#TAFAKARI YA LEO; KAMA HAKIKUI, KUNA TATIZO…

By | July 4, 2021

Kama kitu kimezaliwa au kuanzishwa, kinapaswa kukua. Kama hakuna ukuaji maana yakr kuna tatizo, kuna kikwazo kinachozuia kitu hicho kisikue. Wajibu wako ni kujua tatizo au kikwazo kiko wapi, kukifanyia kazi ili kitu kiweze kukua. Na ili ujue kama kitu kinakua au la, lazima uwe na njia ya kukipima. Bila (more…)

2376; Vinavyozuia Biashara Kukua…

By | July 3, 2021

2376; Vinavyozuia Biashara Kukua… Kwa asili, kitu chochote kinachozaliwa kinapaswa kukua. Na kama hakikui basi kuna sababu, kuna kitu kinazuia. Kama mtoto amezaliwa na hakui, haongezeki uzito, hukai na kuridhika, lazima ujue sababu ni nini na kuchukua hatua. Hivyo ndivyo inavyopaswa kuwa kwenye biashara pia. Biashara inapoanzishwa, inapaswa kukua. Kama (more…)

#TAFAKARI YA LEO; IFANYE KAZI HII NGUMU….

By | July 3, 2021

Kwa kawaida huwa hatupendi kufanya vitu vigumu, badala yake tunakimbilia kwenye vitu rahisi. Sasa kwa kuwa vitu rahisi kila mtu anafanya, vinakosa thamani na inakuwa vigumu kufanikiwa. Moja ya kazi ngumu ambayo huwa tunaitoroka ni kufikiri na akili zetu huwa zinatafuta kila aina ya sababu ili tu tusifikiri mambo magumu. (more…)

2375; Ni Mapendekezo, Siyo Amri…

By | July 2, 2021

2375; Ni Mapendekezo, Siyo Amri… Mawazo mengi yanayokuja kwenye akili yako huwa ni mapendekezo na siyo amri. Ni maoni na siyo ukweli. Akili yako ni kiwanda cha kuchakata mawazo ya kila aina. Na huwa yanabadilika kulingana na hali na mazingira yanavyobadilika. Mfano unaweza kuwa umepanga jukumu muhimu la kufanya, lakini (more…)

#TAFAKARI YA LEO; UNATAKA KUJISIKIA VIZURI AU KUWA BORA?

By | July 2, 2021

Ukitaka kujisikia vizuri, sikiliza uongo, maana huo unakubembeleza na haukuumizi. Ukitaka kuwa bora sikiliza ukweli, huo hakubembelezi na unakuumiza. Walio wengi wanapenda kubembelezwa na kutokuumizwa, ndiyo maana hawapigi hatua kwenye maisha yao. Ni wachache sana walio tayari kuukabili ukweli unaowaumiza na usiowabembeleza, lakini unawafanya kuwa bora zaidi. Kama unataka kufanikiwa, (more…)

2374; Mrejesho Ni Zawadi…

By | July 1, 2021

2374; Mrejesho Ni Zawadi… Huwa kuna kauli kwamba zawadi ni zawadi, hakuna ndogo wala kubwa. Ukipewa zawadi unapaswa kushukuru. Moja ya zawadi ambayo mtu yeyote anaweza kukupa ni mrejesho kwenye kile unachofanya. Unapompata mtu anayeelewa kile unachofanya, na akawa tayari kukupa mrejesho kwenye kile unachofanya, hiyo ni zawadi ya kipekee. (more…)

#TAFAKARI YA LEO; TUMIA VIZURI KILA UNACHOKUTANA NACHO…

By | July 1, 2021

Kila kitu unachokutana nacho kwenye maisha, ni rasilimali muhimu kwako kufika kule unakotaka kufika. Usikipoteze wala kukitumia vibaya, badala yake kitumie kwa manufaa. Matumizi mazuri ya kitu ni kujiuliza namna ya kukitumia ili kufika kule unakotaka kufika. Matumizi mabaya ya kitu ni kulaumu au kulalamika kwa kukutana nacho. Kila unachokutana (more…)

2373; Usichezee ‘Matirio’…

By | June 30, 2021

2373; Usichezee ‘Matirio’… Kila kitu unachokutana nacho kwenye maisha yako, ni ‘matirio’ ambayo unaweza kutumia kuyafanya maisha yako kuwa bora zaidi. Usikubali kupoteza chochote unachokutana nacho, badala yake kitumie kwa namna yenye manufaa kwako. Huwa unakula chakula, kinaenda tumboni na kumeng’enywa, virutubisho muhimu vinafyonzwa mwilini na uchafu kuondolewa. Hivyo ndivyo (more…)

#TAFAKARI YA LEO; UNAATHIRI WENGINE…

By | June 30, 2021

Kila maamuzi unayofanya kwenye maisha yako huwa yana athari kwenye maisha ya wengine. Hiyo ni kwa sababu sisi binadamu tunategemeana sana kwenye maisha. Na chochote unachotaka kwenye maisha yako wanacho wengine, hivyo unachohitaji ni kuweza kuwapa wanachotaka ili nao wakupe unachotaka. Huwezi kufanikiwa peke yako bila kuhusiana na wengine, hivyo (more…)

Mawazo 10 ya kuingiza fedha kupitia

By | June 29, 2021

Mawazo 10 ya kuingiza fedha kupitia ushereheshaji. Watu huwa wanafanya matukio mbalimbali kwenye maisha na kuhitaji washereheshaji (MC) wa kuyaendesha matukio hayo. Hili linatoa fursa kwa mtu kuweza kuingiza kipato kama mshereheshaji. Hapa kuna mawazo 10 ya kuingiza kipato kupitia ushereheshaji; Kuendesha shughuli za sherehe kwa watu binafsi. Kuendesha mikutano (more…)