3189; Unaanza na kufanya.

By | September 24, 2023

3189; Unaanza na kufanya. Rafiki yangu mpendwa,Kinachowakwamisha watu wengi kupata kile wanachotaka kwenye maisha yao ni kushindwa kuelewa jinsi mipango, hamasa na ufanyaji vinavyohusiana. Hivyo wengi huwa wanatumia muda wao mwingi kupanga nini watafanya. Na hata baada ya kupanga, bado wanatumia muda mwingi kupitia mipango waliyojiwekea. Halafu wanakuja kusubiri mpaka (more…)

Ukimpenda Mtu Huyu Mmoja, Umewapenda Watu Wote

By | September 23, 2023

Mpendwa mstoa mwenzangu, Maandiko ya kiimani yanasema kwamba, huwezi kumpenda Mungu usiyemwona kama huwezi kumpenda jirani yako. Mafundisho mengi yanatufundisha sisi kuwapenda wengine. Ndiyo maana hata mtu akipata fedha, anaanza kuwalipa watu wengine kwanza na kujisahau yeye mwenyewe. Watu wengi hatujafundishwa kujipenda sisi wenyewe kwanza. Na matatizo mengi kwenye maisha (more…)

3188; Ni milioni tu.

By | September 23, 2023

3188; Ni milioni tu. Rafiki yangu mpendwa,Mwenzetu hapa, Martin Tindwa, anaandika kitabu ambacho anakiita Jilipe Wewe Mwenyewe. Ni kitabu kuhusu mpango binafsi wa kifedha wa kujilipa wewe mwenyewe kwanza kwenye kila kipato ambacho mtu unaingiza. Kwenye kitabu hicho, Martin kuna dhana moja muhimu sana ambayo ameizungumzia na ina uzito mkubwa (more…)

Barua ya XXI; Kuhusu Sifa ambazo falsafa ya Ustoa inatupatia.

By | September 22, 2023

Barua ya XXI; Kuhusu Sifa ambazo falsafa ya Ustoa inatupatia. Rafiki yangu Mstoa, Sisi binadamu huwa tunapenda kuwa na sifa fulani mbele ya wengine.Huwa tunapenda umaarufu kupitia yale tunayofanya au tunayokuwa nayo kwenye maisha.Na tamaa hiyo ya sifa na umaarufu ndiyo inawasukuma wengi kufanya hata mambo yasiyo sahihi ili tu (more…)

3187; Siyo ngumu kihivyo.

By | September 22, 2023

3187; Siyo ngumu kihivyo. Rafiki yangu mpendwa,Watu wengi wamekuwa wanalalamika maisha ni magumu na kuna ukweli fulani kwenye hilo.Lakini bado tukiangalia kwenye uhalisia, maisha siyo magumu kihivyo, bali watu wenyewe wamekuwa wanazidisha ugumu wa maisha kwa mambo wanayofanya. Kwa mfano kwa walio wengi, kuamka asubuhi na mapema ili kuianza siku (more…)

3186; Mrejesho wa watu.

By | September 21, 2023

3186; Mrejesho wa watu. Rafiki yangu mpendwa,Sisi binadamu kama viumbe wa kijamii, huwa tunapenda sana kuwa ndani ya kundi la watu.Ili kujihakikishia nafasi yetu kwenye kundi lolote tulilopo, huwa tunajali sana kuhusu mrejesho wa watu wengine kuhusu sisi. Huwa tunataka sana kukubalika na kila mtu, tukiamini ndiyo njia salama ya (more…)

3185; Mateso unayoyafurahia.

By | September 20, 2023

3185; Mateso unayoyafurahia. Rafiki yangu mpendwa,Huwa kuna kauli inayosema watu waliofanikiwa wanakuwa wamefanya vitu ambavyo wasiofanikiwa hawapendi kuvifanya. Pia ni vitu ambavyo wao wenyewe hawapendi kuvifanya, ila wanakuwa hawana namna bali kuvifanya. Ukweli ni kwamba huwezi kupata mafanikio makubwa kwa kufanya yale ambayo kila mtu anayafanya, tena kwa namna ambavyo (more…)

3184; Haina Mjadala.

By | September 19, 2023

3184; Haina Mjadala. Rafiki yangu mpendwa,Kwenye safari ya kujenga mafanikio makubwa kwenye maisha, lazima uwe na mchakato ambao unaufuata mara zote bila kuacha.Unapaswa kuwa na mambo ambayo utayafanya bila ya kuruhusu hofu au sababu zozote zile kukuzuia.Hii ni dhana inayoitwa Haina Mjadala (Non Negotiable). Kwenye mambo hayo, hupotezi muda kujiuliza (more…)

3183; Nini naweza kupenda kwake?

By | September 18, 2023

3183; Nini naweza kupenda kwake? Rafiki yangu mpendwa,Wateja tulionao kwenye kile tunachouza ni watu muhimu sana kwetu.Hao ndiyo wanaotuwezesha kulipa gharama mbalimbali kwenye maisha yetu. Ni kupitia wao kununua kwetu ndiyo tunapata fedha za kuyaendesha maisha yetu.Wateja wanaonunua kwetu ni watu muhimu sana kwetu. Swali ni je tunawafanyaje ili waweze (more…)

3182; Suuza kisha rudia.

By | September 17, 2023

3182; Suuza kisha rudia. Rafiki yangu mpendwa,Japokuwa safari ya kupata mafanikio makubwa kwenye maisha ni ngumu, watu wamekuwa wanazidisha ugumu huo kwa kuamua kuacha kufanya yale ya msingi kwenye hiyo safari. Kwenye kila eneo la maisha, huwa kuna mambo mengi ya kufanya.Lakini yapo ya msingi kabisa ambayo ni lazima yafanywe (more…)