Author Archives: Dr. Makirita Amani

About Dr. Makirita Amani

Dr. Makirita Amani ni daktari wa binadamu, mwandishi, mhamasishaji na mjasiriamali. Dhumuni lake kubwa kwenye maisha ni KUWASAIDA WATU KUBORESHA MAISHA YAO NA KUFIKIA MAFANIKIO MAKUBWA KUPITIA KAZI ANAZOFANYA. Mawasiliano 0717396253 email makirita@kisimachamaarifa.co.tz

2447; Hakuna Kuchelewa.

By | September 12, 2021

2447; Hakuna Kuchelewa. Safari ya mafanikio huwa haina kuchelewa. Wakati wowote ambapo mtu unaamua unayataka mafanikio, ndiyo wakati sahihi kwako kuyafanyia kazi na kuyapata. Wapo ambao huona kwa sababu umri umekwenda na wamechelewa kujitambua kwenye eneo la mafanikio basi hawawezi tena kupata mafanikio makubwa. Hiyo siyo kweli, kama tu unaweza (more…)

2446; Nia njema huishia pabaya…

By | September 11, 2021

2446; Nia njema huishia pabaya… Kila mtu anayefanya jambo lolote lile, huwa anakuwa na sababu za msingi kabisa za kulifanya na huwa analifanya kwa nia njema kabisa. Hata kama kwa nje jambo hilo linaonekana ni la hovyo na la kijinga, sivyo anavyoona mfanyaji. Yeye anakuwa amefikiri na kufanya maamuzi ambayo (more…)

2444; Hakikisha Una Pa Kusimama.

By | September 9, 2021

2444; Hakikisha Una Pa Kusimama. Utegemezi uliopitiliza kwa wengine ndiyo kitu kinachowayumbisha wengi na kuwazuia kupata mafanikio makubwa. Ni kweli unawahitaji sana wengine na ushirikiano wao ni muhimu kwa mafanikio yako. Lakini kama unawategemea wengine kwa kila kitu na huna pa kusimama mwenyewe, unakuwa kwenye hatari kubwa. Unapowategemea wengine kwa (more…)

2443; Unahitaji kufikiri kwa utofauti.

By | September 8, 2021

2443; Unahitaji kufikiri kwa utofauti. Albert Einstein aliwahi kunukuliwa akisema ujinga ni kufanya jambo lile lile, kwa namna ile ile halafu kutegemea kupata matokeo ya tofauti. Unaweza kuona hii ni kauli ambayo haikuhusu, lakini hebu itafakari kwa kina. Kuna maeneo ya maisha yako ambayo umekuwa unapata matokeo yale yale, japo (more…)

2442; Barabara lazima zifagiliwe.

By | September 7, 2021

2442; Barabara lazima zifagiliwe. Pata picha kama hakungekuwa na watu wanaofanya usafi kwenye barabara tunazotumia. Au hakuna watu wanaoondoa takataka kwenye mazingira yetu. Au hakuna watu wanaolima chakula tunachohitaji sana. Kwa hakika maisha yangekuwa magumu, bila ya kujali mtu una fedha kiasi gani. Ninachotaka kusema hapa ni hiki, kila kazi (more…)

2441; Kukata tamaa…

By | September 6, 2021

2441; Kukata tamaa… Kila mmoja wetu huwa anakutana na hali ya kukata tamaa katiks nyakati tofauti tofauti za maisha yake kulingana na kile anachokuwa anapitia. Hali hii ya kukata tamaa haisababishwi na kile ambacho mtu unapitia, bali inasababishwa na namna mtu unatafsiri kile unachopitia. Kuna mtazamo unaokuwa nao kuhusu unachopitia, (more…)

2440; Shabiki wako namba moja…

By | September 5, 2021

2440; Shabiki wako namba moja… Wewe ndiye unayepaswa kuwa shabiki wa kwanza kwako mwenyewe. Unapaswa kujikubali sana na kujishabikia kwenye yale makubwa ambayo unayafanya. Usiwe shabiki wa wengine au wa michezo mbalimbali kabla hujawa shabiki wako mwenyewe. Usifurahie ushindi wa wengine unaowashabikia na kuona kama ni ushindi wako wakati wewe (more…)

2439; Alama kwamba umefanya wewe…

By | September 4, 2021

2439; Alama kwamba umefanya wewe… Kitu chochote kile unachofanya, unapaswa kuacha alama kwamba ni wewe umefanya. Unapaswa kukifanya kwa upekee wa hali ya juu sana, kwa namna ambayo hakuna mwingine anayeweza kukifanya hivyo. Na hilo linawezekana kabisa kama utajitambua wewe mwenyewe na kuchagua kuwa wewe badala ya kuhangaika kuwaiga wengine. (more…)

2438; Pata Pesa Kwanza…

By | September 3, 2021

2438; Pata Pesa Kwanza… Huwa kuna picha huwa inazunguka mtandaoni, ikimnukuu Warren Buffett akisema; pesa siyo kila kitu, ila hakikisha unazo za kutosha kabla hujaongea huo ujinga. Nina hakika Buffett hajawahi kusema maneno ya aina hiyo, ila ujumbe huo umekuwa maarufu kwa sababu umebeba ujumbe mkubwa na muhimu sana kuhusu (more…)