Author Archives: Dr. Makirita Amani

About Dr. Makirita Amani

Dr. Makirita Amani ni daktari wa binadamu, mwandishi, mhamasishaji na mjasiriamali. Dhumuni lake kubwa kwenye maisha ni KUWASAIDA WATU KUBORESHA MAISHA YAO NA KUFIKIA MAFANIKIO MAKUBWA KUPITIA KAZI ANAZOFANYA. Mawasiliano 0717396253 email makirita@kisimachamaarifa.co.tz

2572; Kipi kingine unachojali zaidi?

By | January 15, 2022

2572; Kipi kingine unachojali zaidi? Kile unachokijali zaidi, ndiyo unachokipa umakini wako na hicho ndiyo kinachokua zaidi. Kama una ndoto kubwa ambazo ndiyo unazijali zaidi, fikra zako zote zinakuwa kwenye ndoto hizo na mengine yote unayapuuza. Kila wakati unakuwa unapambana na namna ya kufikia ndoto ulizonazo na hicho tu ndiyo (more…)

#SheriaYaLeo (76/366); Badili mtazamo wako.

By | January 15, 2022

#SheriaYaLeo (76/366); Badili mtazamo wako. Ubunifu ni matokeo ya kuwa muwazi na kuweza kukiangalia kitu kwa mitazamo mbalimbali. Wakati wengine wanakiona kitu kwa mazoea, walio wabunifu huwa wanakiona kwa namna ya tofauti na ya kipekee. Wanaona kitu kikiweza kutumika kwa namna tofauti na ilivyozoeleka. Hivyo pia ndivyo unavyopaswa kuwa ili (more…)

2571; Machache kabla ya mengi.

By | January 14, 2022

2571; Machache kabla ya mengi. Mawazo unayoweza kuyafanyia kazi ni mengi. Fursa unazoweza kunufaika nazo ni chungu mzima. Lakini kuna ukomo wa rasilimali muhimu kama muda, nguvu na fedha. Ukomo huo unakutaka uweke vizuri vipaumbele vyako ili uweze kuzitumia rasilimali hizo vizuri. Lakini wengi wamekuwa wanashindwa na hilo, wanashindwa kuweka (more…)

#SheriaYaLeo (75/366); Ipe kazi yako maisha.

By | January 14, 2022

#SheriaYaLeo (75/366); Ipe kazi yako maisha. Kila unachofanya, kina aina yake ya kipekee ya maisha. Pale unapokifanya kitu hicho kwa kina na kuweka umakini kwenye mambo madogo madogo ndiyo unaipa kazi hiyo maisha. Unaifanya kazi hiyo iweze kusimama na kujitofautisha na kazi nyingine za aina hiyo. Na pia unaifanya kazi (more…)

#SheriaYaLeo (74/366); Zama kwenye maelezo.

By | January 13, 2022

#SheriaYaLeo (74/366); Zama kwenye maelezo. Kitu chochote kile unachotaka kubobea, unapaswa kuzama kwenye maelezo na kukijua kwa kina kabisa. Kadiri unavyokijua kitu kwa kina, ndivyo unavyoona mengi na kuweza kukitumia kwa fursa kubwa. Maelezo mengi ya kila kitu yanapatikana, kwa kuanzia ndani ya kitu hicho katika kukifanya na pia kwenye (more…)

2569; Kuadhibiwa na unachokitaka.

By | January 12, 2022

2569; Kuadhibiwa na unachokitaka. Werevu wamewahi kusema ukitaka kumwadhibu mtu, mpe kile anachokitaka, tena kwa namna anavyokitaka. Ni kauli ambayo wengi huwa hawaielewi, ila twende kwenye mifano tuweze kujionea uhalisia wake. Chukua mtu anayecheza bahati nasibu, wote tunajua anataka ushindi. Sasa chukua mtu aliyeshinda bahati nasibu, baada ya muda maisha (more…)

#SheriaYaLeo (73/366); Jijengee ustahimilivu.

By | January 12, 2022

#SheriaYaLeo (73/366); Jijengee ustahimilivu. Safari ya kuelekea kwenye ubobezi wa hali ya juu na mafanikio makubwa siyo rahisi. Kadiri unavyokwenda ndivyo inataka zaidi kutoka kwako, ikitaka muda wako na juhudi zako zaidi na zaidi. Hilo huwachosha wengi na kuamua kuishia njiani, maana hujikuta wanaishiwa nguvu na kuchoka sana. Kama wewe (more…)

2568; Uhakika upo kwenye mchakato.

By | January 11, 2022

2568; Uhakika upo kwenye mchakato. Ukienda kununua baadhi ya vifaa, mfano simu, tv, redio n.k, huwa unapewa uhakika. Kwamba kifaa hicho kitafanya kazi vizuri na kama kitakuwa na shida basi unaweza kukirudisha na kupewa kingine. Hii ni njia ya masoko ambayo imekuwa na nguvu kwa sababu binadamu tunapenda sana uhakika. (more…)

#SheriaYaLeo (72/366); Jiboreshe kupitia kushindwa.

By | January 11, 2022

#SheriaYaLeo (72/366); Jiboreshe kupitia kushindwa. Kukosea na kushindwa ni zawadi kubwa kwako. Kwani kunakuonyesha ni maeneo gani ambayo una madhaifu au bado hujawa imara kama inavyohitajika. Unapofanya kitu na ukakosea au ukashindwa, haimaanishi kwamba huwezi kamwe kukifanya. Bali inamaanisha kuna vitu bado hujavijua katika kufanya kitu hicho. Hivyo unapaswa kujifunza (more…)