#TAFAKARI YA LEO; UHURU BILA NIDHAMU…

By | June 26, 2021

Uhuru bila ya nidhamu ni sawa na gari bila ya breki, linaweza kukupeleka kasi sana, lakini kasi hiyo itakupoteza kabisa, kwa sababu huna namna ya kulidhibiti gari. Watu wengi wamekuwa wanakimbilia kuwa huru kabla hawajajijengea nidhamu na kinachotokea ni wanapotezwa kabisa na uhuru wanaokuwa wamepata. Wewe pambana kujijengea kwanza nidhamu (more…)

2368; Uhuru Siyo Rahisi…

By | June 25, 2021

2368; Uhuru Siyo Rahisi… Watu huwa wanapenda kuzungumzia uhuru, kueleza jinsi wanavyotaka kuwa na uhuru zaidi kwenye maisha yao. Lakini ukweli ni kwamba, uhuru siyo rahisi. Kwanza siyo rahisi kuupata. Na pili siyo rahisi kuutunza. Kuupata uhuru ni vigumu kwa sababu hakuna atakayekuwa tayari kukuacha uwe huru, unahitaji kupambana kweli (more…)

#TAFAKARI YA LEO; HAKUNA KESHO….

By | June 25, 2021

Unapopanga kufanya kitu, chukuli kwamba hakuna kesho na pambana ukifanye kama ulivyopanga. Ni rahisi kujishawishi na kukisogeza mbele kile ulichopanga kufanya, lakini ukisharuhusu hilo, itakuwa vigumu kwako kufanya kitu hicho. Panga na fanya kama ulivyopanga na kama kutakuwa na usumbufu unaokuzuia usifanye, panga kufanya siku hiyo baada ya usumbufu kuisha (more…)

2367; Ngwe nyingine….

By | June 24, 2021

2367; Ngwe nyingine…. Igawe siku yako kwenye ngwe mbalimbali. Hiyo itakusaidia pale unaposhindwa kufanya ulichopanga, badala ya kusema utakifanya kesho, jiambie utakifanya kwenye ngwe nyingine. Huwa unaanza siku kwa kuipanglia vizuri, lakini huwa yanatokea mambo na kuvuruga mipango yako. Ni rahisi kuona siku imeharibika na kujiambia utafanya tena kesho. Lakini (more…)

#TAFAKARI YA LEO; UNAHAKIKISHAJE UNAUPATA UKWELI…

By | June 24, 2021

Ukweli mara nyingi huwa unaumiza na wengi wanaokujali hawapo tayari kukuumiza, hivyo wanaweza kuuona ukweli ila wasikuambie. Watu wakishagundua hupendi ukweli unaokuumiza, wanakulisha uongo, ili tu ujisikie vizuri. Lakini uongo huo haukusaidii zaidi ya kukupoteza. Unachohitaji sana ni kuujua ukweli, hata kama unakuumiza, maana huo ndiyo unaokuweka huru. Tafuta watu (more…)

2366; Mtu Sahihi Wa Kusikiliza Ukosoaji Wake

By | June 23, 2021

2366; Mtu Sahihi Wa Kusikiliza Ukosoaji Wake Kwako… Kitu chochote kile utakachofanya kwenye maisha yako, kuna watu watakukosoa. Watu watachagua kuwa na maoni kuhusu wewe kwa namna wanavyotaka wao wenyewe na siyo unavyotaka wewe. Ukisema umsikilize kila mtu au kutaka kumridhisha kila mtu, hutaweza kufanya kitu chochote kikubwa kwenye maisha (more…)

#TAFAKARI YA LEO; KAMA WENGI WANAFANYA, SIYO SAHIHI…

By | June 23, 2021

Ipo kauli ya kiswahili inayosema wengi wape, kauli hiyo ni sahihi kwenye mambo ya kawaida. Inapokuja kwenye mafanikio makubwa, wengi huwa hawapo sahihi. Kwa sababu njia ya kuelekea kwenye mafanikio ni ngumu na yenye vikwazo na changamoto nyingi, wengi huwa wanaikwepa. Hivyo ukikutana na kitu ambacho wengi wanakikubali na kukisifia, (more…)

2365; Ingekuwa rahisi, kila mtu angefanya…

By | June 22, 2021

2365; Ingekuwa rahisi, kila mtu angefanya… Kama inanibidi nifanye maamuzi ya haraka kwenye kitu ambacho sina taarifa za kutosha, huwa ninaangalia aina ya watu wanaokubaliana na kitu hicho au kukipigia debe. Nikiona watu wengi wanakubaliana nacho na kukisifia, naweza kuwa na uhakika kwamba kitu hicho siyo bora na kinachoweza kumfikisha (more…)

#TAFAKARI YA LEO; UNAVYOWEZA KUACHA ALAMA HAPA DUNIANI.

By | June 22, 2021

Huhitaji kufanya ugunduzi mkubwa au mapinduzi fulani ndiyo uache alama hapa duniani. Ipo njia rahisi ambayo kila mmoja wetu anaweza kuitumia na akaacha alama kubwa. Njia hiyo ni kujifunza kwa kupata maarifa sahihi, kuyatumia maarifa hayo ili kuyafanya maisha yako kuwa bora kisha kuwafundisha wengine kile unachojia na uzoefu uliopata. (more…)