Category Archives: SHERIA ZA SIKU

#SheriaYaLeo (143/366); Tambua uimara wa tabia za watu.

By | March 23, 2022

#SheriaYaLeo (143/366); Tambua uimara wa tabia za watu. Tabia za watu zina nguvu kubwa kwenye maisha yao. Mtu mwenye tabia dhaifu, itadhoofisha hata sifa nyingine alizonazo. Kwa mfano mtu mwenye akili sana lakini mwenye tabia dhaifu, anaweza kuja na mawazo mzuri sana na hata kufanya kazi bora. Lakini wanapokutana na (more…)

#SheriaYaLeo (142/366); Kuridhisha kulikopitiliza.

By | March 22, 2022

#SheriaYaLeo (142/366); Kuridhisha kulikopitiliza. Kuna watu ambao ni rahisi sana kukubaliana na wewe pale unapokutana nao. Wanatabasamu sana, wana shauku kubwa na wanakuwa tayari kukusaidia kwa lolote. Hilo linakufanya uwaone ni watu sahihi kwako na kuwakubali kwenye maisha yako. Wanakuwa ni watu wanaokuridhisha na hivyo unawapa fursa mbalimbali kwenye maisha (more…)

#SheriaYaLeo (141/366); Wajue sitaki nataka.

By | March 21, 2022

#SheriaYaLeo (141/366); Wajue sitaki nataka. Kuna watu ambao kwa nje wanajifanya kama hawakitaki kitu, ila kwa ndani wanakitaka sana. Kwa nje wanakikataa, ila ni kwa lengo la kuwafanya watu wawabembeleze ndiyo wakubali. Watu hao wanakuwa wanajua tabia ya binadamu, kwamba ukionekana unataka sana kitu, watu wanakuzuia usikipate. Au hata ukikipata (more…)

#SheriaYaLeo (140/366); Kutaka usawa kwa kila mtu.

By | March 20, 2022

#SheriaYaLeo (140/366); Kutaka usawa kwa kila mtu. Njia nyingine ambayo hutumiwa sana na wale wanaotaka mamlaka bila ya kuonekana wazi wazi ni kutaka usawa kwa kila mtu. Hapa husisitiza kila mtu ni sawa na lazima watu wote wachukuliwe kwa usawa. Hukazana kuwaaminisha wengine kwamba uwezo, uimara na hadhi tofauti za (more…)

#SheriaYaLeo (139/366); Angalia nyuma ya barakoa.

By | March 19, 2022

#SheriaYaLeo (139/366); Angalia nyuma ya barakoa. Kunbuka kwa kawaida watu huwa wanatengeneza mwonekano fulani wanaotaka dunia ione. Hivyo kila mtu ni kama amevaa barakoa, akionyesha kile ambacho anataka wengine waone na kuficha nia kuu aliyonayo. Mtu anaweza kuwa na uso wa tabasamu na maneno mazuri kabisa. Hii ni barakoa inayowafanya (more…)

#SheriaYaLeo (138/366); Tambua Kivuli Cha Watu.

By | March 18, 2022

#SheriaYaLeo (138/366); Tambua Kivuli Cha Watu. Kwenye safari yako ya maisha utakutana na watu ambao wanatumia nguvu kubwa kuonyesha tabia fulani nzuri kwa nje. Inaweza kuwa ni huruma iliyopitiliza, kujali sana, kuonekana watakatifu au imara sana. Lakini pale unapowajua watu hao kwa undani, unaona kuna kivuli kipo nyuma ya tabia (more…)

#SheriaYaLeo (137/366); Tambua Wanaojificha nyuma ya jadi.

By | March 17, 2022

#SheriaYaLeo (137/366); Tambua Wanaojificha nyuma ya jadi. Wapo watu ambao wanataka kuleta mabadiliko ya aina fulani. Lakini wanajua jamii huwa haipo tayari kwa mabadiliko makubwa na ya haraka. Hivyo hujificha nyuma ya jadi, kwa kujionyesha kwamba ni watu ambao wanadumisha jadi. Wanatumia nguvu nyingi kuonekana wanakubali mfumo uliopo na wanaulinda (more…)

#SheriaYaLeo (136/366); Zawadi za kimtego.

By | March 16, 2022

#SheriaYaLeo (136/366); Zawadi za kimtego. Watu wenye hila ya kupata kitu fulani, huwa wanapenda kuficha nia yao kwenye kitu kingine ili wasionekane waziwazi. Moja ya maeneo ambayo watu wanaotaka kujinufaisha kupitia wengine ni utoaji zawadi. Watu hao huwa wanatoa zawadi za kimtego. Wanachofanya ni kumpa mtu zawadi ndogo, halafu baadaye (more…)

#SheriaYaLeo (135/366); Wajue viongozi wanaopenda kutukuzwa.

By | March 15, 2022

#SheriaYaLeo (135/366); Wajue viongozi wanaopenda kutukuzwa. Katika safari yako ya maisha na mafanikio utapita maeneo mbalimbali. Kwenye baadhi ya maeneo utakutana na viongozi ambao wanapendwa kutukuzwa. Viongozi hao huamini hawawezi kukosea. Huona kila wanachofikiri wao ndiyo sahihi zaidi na wengine wote wanakubaliana nao. Kufikiri tofauti na wao wanachukulia kama usaliti (more…)

#SheriaYaLeo (134/366); Watambue wenye majigambo kabla hawajakunasa.

By | March 14, 2022

#SheriaYaLeo (134/366); Watambue wenye majigambo kabla hawajakunasa. Watu wenye majigambo yaliyopitiliza (Narcissists) ni watu ambao ndani yao hawajiamini. Wanatumia majigambo hayo kuficha udhaifu huo mkubwa ulio ndani yao. Watu hao huwa wanajiona wao ni muhimu kuliko watu wengine na hivyo hutaka watu wote wawatii wao. Huwa wanataka kila mtu awe (more…)