wanapokuwa na udhaifu fulani, huwa wanatengeneza mwonekano unaoficha udhaifu huo. Lengo lao ni kuwanasa wengine kwa namna ambayo wao watanufaika zaidi. Wewe kuwa makini usinase kwenye mitego huo. Jua siyo kila unachoona kwa nje ndiyo uhalisia (more…)

#SheriaYaLeo (126/366); Kuwa makini na watu unaowachokoza.

By | March 6, 2022

#SheriaYaLeo (126/366); Kuwa makini na watu unaowachokoza. Watu huwa wanabadilika, hakuna anayebaki pale alipoanzia. Mtu anaweza kuwa chini leo, lakini siku zijazo akawa juu kabisa. Hivyo kuwa makini sana na watu unaowachokoza, kuwadharau au kuwatukana. Leo anaweza asiwe na nguvu ya kukufanya chochote, lakini siku zijazo akawa na nguvu na (more…)

#SheriaYaLeo (125/366); Usidanganyike na mwonekano wa nje.

By | March 5, 2022

#SheriaYaLeo (125/366); Usidanganyike na mwonekano wa nje. Mara nyingi watu wamekuwa wanatengeneza mwonekano fulani wa nje ambao unaficha nia yao halisi. Kwa nje wanaigiza kama wajinga na wasiojua vitu fulani. Lengo lao ni kuwahadaa watu ili wasijue nia zao na kuwa kikwazo kwao. Wewe kuwa makini, usikimbilie kuamini mwonekano wa (more…)

#SheriaYaLeo (124/366); Wahukumu kwa tabia zao, siyo maneno yao.

By | March 4, 2022

#SheriaYaLeo (124/366); Wahukumu kwa tabia zao, siyo maneno yao. Kwenye safari yako ya mafanikio na maisha kwa ujumla, jifunze kutokudanganyika na maneno ambayo watu wanakuambia, badala yake angalia tabia wanazokuonyesha. Watu husema maneno ya kila aina na kujaribu kuficha nia zao halisi kwa maneno mazuri. Lakini matendo yao huwa hayadanganyi, (more…)