Author Archives: Dr. Makirita Amani

About Dr. Makirita Amani

Dr. Makirita Amani ni daktari wa binadamu, mwandishi, mhamasishaji na mjasiriamali. Dhumuni lake kubwa kwenye maisha ni KUWASAIDA WATU KUBORESHA MAISHA YAO NA KUFIKIA MAFANIKIO MAKUBWA KUPITIA KAZI ANAZOFANYA. Mawasiliano 0717396253 email makirita@kisimachamaarifa.co.tz

ONGEA NA KOCHA; Safari Ya Maisha Ya Farhia Omar.

By | January 10, 2022

Habari wanamafanikio? Karibuni kwenye kipindi cha ONGEA NA KOCHA ambapo tumefanya mahojiano na mwanamafanikio mwenzetu Farhia Omar aliyetushirikisha safari yake ya maisha. Farhia ametushirikisha historia fupi ya maisha yake tangu kuzaliwa. Ametushirikisha kusoma na kufanya kazi kabla ya kusafiri kwenda nje ya nchi. Ametushirikisha sababu zilizomsukuma kwenda nje ya nchi (more…)

2567; Kwa sababu wengine wanafanya.

By | January 10, 2022

2567; Kwa sababu wengine wanafanya. Sisi binadamu tunashawishiwa sana na binadamu wengine kuliko kitu kingine chochote. Ni rahisi sana kufanya kile ambacho wengine wanafanya, hata kama umejiambia hutafanya. Mambo yote, mazuri na mabaya huwa yanafanyika kwa sababu hiyo. Pale mtu anapoona wengine wanafanya, basi anaona siyo vibaya na yeye akifanya. (more…)

#SheriaYaLeo (71/366); Weka umakini mkubwa.

By | January 10, 2022

#SheriaYaLeo (71/366); Weka umakini mkubwa. Ili kufikia ubobezi wa hali ya juu, unapaswa kuweka umakini mkubwa sana kwenye chochote kile unachoamua kufanya. Usifanye tu kwa juu juu au kwa mazoea, badala yake fanya kwa kina kabisa. Jua undani wa kile unachokifanya na kifanye kwa namna ya tofauti na ya kipekee (more…)

2566; Vichache na vingi.

By | January 9, 2022

2566; Vichache na vingi. Kwenye zama tunazoishi sasa, kuna mambo mengi sana ya kufanya. Na unaweza kufanya karibu kila kitu. Hebu angalia tu biashara zinazofanyika kwenye eneo ulilopo, karibu zote unaweza kuzifanya. Na wakati mwingine unajiambia kabisa, yaani hawa wanaweza hivi, hata mimi siwezi kushindwa. Hilo linaweza kukushawishi uhangaike na (more…)

#SheriaYaLeo (70/366); Maarifa ndiyo ukuu wako.

By | January 9, 2022

#SheriaYaLeo (70/366); Maarifa ndiyo ukuu wako. Maarifa kidogo ni sumu kubwa. Kwa kujua kidogo unaweza kupata kiburi na kudhani tayari unajua kila kitu. Unachopaswa kujua ni kwamba maarifa yanaendelea kubadilika kadiri muda unavyokwenda. Historia iko wazi kabisa, vitu vingi ambavyo watu waliamini ni kweli, kwa sasa vimethibitishwa siyo kweli. Maendeleo (more…)

2565; Ni juhudi zipi ambazo umeweka?

By | January 8, 2022

2565; Ni juhudi zipi ambazo umeweka? Kuna kitu unachotaka, lakini vikwazo na changamoto zinakuzuia usipate kitu hicho. Ni rahisi kutumia hiyo kama sababu ya kukosa unachotaka, na kujifariji kwamba hakuna namna. Kabla hujaendelea kujifariji, nikukumbushe kitu kimoja muhimu, hakuna aliyefanya makubwa ambaye hakukutana na vikwazo na changamoto. Kwa hakika, pale (more…)

#SheriaYaLeo (69/366); Kukosa uvumilivu ni adui mkubwa.

By | January 8, 2022

#SheriaYaLeo (69/366); Kukosa uvumilivu ni adui mkubwa. Kikwazo kikubwa zaidi kwenye ubunifu wako ni kukosa uvumilivu. Ile hali ya kuharakisha na kutaka kupata matokeo makubwa kwa haraka ni kikwazo kikubwa kwako kufikia ubobezi wa hali ya juu. Unapoharakisha, hupati muda wa kujifunza kwa kina na kubobea yale ya msingi kwenye (more…)

Ongea Na Kocha; Uwajibikaji, Tribe Na Isaack Zake.

By | January 7, 2022

Habari mwanamafanikio? Karibu kwenye kipindi hiki cha ONGEA NA KOCHA ambapo unakwenda kujifunza yafuatayo. Kwenye somo la juma utajifunza umuhimu wa kuwa kwenye jamii ambayo inakuwajibisha ili kuweza kufanya makubwa. Kwa asili sisi binadamu ni wavivu na huwa tunapenda kufanya vitu rahisi. Lakini hivyo haviwezi kutufikisha kwenye mafanikio. Tunahitaji sana (more…)

#SheriaYaLeo (68/366); Baki na udadisi wako.

By | January 7, 2022

#SheriaYaLeo (68/366); Baki na udadisi wako. Wakati unaanza safari ya ubobezi, unakuwa na udadisi mkubwa, kitu kinachokusukuma kujifunza mambo mengi na kuweza kufanya mapya na makubwa. Hilo linapelekea upate matokeo mazuri. Na hapo ndipo hatari inapoanzia. Kutokana na matokeo mazuri unayokuwa umepata, unaacha kuwa mdadisi, unajiona umeshajua kila kitu na (more…)