2642; Njia za kukabiliana na msongo.

By | March 26, 2022

2642; Njia za kukabiliana na msongo. Kila binadamu huwa anapitia hali ya msongo kwenye maisha yake. Hiyo inatokana na kwamba dunia huwa haiendi vile tunavyopanga sisi. Hivyo chochote unachopanga, kuna mambo huwa yanaenda tofauti kabisa. Mambo hayo yanayoenda tofauti ndiyo yanaleta hali ya msongo. Kuna njia mbalimbali ambazo watu wamekuwa (more…)

#SheriaYaLeo (146/366); Waepuke wapenda drama.

By | March 26, 2022

#SheriaYaLeo (146/366); Waepuke wapenda drama. Kuna watu ambao wanatumia drama kama njia ya kuwatawala watu wengine. Watu hawa ni wazuri sana kwenye kutengeneza mambo na kuigiza kwa namna ambayo wataonekana wanaonewa. Wanahakikisha wanawateka wengine kihisia ili wayaamini maigizo yao, wakitafuta zaidi huruma. Watu hawa wana hadithi na mapito mengi ambapo (more…)

2641; Dawa kuu ya hasira.

By | March 25, 2022

2641; Dawa kuu ya hasira. Ni kupuuza. Chukua mfano huu. Wewe hujui lugha ya kireno. Umekutana na mreno, Halafu akakutukana kwa kireno. Je utakasirika? Jibu ni hapana, Hutakasirika, Kwa sababu hutajua hata kama amakutumana. Kimbembe sasa ni unapokutana na mswahili mwenzako. Akakuambia wewe ni mpumbavu kabisa. Kinachotokea ni unaanza kujichaji (more…)

#SheriaYaLeo (145/366); Pesa rahisi.

By | March 25, 2022

#SheriaYaLeo (145/366); Pesa rahisi. Matapeli wote huwa wanajua mbinu moja ambayo inawasaidia sana kuwanasa wale wanaowalenga. Mbinu hiyo ni kuibua tamaa kwa mtu. Hakuna kitu kinachoibua tamaa kwa wengi kama fursa ya kupata pesa bure au kwa urahisi. Tangu enzi na enzi, watu wamekuwa wanatapeliwa kwa mbinu hii. Wanaonyeshwa kwamba (more…)

2640; Kiranja mkuu wa dunia.

By | March 24, 2022

2640; Kiranja mkuu wa dunia. Ni cheo ambacho wengi wanakitaka, lakini hawawezi kukipata. Kwa sababu cheo hicho hakipo. Huwa tunapenda sana dunia iende vile tunavyotaka sisi. Lakini hilo haliwezekani, halipo kabisa ndani ya uwezo wetu. Tunataka kuwabadili watu, wawe na kufanya vile tunavyotaka sisi. Lakini hilo haliwezekani, hata uwe na (more…)

#SheriaYaLeo (144/366); Usiyaamini macho yako mara zote.

By | March 24, 2022

#SheriaYaLeo (144/366); Usiyaamini macho yako mara zote. Wale wanaotaka kukushawishi kwa namna mbalimbali, huwa wanatumia zaidi picha ili kukujengea taswira ya aina fulani itakayokufanya uamini vitu fulani. Wanajua udhaifu wetu binadamu kwamba kile tunachoona huwa kina nguvu kubwa na huwa tunakiamini zaidi. Wanaunganisha picha mbalimbali pamoja na maelezo yanayotengeneza taswira (more…)

2639; Kama watu wangesimamia maneno yao.

By | March 23, 2022

2639; Kama watu wangesimamia maneno yao. Leo hii ungekuwa mbali sana. Hebu fikiria kama watu wote waliokuahidi watanunua unachouza, kama kweli wangenunua kama walivyoahidi si ungekuwa mbali sana? Hebu kumbuka wote waliokuambia wapo pamoja na wewe na watapambana kufa na kupona wakiwa upande wako. Kama wangefanya hivyo leo si ungekuwa (more…)

#SheriaYaLeo (143/366); Tambua uimara wa tabia za watu.

By | March 23, 2022

#SheriaYaLeo (143/366); Tambua uimara wa tabia za watu. Tabia za watu zina nguvu kubwa kwenye maisha yao. Mtu mwenye tabia dhaifu, itadhoofisha hata sifa nyingine alizonazo. Kwa mfano mtu mwenye akili sana lakini mwenye tabia dhaifu, anaweza kuja na mawazo mzuri sana na hata kufanya kazi bora. Lakini wanapokutana na (more…)

2638; Ni kujenga, siyo kuota.

By | March 22, 2022

2638; Ni kujenga, siyo kuota. Mafanikio huwa yanaanza na ndoto, mtu kuwa na picha ya kile unachotaka, ambacho kwa sasa huna. Lakini ili kufikia ndoto hiyo, ni lazima ujenge. Ndoto haitafikiwa tu kwa kuota, Bali itafikiwa kwa kujenga. Hatua unazochukua katika kuifikia ndoto ndizo zinaifanya ndoto hiyo kuwa uhalisia. Thamani (more…)

#SheriaYaLeo (142/366); Kuridhisha kulikopitiliza.

By | March 22, 2022

#SheriaYaLeo (142/366); Kuridhisha kulikopitiliza. Kuna watu ambao ni rahisi sana kukubaliana na wewe pale unapokutana nao. Wanatabasamu sana, wana shauku kubwa na wanakuwa tayari kukusaidia kwa lolote. Hilo linakufanya uwaone ni watu sahihi kwako na kuwakubali kwenye maisha yako. Wanakuwa ni watu wanaokuridhisha na hivyo unawapa fursa mbalimbali kwenye maisha (more…)