Author Archives: Dr. Makirita Amani

About Dr. Makirita Amani

Dr. Makirita Amani ni daktari wa binadamu, mwandishi, mhamasishaji na mjasiriamali. Dhumuni lake kubwa kwenye maisha ni KUWASAIDA WATU KUBORESHA MAISHA YAO NA KUFIKIA MAFANIKIO MAKUBWA KUPITIA KAZI ANAZOFANYA. Mawasiliano 0717396253 email makirita@kisimachamaarifa.co.tz

2437; Unahangaika na watu wasio sahihi…

By | September 2, 2021

2437; Unahangaika na watu wasio sahihi… Watu ndiyo kazi yetu kubwa kwenye maisha. Tunahitaji kushirikiana na watu mbalimbali kwenye safari yetu ya mafanikio. Watu hawafanani, wana sifa na tabia mbalimbali. Wapo ambao tunaweza kwenda nao vizuri na wakawa na manufaa makubwa kwetu. Lakini pia wapo ambao tunapokuwa nao tunasumbuana sana (more…)

2436; Kuiga mpaka uwe…

By | September 1, 2021

2436; Kuiga mpaka uwe… Huwa kuna kauli maarufu ya Kiingereza inayosema; fake it till you make it. Ikiwa inamaanisha chochote kile unachotaka, unapaswa kukiigiza mpaka kiwe kweli kwenye maisha yako. Na dhana kuu ni kwamba akili yetu ya ndani huwa haiwezi kutofautisha ukweli na maigizo. Yenyewe inachukulia kile mtu anachofanya (more…)

2435; Kukusanya na kutawanya…

By | August 31, 2021

2435; Kukusanya na kutawanya… Kitu kimoja ambacho nazidi kujifunza kwenye eneo la mafanikio ni wanaofanikiwa na wanaoshindwa wote wanaanza na rasilimali zinazolingana. Mwanzoni watu hao hawatofautiani sana kwenye eneo la rasilimali. Kama ni muda wanakuwa nao sawa. Akili pia hawatofautiani sana. Na hata kwenye fedha, wengi huanzia chini wakiwa hawana (more…)

#TAFAKARI YA LEO; KUBADILI MAISHA YAKO, BADILI HADITHI YAKO…

By | August 31, 2021

Hadithi unayijiambia kila siku na kuiamini ndiyo inayojenga maisha yako. Kama unataka kuyabadili maisha yako, anza kwa kuibadili hadithi unayojiambia. Tengeneza hadithi mpya inayoendana na kile unachotaka, jiambie hadithi hiyo mara kwa mara na kuiamini. Jipime jinsi unavyoiishi hadithi yako na endelea kuboresha kadiri unavyokwenda. Kwa kusimama kwenye hadithi yako (more…)

2434; Hadithi unayojilisha na kupima…

By | August 30, 2021

2434; Hadithi unayojilisha na kupima… Kitu pekee kinachotutofautisha sisi binadamu na wanyama wengine kama mbuzi ni hadithi ambazo tunajipa. Na hadithi hizo zinatokana na ubongo wetu wa mbele, ambao ni mkubwa na umeendelezwa ukilinganisha na wa wanyama wengine. Wanyama wengine wanapokea na kuishi katika hali walizozaliwa nazo. Lakini sisi binadamu (more…)

#TAFAKARI YA LEO; ISHI MAISHA YAKO…

By | August 30, 2021

Sisi binadamu kama viumbe wa kijamii, huwa tunajali sana wengine wanatuchukuliaje. Hilo lilikuwa muhimu kipindi cha nyuma, ambapo tuliishi ndani ya kundi lisilozidi watu 150 wanaojuana. Kama kikundi chako kidogo kingekukataa, huo ndiyo ungekuwa mwisho wa maisha yako. Lakini sasa tunaishi ndani ya kundi kubwa la watu na hakuna mwenye (more…)

2433; Kichekesho cha jamii…

By | August 29, 2021

2433; Kichekesho cha jamii… Mchekeshaji mmoja amewahi kusema watu wanatumia fedha ambazo hawana, kununua vitu ambavyo hawavitaki ili kujionyesha kwa watu ambao hawajali. Na mwandishi Morgan Housel kwenye kitabu chake cha psychology of money ameandika kuhusu dhana ya mtu aliye kwenye gari la kifahari. Anasema wengi hununua magari ya kifahari (more…)

#TAFAKARI YA LEO; RAHISI VS SAHIHI…

By | August 29, 2021

Fanya vitu rahisi na utakuwa na maisha magumu. Fanya vitu sahihi na utakuwa na maisha rahisi. Vitu rahisi kufanya siyo sahihi na vitu sahihi kufanya siyo rahisi. Kila unachofanya, jiulize kwanza unakifanya kwa sababu ni rahisi au sahihi? Utajikamata mara nyingi ukifanya vilivyo rahisi wakati vilivyo sahihi vipo mbele yako (more…)

2432; Kila kitu ni rahisi isipokuwa kufanya…

By | August 28, 2021

2432; Kila kitu ni rahisi isipokuwa kufanya… Kuahidi ni rahisi, Kuweka malengo ni rahisi, Kupanga ni rahisi, Kukosoa ni rahisi, Kuomba ushauri ni rahisi, Kushauri ni rahisi, Kulalamika ni rahisi. Kila kitu ni rahisi, isipokuwa kimoja tu, ambacho ni kufanya. Kuweka juhudi katika kufanya kitu, ili kuleta matokeo ya tofauti, (more…)

#TAFAKARI YA LEO; USIPOTEZE KINACHOKUNUFAISHA…

By | August 28, 2021

Sisi binadamu huwa tunazoea vitu haraka, kisha tunavichoka na kutaka kuvibadilisha. Tunapenda vitu vinavyotusisimua na kuibua hisia zetu. Ni katika harakati hizo ndiyo tunajikuta tumeharibu au kupoteza kile kilichokuwa na manufaa kwetu huko nyuma. Unapaswa kuwa makini sana kwenye hili, kwa kuhakikisha unalinda kila ambacho kina manufaa kwako ili usikiharibu (more…)