#SheriaYaLeo (37/366); Jichukulie Kama Mjenzi.

By | December 7, 2021

#SheriaYaLeo (37/366); Jichukulie Kama Mjenzi. Haijalishi upo kwenye tasnia gani, unapaswa kufikiri na kujichukulia kama mjenzi. Wewe ni mjenzi unayetumia rasilimali na mawazo mbalimbali kutengeneza kitu chenye manufaa kwa wengine. Kujenga kitu chochote vizuri, iwe ni nyumba, taasisi, biashara au kazi ya sanaa, ni lazima uuelewe mchakato wa ujenzi na (more…)

ONGEA NA KOCHA; Kupata Hamasa Isiyoisha, Kitabu cha Four Thousand Weeks na Mahojiano na Regina Panga.

By | December 6, 2021

Karibu mwanamafanikio kwenye kipindi hiki cha ONGEA NA KOCHA. Kwenye kipindi hiki unakwenda kujifunza mengi kwa kina kama ifuatavyo. Kwenye somo la juma tunajifunza jinsi ya kupata hamasa isiyoisha ili uweze kuyafanyia kazi malengo yako bila kurudi nyuma. Hapa utajifunza hatua tano za kuchukua kwenye kila siku yako ili kuchochea (more…)

2532; Ngumu Ndiyo Sahihi.

By | December 6, 2021

2532; Ngumu Ndiyo Sahihi. Kwa zama tulizopo sasa, mambo tunayokabiliana nayo ni mengi kiasi kwamba kufanya maamuzi ni zoezi gumu kidogo. Kuna taarifa nyingi za kupitia katika kufanya maamuzi yako. Lakini muda wa kuzipitia zote ndiyo huna. Kuvuka hilo, unahitaji kujijengea njia za mkato za kufikia maamuzi kwa haraka. Japo (more…)

#SheriaYaLeo (36/366); Kusanya Ujuzi Mwingi.

By | December 6, 2021

#SheriaYaLeo (36/366); Kusanya Ujuzi Mwingi. Lengo lako kuu kwenye mafunzo unayoyapata ni kujifunza na kukusanya ujuzi mwenye kwenye yale maeneo yanayokuvutia na kukuhamasisha. Kama baadaye mambo yatabadilika na kulazimika kubadili kazi au biashara unayofanya, ujuzi mwingi uliojijengea unakupa fursa ya kufanya hivyo. Lakini pia utakuwa tayari unajua jinsi ya kujifunza (more…)

2531; Usijipe umuhimu usiokuwa nao.

By | December 5, 2021

2531; Usijipe umuhimu usiokuwa nao. Ndiyo, wewe ni mtu muhimu sana kwako, mtu wa kipekee, mwenye uwezo mkubwa mno. Hayo yote yako ndani yako tayari. Lakini unashindwa kuyatumia kwa sababu unajipa umuhimu kupitiliza, umuhimu usiokuwa nao. Pale unapodhani kwamba dunia inapaswa kwenda kwa matakwa yako wewe unajidanganya sana. Kwa sababu (more…)

#SheriaYaLeo (35/366); Thamini kujifunza kuliko

By | December 5, 2021

#SheriaYaLeo (35/366); Thamini kujifunza kuliko mengine yote. Kadiri unavyopiga hatua kwenye maisha yako, utasukumwa kutafuta fursa zinazokuingizia kipato kikubwa zaidi ili kuweza kuendana na hali ya maisha. Hilo litakusukuma kutafuta kazi au biashara ambayo inakulipa vizuri zaidi. Kwa bahati mbaya sana, unapopata kile kinacholipa zaidi, huwa hakina fursa za kujifunza (more…)

2530; Mnyoo Mjinga.

By | December 4, 2021

2530; Mnyoo Mjinga. Kwenye baiolojia kuna dhana kwamba mnyoo (parasite) mwenye akili anahakikisha kiumbe anayemtegemea hafi. Hivyo hata kama anamnyonya virutubisho mbalimbali, anahakikisha hachukui kila kitu mpaka kupelekea afe. Hiyo ni kwa sababu kama kiumbe ambaye mnyoo anamtegemea atakufa, basi na yeye atakufa pia. Hivyo tunaweza kusema mnyoo ambao unamuua (more…)

#SheriaYaLeo (34/366); Lengo Kuu Moja.

By | December 4, 2021

#SheriaYaLeo (34/366); Lengo Kuu Moja. Unapochagua kufanya kazi chini ya mtu ambaye amebobea ili ujifunze kwake, lengo lako kuu ni kujifunza na siyo kulipwa vizuri au kupata hadhi kubwa. Unachohitaji ni kujijengea ujuzi bora na wa kipekee, ambao utaweza kuutumia kufanya makubwa kwenye maisha yako. Unapokuwa kijana na ndiyo unaanza (more…)

2529; Mrefu halafu mfupi.

By | December 3, 2021

2529; Mrefu halafu mfupi. Kwenye ukurasa uliopita (2528), tumejifunza tamaa ya kutaka vingi kwa pamoja inavyokuwa kikwazo kwa wengi kufanya maamuzi. Watu wanachelewa kufanya maamuzi kwa sababu hawataki kukosa fursa nzuri zinazoweza kujitokeza baadaye na hilo linakuwa kikwazo kwao. Huo ni upande mmoja ambao watu wamekuwa wanatumia kukwepa kufanya maamuzi. (more…)

#SheriaYaLeo (33/366); Anachohitaji Menta.

By | December 3, 2021

#SheriaYaLeo (33/366); Anachohitaji Menta. Ili kujifunza kwa vitendo na uhalisia, unahitaji mtu ambaye tayari ameshafanikiwa kwenye kile unachotaka kufanikiwa ili awe menta wako. Ni kupitia menta huyo ndiyo utajifunza kwa uzoefu ambao yeye ameupitia mpaka kufika alipofika. Atakusaidia kuepuka makosa ambayo yeye alifanya ili usijicheleweshe. Ni muhimu sana kumpata aliyefanikiwa (more…)