Author Archives: Dr. Makirita Amani

About Dr. Makirita Amani

Dr. Makirita Amani ni daktari wa binadamu, mwandishi, mhamasishaji na mjasiriamali. Dhumuni lake kubwa kwenye maisha ni KUWASAIDA WATU KUBORESHA MAISHA YAO NA KUFIKIA MAFANIKIO MAKUBWA KUPITIA KAZI ANAZOFANYA. Mawasiliano 0717396253 email makirita@kisimachamaarifa.co.tz

2515; Maswali yanayoulizwa mara kwa mara.

By | November 19, 2021

2515; Maswali yanayoulizwa mara kwa mara. Kwa shughuli yoyote unayofanya, iwe ni kazi au biashara, kuna maswali ambayo wale unaowahudumia huwa wanayauliza mara kwa mara. Kwa kiingereza huwa wanaita FAQ (Frequently Asked Questions). Haya ni maswali yanayoweza kukukera na kuona kwa nini watu hawaelewi vitu vidogo na vya kawaida kiasi (more…)

#SheriaYaLeo (19/366); Sikiliza Mamlaka Yako Ya

By | November 19, 2021

#SheriaYaLeo (19/366); Sikiliza Mamlaka Yako Ya Ndani. Upo hapa duniani siyo tu kwa ajili ya kutimiza tamaa zako na kutumia vile wengine wametengeneza, bali pia kuchangia, kutimiza kusudi kubwa. Ili kuweza kutimiza kusudi hilo, lazima utengeneze kile cha kipekee ndani yako. Acha kusikiliza sana maneno na maoni ya wengine wanaokuambia (more…)

2514; Uasi usio na msingi wowote.

By | November 18, 2021

2514; Uasi usio na msingi wowote. Tunajua umuhimu wa kukataa mazoea na kuepuka kundi ili kuweza kufanikiwa. Kwamba tunajua ni vigumu sana kufanikiwa kwa kufanya mambo ambayo yamezoeleka kufanyika na yanafanywa na kila mtu. Lakini pia haimaanishi unapaswa kutembea kwa mikono kwa sababu kila mtu anatembea kwa miguu. Kuna baadhi (more…)

#SheriaYaLeo (18/366); Acha Kutaka Kumfurahisha Kila Mtu.

By | November 18, 2021

#SheriaYaLeo (18/366); Acha Kutaka Kumfurahisha Kila Mtu. Utalipa gharama kubwa sana kwa kutaka kumfurahisha kila mtu na kuonekana kujali kuliko kuyaishi maisha yako halisi na kuonyesha kivuli chako. Kuyaishi maisha yako; Kwanza kabisa unapaswa kuheshimu maoni yako kuliko ya wengine, hasa inapokuja kwenye eneo lako la ubobezi, eneo ambalo umechagua (more…)

2513; Ubinafsi wa watu.

By | November 17, 2021

2513; Ubinafsi wa watu. Watu watakujali na kuwa wema kwako pale wanapokuwa na kitu wanachokihitaji kutoka kwako. Pale unapokuwa una matumizi kwao, watakujali sana. Lakini unapokuwa huna manufaa kwao, wanapokuwa hawana chochote wanachohitaji kutoka kwako, hawatakujali wala kuwa wema kwako. Watakudharau na kukupotezea. Hilo linaweza kukuumiza, kukukasirisha na kukufanya uwe (more…)

#SheriaYaLeo (17/366); Chanzo sahihi cha ubunifu.

By | November 17, 2021

#SheriaYaLeo (17/366); Chanzo sahihi cha ubunifu. Unapaswa kubadili dhana yako ya ubunifu na kuuangalia kwenye kona mpya. Mara nyingi watu huhusianisha ubunifu na akili au namna fulani ya kufikiri. Ukweli ni kwamba ubunifu ni kitendo kinachohusisha nafsi yako nzima – kuanzia hisia, nguvu, tabia na fikra. Kuja na uvumbuzi mpya, (more…)

2512; Kuna wengine pia.

By | November 16, 2021

2512; Kuna wengine pia. Ukiona mende mmoja ndani ya nyumba, jua kabisa mende huyo hayupo peke yake. Kuna mende wengine pia, hata kama huwaoni, wewe jua wapo. Unapaswa kutumia fursa uliyoipata ya kumuona mende mmoja kuhakikisha unaondoa mende wengine wot. Usiue mende mmoja uliyemuona na kudhani umemaliza tatizo. Hivyo ndivyo (more…)

#SheriaYaLeo (16/366); Hakuna Wito Bora Zaidi Ya Mwingine.

By | November 16, 2021

#SheriaYaLeo (16/366); Hakuna Wito Bora Zaidi Ya Mwingine. Tambua kwamba mchango wako kwenye jamii unaweza kuja kwa namna tofauti tofauti. Siyo lazima uwe mjasiriamali mkubwa, kiongozi mkubwa au mvumbuzi ndiyo uweze kuleta mchango mkubwa kwenye jamii. Unaweza kufanya makubwa ukiwa peke yako au ukiwa ndani ya taasisi kubwa. Muhimu ni (more…)

2511; Hawajui unachojua wewe.

By | November 15, 2021

2511; Hawajui unachojua wewe. Watu wanaweza kukushangaa kwa yake unayofanya. Wanaweza kwenda mbali zaidi na kukukosoa au kukupinga. Lakini wengi wanafanya hivyo bila kujua mengi ambayo wewe unayajua. Kwa kuwa wana taarifa chache na za juu juu tu, ni rahisi kwao kuona unachofanya siyo sawa. Lakini kama wakipata taarifa za (more…)

#SheriaYaLeo (15/366); Acha Kusudi Likuongoze.

By | November 15, 2021

#SheriaYaLeo (15/366); Acha Kusudi Likuongoze. Kitu muhimu ambacho watu wengi wanakikosa kwenye zama tunazoishi sasa ni kusudi kubwa la maisha yao. Kipindi cha nyuma watu walipewa kusudi la maisha na dini au jamii zao. Kwa sababu kipindi hicho dini na jamii zilikuwa na nguvu kubwa ya kuwaamulia watu maisha yao. (more…)