Author Archives: Dr. Makirita Amani

About Dr. Makirita Amani

Dr. Makirita Amani ni daktari wa binadamu, mwandishi, mhamasishaji na mjasiriamali. Dhumuni lake kubwa kwenye maisha ni KUWASAIDA WATU KUBORESHA MAISHA YAO NA KUFIKIA MAFANIKIO MAKUBWA KUPITIA KAZI ANAZOFANYA. Mawasiliano 0717396253 email makirita@kisimachamaarifa.co.tz

2457; Matumizi Ya Teknolojia Mpya.

By | September 22, 2021

2457; Matumizi Ya Teknolojia Mpya. Kila wakati huwa kuna teknolojia mpya ambazo zinavumbuliwa. Teknolojia hizo huwa zina nguvu ya kuleta mabadiliko makubwa na hivyo kuonekana ni fursa nzuri. Watu wengi hukimbizana na teknolojia hizo mwanzoni, ili kuzihodhi wakiona ndiyo namna ya kunufaika nazo. Lakini mwisho wa siku wanaofaidika sana siyo (more…)

2456; Kujaribu.

By | September 21, 2021

2456; Kujaribu. Mbwa huwa hajaribu kubwa mbwa, bali anakuwa mbwa. Kadhalika ukipanda mahindi, mche unapoota haujaribu kuwa mhindi, bali unakuwa. Kila kitu kwenye asili tayari kina uwezo na upekee ndani yake. Kinachopaswa kufanya siyo kujaribu bali kuwa. Hakipaswi kuiga vitu vingine bali kinapaswa kuwa kilivyo. Lakini inapokuja kwetu binadamu, pamoja (more…)

2455; Siyo lazima ujibu.

By | September 20, 2021

2455; Siyo lazima ujibu. Matatizo na changamoto nyingi tunazopitia kwenye maisha, chimbuko lake ni midomo yetu, tunaongea wana na kuongea hovyo. Mtu anaweza kufanya jambo, likakukera au kukuudhi, maneno yanaanza kukutoka ambayo yanazidi kuharibu kuliko kujenga. Mtu anaweza kukujibu vibaya na wewe ukasukumwa kumjibu vibaya zaidi. Maneno ni upepo mtupu, (more…)

2454; Ukitaka sana kitu, unakifukuza.

By | September 19, 2021

2454; Ukitaka sana kitu, unakifukuza. Pale unapokuwa unakitaka sana kitu na kutaka kukipata kwa wakati unaotaka wewe mwenyewe, huwa inakuwa vigumu zaidi kukipata. Utakazana na kulazimisha sana ukipate, utatumia kila aina ya njia. Lakini kadiri unavyohangaika ili kukipata, ndivyo kinakwenda mbali na wewe. Cha kushangaza sasa, pale unapokuwa hakitaki sana (more…)

2453; Ukiwa huna cha kupoteza.

By | September 18, 2021

2453; Ukiwa huna cha kupoteza. Umewahi kugundua kwamba ukiwa na fedha huwa hazikosi matumizi? Na ukiwa huna fedha bado maisha hayasimami? Yaani ukiwa na fedha, utashangaa zinatumika na bado yale mahitaji muhimu uliyonayo yanakuwa hayajaisha. Kadhalika ukiwa huna fedha, hata kama una mahitaji mengi kiasi gani ambayo hujaweza kuyatimiza, bado (more…)

2450; Hakuna Aliyekamilika.

By | September 15, 2021

2450; Hakuna Aliyekamilika. Sisi binadamu tuna changamoto na mapungufu mbalimbali. Hivyo ndivyo asili yetu ilivyo. Kama ilivyo kwamba ndege ni usafiri mzuri na wa haraka, ila ajali yake ni hatari kubwa sana. Inawezekana kabisa kutengeneza ndege ambayo ni salama kwenye ajali, lakini haitaweza kuruka hewani. Ni kanuni ya asili kwamba (more…)

2448; Ukiwa njia panda, chagua kazi zaidi…

By | September 13, 2021

2448; Ukiwa njia panda, chagua kazi zaidi… Pale unapojikuta njia panda, ukiwa hujui uchague kipi kati ya vingi vilivyo mbele yako, mara zote chagua kile kinachotaka kazi zaidi. Najua hili ni kinyume na wengi tunavyofikiri na kuamua. Huwa tunakimbilia kuchagua kile ambacho ni rahisi na hakihitaji kazi zaidi. Na hiyo (more…)