Author Archives: Dr. Makirita Amani

About Dr. Makirita Amani

Dr. Makirita Amani ni daktari wa binadamu, mwandishi, mhamasishaji na mjasiriamali. Dhumuni lake kubwa kwenye maisha ni KUWASAIDA WATU KUBORESHA MAISHA YAO NA KUFIKIA MAFANIKIO MAKUBWA KUPITIA KAZI ANAZOFANYA. Mawasiliano 0717396253 email makirita@kisimachamaarifa.co.tz

#SheriaYaLeo (81/366); Mbobezi wa ulimwengu.

By | January 20, 2022

#SheriaYaLeo (81/366); Mbobezi wa ulimwengu. Wanaofikia ubobezi wa hali ya juu siyo wale wanaojua tu kuhusu eneo walilochagua, bali wale wanaojua na maeneo mengine pia. Ni wale wanaotafuta muunganiko uliopo kwenye maeneo tofauti tofauti na kutumia muunganiko huo kufanya makubwa zaidi. Akili ya mbobezi wa ulimwengu huwa inaendelea kukua kadiri (more…)

2576; Marudio.

By | January 19, 2022

2576; Marudio. Kama hujawahi kuelewa hili basi nikusisitize tena, kila kitu kwenye maisha kinategemea sana marudio. Hebu fikiria siku moja moyo wako ungesema umechoka kudunda na hivyo inabidi upumzike kwa siku chache. Ni hakika hakutakuwa na maisha. Kula, kupumua, kujifunza na hata kuchukua hatua ili ufanikiwe, inahitaji marudio yasiyo na (more…)

#SheriaYaLeo (80/366); Ubongo wa mbobezi.

By | January 19, 2022

Wakati wa kujifunza na kufanya kitu kipya, mishipa mingi ya fahamu huwa inazaliwa kwenye ubongo wa mbele. Mishipa hiyo ndiyo inayotuwezesha sisi binadamu kujifunza na kufanya mambo mapya. Wakati huo wa kujifunza ubongo huwa na kazi nyingi, huwa katika hali ya msongo. Lakini kitu kikisharudiwa rudiwa kwa muda mrefu, kinakuwa (more…)

2575; Mabadiliko makubwa hayaletwi na wengi.

By | January 18, 2022

2575; Mabadiliko makubwa hayaletwi na wengi. Mabadiliko makubwa kabisa hayajawahi kuletwa na watu wengi. Bali huwa ni matokeo ya watu wachache waliojitoa kweli ili kuhakikisha wanakamilisha wanachotaka. Ni vigumu sana kwa watu walio wengi kuweza kukitoa kwa muda mrefu bila kuchoka. Kundi la watu wengi huwa ni rahisi kupotea kwa (more…)

#SheriaYaLeo (79/366); Mazoea yanayoua ubunifu.

By | January 18, 2022

#SheriaYaLeo (79/366); Mazoea yanayoua ubunifu. Kikwazo kikubwa kabisa cha ubunifu kwa watu ni mazoea. Kwenye kila tasnia, ugunduzi mpya unapopatikana na kuwa na mafanikio, huo ndiyo huchukuliwa na kuzoewa na kila mtu. Hiyo inachukuliwa kama ndiyo njia kuu ya kufanya kitu hicho. Kila mtu anaifuata hiyo kwa sababu ndiyo iliyozoeleka (more…)

Ongea Na Kocha; Breakfast With Seneca (Falsafa Ya Ustoa)

By | January 17, 2022

Habari Mwanamafanikio? Karibu kwenye kipindi cha ONGEA NA KOCHA ambapo tumepata nafasi ya kujadili kwa kina uchambuzi wa kitabu kinachoitwa Breakfast With Seneca. Ni kitabu kinachoelezea vizuri falsafa ya Ustoa kwa namna inavyoweza kutumika kwenye zama tunazoishi sasa. Mwandishi amekusanya pamoja kazi za Seneca kwa namba ambayo zinajibu changamoto nyingi (more…)

#SheriaYaLeo (78/366); Nguvu ya matakwa na maamuzi.

By | January 17, 2022

#SheriaYaLeo (78/366); Nguvu ya matakwa na maamuzi. Pale unapokitaka kitu kweli na unapokuwa huna mbadala mwingine wa kitu hicho, huwa unapata nguvu ya kupambana mpaka kukipata. Unajitoa kwa kila namna na unafanya kazi kwa muda wa ziada ili upate kile unachotaka. Pale unapojua kwa hakika nini unachotaka na unapoamua kwamba (more…)

2573; Hakuna kisicho na manufaa.

By | January 16, 2022

2573; Hakuna kisicho na manufaa. Kwenye maisha yetu, huwa tunapitia mambo mbalimbali kwa nyakati mbalimbali. Baadhi ya mambo hayo yapo ndani ya uwezo wetu, huku mengi yakiwa nje ya uwezo wetu. Kwa tafsiri zetu wenyewe, kuna baadhi ya mambo tunasema ni mazuri huku mambo mengine tukisema ni mabaya. Kama yanaendana (more…)

#SheriaYaLeo (77/366); Ubobezi Na Mafanikio Haviji Kirahisi.

By | January 16, 2022

#SheriaYaLeo (77/366); Ubobezi Na Mafanikio Haviji Kirahisi. Kutengeneza kazi yoyote ya kibunifu na yenye maana au kufanya ugunduzi wa kitu kipya inahitaji nidhamu ya hali ya juu, kuweza kujidhibiti na utulivu na uimara wa kihisia. Inahitaji sana mtu kuweza kubobea kwenye kila eneo linalohusika na kile anachofanya. Nguvu hizo haziwezi (more…)