Author Archives: Dr. Makirita Amani

About Dr. Makirita Amani

Dr. Makirita Amani ni daktari wa binadamu, mwandishi, mhamasishaji na mjasiriamali. Dhumuni lake kubwa kwenye maisha ni KUWASAIDA WATU KUBORESHA MAISHA YAO NA KUFIKIA MAFANIKIO MAKUBWA KUPITIA KAZI ANAZOFANYA. Mawasiliano 0717396253 email makirita@kisimachamaarifa.co.tz

3110; Raha kufanya.

By | July 7, 2023

3110; Raha kufanya. Rafiki yangu mpendwa,Huwa kuna kauli mbili ambazo huwa zinawachanganya watu wengi.Ya kwanza inasema; Fanya kile unachopenda kufanya na fedha zitakufuata zenyewe.Ya pili inasema; Kama unataka mafanikio makubwa usifanye kazi, bali fanya kile unachopenda. Mkanganyiko ambao umekuwa unatokana na kauli hizo ni imani ambayo watu wengi wanayo kwamba (more…)

3109; Tarehe ya mwisho wa matumizi.

By | July 6, 2023

3109; Tarehe ya mwisho wa matumizi. Rafiki yangu mpendwa,Kila kitu huwa kina tarehe ya mwisho wa matumizi yake (expire date).Hiyo ni tarehe ambayo baada ya hapo kitu hicho hakiwezi kutumika tena. Inaanza na maisha yetu wenyewe, huwa yanaanza pale tunapozaliwa na kuisha matumizi pale tunapokufa.Kila mtu anayo tarehe ya mwisho (more…)

3108; Kuepuka ushindani.

By | July 5, 2023

3108; Kuepuka ushindani. Rafiki yangu mpendwa,Ushindani ni moja ya vikwazo vinavyowazuia watu wengi kupiga hatua kwenye maisha yao.Ushindani mkali unawazuia watu wasipige hatua kubwa. Pamoja na changamoto kubwa ya ushindani, bado ni kitu cha mtu kujitakia.Yaani kama mtu anakabiliwa na ushindani, anakuwa amechagua yeye mwenyewe. Huwa wanasema hakuna foleni kwenye (more…)

3107; Kitu pekee kinachokuzuia.

By | July 4, 2023

3107; Kitu pekee kinachokuzuia. Rafiki yangu mpendwa,Ni ukweli usiopingika kwamba ili kupata mafanikio makubwa, lazima uchukue hatua kubwa sana.Hatua ambazo hujawahi kuzichukua na wala hazijazoeleka kwa wale wanaokuzunguka. Wale wote waliofanikiwa sana, huwa wanalijua hilo vizuri na wanalitekeleza. Wanajua hakuna mbadala wa kuchukua hatua kubwa, hivyo wanaanza kufanya hivyo mapema (more…)

3106; Kitu cha kwanza kufanya kila unapoamka asubuhi.

By | July 3, 2023

3106; Kitu cha kwanza kufanya kila unapoamka asubuhi. Rafiki yangu mpendwa,Kwenye zama tunazoishi sasa, zama za teknolojia ambapo simu zetu janja (smartphones) zimeshika sehemu kubwa ya maisha yetu, huwa ndiyo kitu ambacho tunakigusa mara nyingi zaidi. Huwa natania kwamba mtu anaweza kuamka asubuhi, kabla hata hajajua kama anaweza kutembea au (more…)

3105; Anasa za watu wa kawaida.

By | July 2, 2023

3105; Anasa za watu wa kawaida. Rafiki yangu mpendwa,Watu wa kawaida, ambao ndiyo wengi, huwa hawapati mafanikio makubwa kwenye maisha yao.Na sababu kubwa kabisa inayozuia watu hao wa kawaida wasipate mafanikio ni kusumbuliwa na anasa nyingi ambazo zinahamisha sana umakini wao. Watu hao huwa wanaridhika sana haraka na vitu ambavyo (more…)

3104; Ishara moja, maneno matano. LAZIMA.

By | July 1, 2023

3104; Ishara moja, maneno matano. LAZIMA. Rafiki yangu mpendwa,Moja ya malengo makubwa tunayoyafanyia kazi kwenye biashara zetu ni kujenga wateja waaminifu.Wateja waaminifu ni wale wanaorudi tena kununua, wananunua kwa wingi na wanakupa wateja wa rufaa. Huwa inashangaza pale unapoona biashara inakazana kutafuta wateja wapya kila wakati, huku kukiwa hakuna wateja (more…)

3103; Msimamo pekee hautoshi.

By | June 30, 2023

3103; Msimamo pekee hautoshi. Rafiki yangu mpendwa,Tunajua umuhimu wa msimamo kwenye safari yetu ya mafanikio.Hakuna kitu tunaweza kufanya mara moja au mara chache na kikatupa mafanikio makubwa.Mafanikio makubwa yanatokana na kufanya kwa msimamo kwa muda mrefu bila kuacha. Lakini msimamo peke yake hautoshi.Kuwa na msimamo kwenye kitu ambacho siyo sahihi (more…)

3102; Ni kuwa bora, siyo kufurahia tu.

By | June 29, 2023

3102; Ni kuwa bora, siyo kufurahia tu. Rafiki yangu mpendwa,Hakuna kipindi ambapo maarifa ya mafanikio yamekuwa yanapatikana kwa wingi na urahisi. Lakini pia ndiyo wakati ambao watu wanaopata mafanikio makubwa wanayoyataka wamekuwa wachache sana. Ni jambo la kushangaza, iweje maarifa ya mafanikio kupatikana kwa wingi na urahisi, lakini wanaofanikiwa kuwa (more…)