Author Archives: Dr. Makirita Amani

About Dr. Makirita Amani

Dr. Makirita Amani ni daktari wa binadamu, mwandishi, mhamasishaji na mjasiriamali. Dhumuni lake kubwa kwenye maisha ni KUWASAIDA WATU KUBORESHA MAISHA YAO NA KUFIKIA MAFANIKIO MAKUBWA KUPITIA KAZI ANAZOFANYA. Mawasiliano 0717396253 email makirita@kisimachamaarifa.co.tz

2467; Mlango wa sita wa hisia.

By | October 2, 2021

2467; Mlango wa sita wa hisia. Tumefundishwa sana kuhusu milango mitano ya hisia. Macho yanayoona. Pua inayonusa. Ulimi unaoonja. Masikio yanayosikia. Ngozi inayohisi. Hiyo ni milango inayoeleweka kirahisi na ndiyo maana inafundishwa bila tatizo. Kuna mlango wa sita wa hisia ambao umekuwa haueleweki kirahisi jinsi unavyofanya kazi, ndiyo maana umekuwa (more…)

2466; Unawafanyia wengine, kwa ajili yako.

By | October 1, 2021

2466; Unawafanyia wengine, kwa ajili yako. Mambo mengi unayowafanyia wengine kwenye maisha, unayafanya kwa ajili yako mwenyewe. Unawatumia hao wengine kama sababu tu, lakini mhusika mkuu ni wewe. Chochote unachomshauri mtu mwingine, ni ushauri ambao unautoa kwa ajili yako mwenyewe. Haijalishi umeutoa kwa nani na kwa ajili ya nini, huo (more…)

2465; Hudanganywi ila unajidanganya.

By | September 30, 2021

2465; Hudanganywi ila unajidanganya. Huwa tunalalamika kwamba watu wengine wametudanganya kwenye mambo mbalimbali. Wakatufanya tuamini kwa namna fulani ambayo siyo sahihi. Unaweza kuona uko sawa kwenye hilo, lakini ukiangalia kwa undani, utaona wazi haupo sawa. Watu huwa hawakudanganyi, ila umekuwa unajidanganya mwenyewe. Twende taratibu hapa maana inahitaji utulivu na umakini (more…)

2464; Unapokuwa huna pa kuanzia.

By | September 29, 2021

2464; Unapokuwa huna pa kuanzia. Kuna kichekesho kimoja, lakini cha kweli, ambapo kikosi cha jeshi kilikuwa kimezungukwa pande zote na maadui. Wanajeshi wakaenda kwa mkuu wa kikosi kumpa taarifa kwamba wamezingirwa pande zote na adui, walimweleza wakiwa na hofu kubwa kwa sababu hawakujua hata wanawezaje kujiokoa. Mkuu wa kikosi alipopata (more…)

2463; Kwenye muda huo huo.

By | September 28, 2021

2463; Kwenye muda huo huo. Watu wamekuwa wanalalamika hawana muda wa kufanya yale wanayopaswa kufanya ili wafanikiwe. Lakini katika muda huo huo, kuna wengi wanaofanya makubwa na kufanikiwa sana. Nimekuwa najiuliza mara nyingi, nini kinapelekea hili? Inakuwaje kwenye muda huo huo wengine wanafanikiwa na wengine wanashindwa? Nilielewa hilo kwa kina (more…)

2462; Ukiwa chini na ukiwa juu.

By | September 27, 2021

2462; Ukiwa chini na ukiwa juu. Unapokuwa chini, kuwa mtu wa shukrani. Na unapokuwa juu, kuwa mnyenyekevu. Hii ni kanuni muhimu ya maisha ambayo itakuwezesha kufanikiwa na kudumu kwenye mafanikio hayo. Unapokuwa chini, pale mambo yanapokuendea vibaya ni rahisi kulalamika na kulaumu kwa nini hayo yawe hivyo kwako. Lakini malalamiko (more…)

2461; Unachojua kinatosha kuanza.

By | September 26, 2021

2461; Unachojua kinatosha kuanza. Kama kuna kitu chochote unachotaka kufanya, lakini unajiambia bado hujajua kiasi cha kutosha kuanza jua unajidanganya. Kitendo cha kujua unataka kufanya kitu fulani, ni kiashiria kwamba unajua kiasi cha kutosha kuanza. Kama ungekuwa hujui kwa kiasi hicho, usingeweza kupata wazo la kufanya kitu hicho. Ni kweli (more…)

2460; Lazima kuna mtu ataumia.

By | September 25, 2021

2460; Lazima kuna mtu ataumia. Kwenye moja ya vitabu ambavyo nimekuwa narudia kusikiliza mara kwa mara, How To Be A Billionaire, mwandishi anasema ukifanikiwa kutengeneza utajiri wa mabilioni, utakuwa pia umefanikiwa kutengeneza maadui wakubwa. Kwa kifupi ni hakuna namna utaweza kufanikiwa bila ya kuwaumiza baadhi ya watu kwa namna fulani, (more…)

2459; Siku Gani?

By | September 24, 2021

2459; Siku Gani? “Ipo siku yangu na mimi nitafanya makubwa.” Sawa, tunakubaliana na wewe, lakini tuna swali kidogo; “ni siku gani hiyo?” Kama huwezi kutujibu swali hilo, tafadhali usituhangaishe, kama umechagua kujidanganya mwenyewe ni sawa kwako, ila kuchagua kutudanganya na sisi siyo sawa. Siku moja haijawahi kutokea, siku ambayo haijatajwa (more…)