2528; Kutaka vingi kwa pamoja.

By | December 2, 2021

2528; Kutaka vingi kwa pamoja. Hadithi tulizokuwa tunajifunza utotoni zilikuwa na masomo makubwa sana kuhusu maisha. Lakini kwa bahati mbaya sana tumekuwa hatuzipi uzito na hivyo kufanya makosa ambayo hadithi hizo zilikuwa zinatuasa tuyaepuke. Chukua hadithi ya sungura kualikwa kwenye sherehe mbili. Kwa ulafi wake akapanga asikose vyote. Hivyo akawa (more…)

#SheriaYaLeo (32/366); Jifunze kwa kufanya.

By | December 2, 2021

#SheriaYaLeo (32/366); Jifunze kwa kufanya. Ulipokuwa mdogo, wazazi na jamii ilikufundisha mambo mengi kuhusu maisha kupitia maelekezo na mifano. Ulipoenda shule ukafundishwa mambo mengine mengi kuhusu kazi na biashara kupitia maelekezo na mifano. Unapoingia kwenye dunia ya uhalisia, katika kuyaishi maisha na kufanya kazi au biashara, ndiyo unagundua yale uliyojifunza (more…)

2527; Kila suluhisho ni tatizo.

By | December 1, 2021

2527; Kila suluhisho ni tatizo. Kwenye maisha huwa tunapitia matatizo na changamoto mbalimbali. Hilo hutusukuna kutafuta suluhisho ili maisha yetu yaweze kwenda vile tunavyotaka. Tunachosahau au ambacho tunakuwa hatujui wakati tunatafuta suluhisho ni kwamba kila suluhisho huwa lina tatizo ndani yake. Ndiyo ni suluhisho la tatizo ambalo unalo, lakini ndani (more…)

#SheriaYaLeo (31/366); Chanzo cha nguvu zote.

By | December 1, 2021

#SheriaYaLeo (31/366); Chanzo cha nguvu zote. Usijaribu kuikwepa kazi ya kugundua kusudi na wajibu wa maisha yako kwa kudhani vitakuja kwako vyenyewe. Japo inaweza kutokea hivyo kwa baadhi ya watu, kuweza kujua kusudi na wajibu wa maisha yao mapema na kwa matukio ya kipekee, kwa wengj wetu hilo linahitaji kazi (more…)

2526; Mtego wa mateso.

By | November 30, 2021

2526; Mtego wa mateso. Haya maisha huwa yana mitego ya mateso ambayo usipoijua utaishi maisha ya kuteseka sana. Mitego hii haijaanza sasa, wanafalsafa wa kale waliielewa sana na wakawa na mafunzo ya kuwatahadharisha watu. Kuna mifano mikubwa miwili ya mafunzo ya kale yanayoonyesha mitego hii. Wa kwanza ni Promethus ambaye (more…)

#SheriaYaLeo (30/366); Amini kwenye mchakato.

By | November 30, 2021

#SheriaYaLeo (30/366); Amini kwenye mchakato. Unapoanza kufanya kitu chochote kile kipya kwako, unakutana na ugumu mkubwa. Unakua hujui mambo mengi kuhusu kitu hicho na hivyo unasumbuka sana mwanzoni. Unaweza kukata tamaa kwa kuona vitu ni vingi na vigumu, huwezi kupambana navyo. Kama utakata tamaa, utakuwa umeishia hapo na kushindwa kufikia (more…)

ONGEA NA KOCHA; Wewe Ni Mshindi, Third Door na Ernest Paschal.

By | November 29, 2021

Karibu mwanamafanikio kwenye kipindi cha juma cha ONGEA NA KOCHA. Kwenye kipindi hiki unakwenda kupata yafuatayo; Moja ni somo la wewe ni mshindi, ambapo nimekushirikisha kwa kina namna ya kufikiri kama mshindi, kufuta kabisa mbadala na kupambana mpaka ufanikiwe. Mbili ni uchambuzi wa kitabu cha Third Door ambapo mwandishi ameshirikisha (more…)

2525; Mbadala Ndiyo Unaokuponza.

By | November 29, 2021

2525; Mbadala Ndiyo Unaokuponza. Kadiri unavyokuwa na machaguo mengi, ndivyo inavyokuwa vigumu kwako kuchukua hatua. Pale unapokuwa na mbadala wa chochote unachofanya, ukikutana na ugumu utakimbilia kwenye mbadala huo. Hiki ni kikwazo kikubwa kwa mafanikio ya wengi, kuwa na mbadala kunawafanya wasikomae na kitu kimoja mpaka wakapata matokeo makubwa. Kujua (more…)

#SheriaYaLeo (29/366); Kuwa jinsi ulivyo.

By | November 29, 2021

#SheriaYaLeo (29/366); Kuwa jinsi ulivyo. Unapaswa kuwa jinsi ulivyo kwa kujifunza wewe ni mtu wa aina gani, kisha kuwa mtu huyo. Ulizaliwa na uwezo, tabia na vipaji vya kipekee ambavyo vinakutofautisha na wengine na kujenga hatima yako. Hivyo ndivyo ulivyo ndani yako. Ni kwa kuishi huo upekee wako ndiyo unaweza (more…)

2524; Pesa ziko wapi?

By | November 28, 2021

2524; Pesa ziko wapi? Wahenga walisema, mali bila daftari, hutumika bila habari. Kama hutunzi vizuri kumbukumbu zako za kila senti inayoingia na kutoka, hutajua pesa zako zinapotelea wapi. Utaona tu umeshika pesa nyingi, lakini hujui zimeenda wapi. Na hapo ndipo wengi huamini kuna chuma ulete, hali ya ushirikina ambapo fedha (more…)