Ongea Na Kocha; Instant Cashflow – Kuongeza Idadi Na Kiwango Cha Manunuzi.

By | March 21, 2022

Habari Mwanamafanikio? Karibu kwenye kipindi cha ONGEA NA KOCHA ambapo tumeendelea na uchambuzi wa kitabu cha INSTANT CASHFLOW kilichoandikwa na Bradley Sugars. Kitabu hiki ni mwendelezo wa msingi mkuu tuliojifunza kwenye kitabu cha BILLIONAIRE IN TRAINING cha mwandishi huyo huyo. Kwenye BILLIONAIRE IN TRAINING tulijifunza ngazi tano za ujasiriamali ambazo (more…)

2637; Sahihi na siyo sahihi.

By | March 21, 2022

2637; Sahihi na siyo sahihi. Mtu mmoja amewahi kunukuliwa akisema kipimo cha akili iliyokomaa ni kuweza kushikilia kwenye akili mawazo mawili yanayopingana kwa wakati mmoja. Hili ni zoezi gumu mno kwa sababu kwa kawaida binadamu huwa tunapenda sana uhakika. Kukaa na mawazo mawili yanayopingana ni kukosa uhakika. Wengi huona ni (more…)

#SheriaYaLeo (141/366); Wajue sitaki nataka.

By | March 21, 2022

#SheriaYaLeo (141/366); Wajue sitaki nataka. Kuna watu ambao kwa nje wanajifanya kama hawakitaki kitu, ila kwa ndani wanakitaka sana. Kwa nje wanakikataa, ila ni kwa lengo la kuwafanya watu wawabembeleze ndiyo wakubali. Watu hao wanakuwa wanajua tabia ya binadamu, kwamba ukionekana unataka sana kitu, watu wanakuzuia usikipate. Au hata ukikipata (more…)

#SheriaYaLeo (140/366); Kutaka usawa kwa kila mtu.

By | March 20, 2022

#SheriaYaLeo (140/366); Kutaka usawa kwa kila mtu. Njia nyingine ambayo hutumiwa sana na wale wanaotaka mamlaka bila ya kuonekana wazi wazi ni kutaka usawa kwa kila mtu. Hapa husisitiza kila mtu ni sawa na lazima watu wote wachukuliwe kwa usawa. Hukazana kuwaaminisha wengine kwamba uwezo, uimara na hadhi tofauti za (more…)

#SheriaYaLeo (139/366); Angalia nyuma ya barakoa.

By | March 19, 2022

#SheriaYaLeo (139/366); Angalia nyuma ya barakoa. Kunbuka kwa kawaida watu huwa wanatengeneza mwonekano fulani wanaotaka dunia ione. Hivyo kila mtu ni kama amevaa barakoa, akionyesha kile ambacho anataka wengine waone na kuficha nia kuu aliyonayo. Mtu anaweza kuwa na uso wa tabasamu na maneno mazuri kabisa. Hii ni barakoa inayowafanya (more…)

2634; Lakini unakosea.

By | March 18, 2022

2634; Lakini unakosea. Hayo ni maneno utakayoyasikia maisha yako yote, mpaka siku unayoondoka hapa duniani. Kwa maamuzi yoyote utakayofanya na chochote utakachofanya, kuna watu watakuambia unakosea. Sema unataka fedha na hicho ndiyo kipaumbele chako cha kwanza na kuna watu watakuambia unakosea, una tamaa sana ya fedha na fedha siyo kila (more…)

#SheriaYaLeo (138/366); Tambua Kivuli Cha Watu.

By | March 18, 2022

#SheriaYaLeo (138/366); Tambua Kivuli Cha Watu. Kwenye safari yako ya maisha utakutana na watu ambao wanatumia nguvu kubwa kuonyesha tabia fulani nzuri kwa nje. Inaweza kuwa ni huruma iliyopitiliza, kujali sana, kuonekana watakatifu au imara sana. Lakini pale unapowajua watu hao kwa undani, unaona kuna kivuli kipo nyuma ya tabia (more…)

2633; Kafanyaje huyu?

By | March 17, 2022

2633; Kafanyaje huyu? Kuna picha ya kichekesho (meme) inayozunguka sana kwenye mitandao. Kwenye picha hiyo mtu anayeonekana kuzimia amebebwa kwenye machela na watu wawili. Mmoja anauliza mtu huyo aliyebebwa amefanya nini? Mwingine anajibu kitu alichofanya mtu huyo na kupata matokeo ambayo hakutegemea. Watu na taasisi mbalimbali wamebadili maelezo ya mtu (more…)