Author Archives: Dr. Makirita Amani

About Dr. Makirita Amani

Dr. Makirita Amani ni daktari wa binadamu, mwandishi, mhamasishaji na mjasiriamali. Dhumuni lake kubwa kwenye maisha ni KUWASAIDA WATU KUBORESHA MAISHA YAO NA KUFIKIA MAFANIKIO MAKUBWA KUPITIA KAZI ANAZOFANYA. Mawasiliano 0717396253 email makirita@kisimachamaarifa.co.tz

3118; Watu wengi wanataka ufanikiwe, mpaka utakapofanikiwa.

By | July 15, 2023

3118; Watu wengi wanataka ufanikiwe, mpaka utakapofanikiwa. Rafiki yangu mpendwa, Unapokuwa na malengo ya mafanikio makubwa, huwa unapata uungwaji mkono na watu walio wengi kwenye maisha yako.Unaposhirikisha malengo na mipango mikubwa unayokuwa nayo, wengi wanafurahia kwa sababu unakuwa unawafanya wakumbuke malengo makubwa ambayo walikuwa nayo pia.Watakutia sana moyo kwamba upambane (more…)

Barua ya XI; Kuhusu tabia za asili.

By | July 14, 2023

Barua ya XI; Kuhusu tabia za asili. Rafiki yangu Mstoa, Watu huwa tuna tabia mbalimbali ambazo tunakuwa nazo.Baadhi ya tabia hizo huwa ni za asili kwetu, yaani tumezaliwa nazo, wakati tabia nyingine huwa tunaziiga. Kuna wakati tabia tunazokuwa nazo zinakuwa kikwazo kwetu na hivyo kutaka kuzibadili.Kwa tabia za kuiga, huwa (more…)

3117; Usife.

By | July 14, 2023

3117; Usife. Rafiki yangu mpendwa,Bilionea Charlie Munger, mshirika wa karibu wa Warren Buffett huwa anaishi kwa kanuni hii; “Ninachotaka kujua ni wapi nikienda nitakufa, ili nisiende hapo.”Anaiita kanuni ya kugeuza, kuanza na matokeo fulani kisha kujiuliza nini kifanyike kwa sasa kuzuia. Munger ana miaka 99 na ni Bilionea, hivyo hiyo (more…)

3116; Kutokuaminika na wengine.

By | July 13, 2023

3116; Kutokuaminika na wengine. Rafiki yangu mpendwa,Watu wengi huwa wanadhani ili waaminike na wengine basi wanapaswa tu kuwa waaminifu.Wanaona kama hawaibi, hawadanganyi au kumdhulumu mtu yeyote basi ni waaminifu. Ni mpaka pale mtu anapokosa kitu anachokitaka sana kutoka kwa wengine ndiyo anagundua kuaminika ni zaidi tu ya kuwa na matendo (more…)

3115; Kufanya na matokeo.

By | July 12, 2023

3115; Kufanya na matokeo. Rafiki yangu mpendwa,Tumejifunza na kuzoea kwamba tunapofanya kitu, tunaona matokeo mara moja.Hivyo inapotokea tumefanya kitu na hatuoni matokeo, basi tunaona tulichofanya siyo sahihi na hivyo tunaacha kukifanya. Hayo ni mazoea mabaya ambayo tumejijengea na ambayo ni kikwazo kwetu kupata mafanikio makubwa. Ukweli muhimu unaopaswa kuujua kuhusu (more…)

3114; Viwango na mipaka.

By | July 11, 2023

3114; Viwango na mipaka. Rafiki yangu mpendwa,Maisha huwa ni magumu, lakini huwa tunayafanya kuwa magumu zaidi kwa kutaka kudhibiti mambo ambayo yapo nje ya uwezo wetu. Moja ya vitu ambavyo huwa tunapenda sana kufanya ni kuwabadili watu.Watu mbalimbali ambao tunachagua kushirikiana nao kwenye maeneo mbalimbali, wanakuwa na tabia ambazo ni (more…)

3113; Una kitu, utafika mbali.

By | July 10, 2023

3113; Una kitu, utafika mbali. Rafiki yangu mpendwa,Leo nataka nikupe maua yako, nikupe sifa kwa vitu ulivyonavyo, ambavyo ukiamua kuvitumia vizuri, utafanya makubwa sana kwenye maisha yako.Ni vitu ambavyo unaweza kuwa unavichukulia kawaida, lakini kama utavipa uzito, utaweza kufikia malengo makubwa uliyonayo. Wewe kuwa hai mpaka sasa ni kitu kikubwa (more…)

3112; Anzia mahali.

By | July 9, 2023

3112; Anzia mahali. Rafiki yangu mpendwa,Kama utasubiri mpaka taa zote za barabarani ziwake kijani ndiyo utoke, kamwe hutatoka nyumbani.Unachopaswa kufanya ni kutoka kisha kufuata taa moja moja kadiri inavyoelekeza, iliyo kijani unapita, nyekundu unasubiri iwake kijani.Lakini hapo unakuwa kwenye mwendo na hivyo inakuwa rahisi kuendelea kuliko ukiwa hujaanza kabisa. Kwa (more…)

3111; Kazi yako kuu.

By | July 8, 2023

3111; Kazi yako kuu. Rafiki yangu mpendwa,Mimi siyo Mkatoliki na wala sifungamani na dini yoyote, lakini kuna ujumbe nimekutana nao mtandaoni kuhusu Wakatoliki na nimeona kuna mengi sana ya kujifunza kwenye hii safari yetu ya mafanikio makubwa. Ujumbe huo, unaeleza kama ifuatavyo; “Ninapenda sana kiwango cha Wakatoliki cha kutokusumbuka. Utakosoa (more…)

Barua ya X; Kuishi maisha yako.

By | July 7, 2023

Barua ya X; Kuishi maisha yako. Rafiki yangu Mstoa, Umekuwa ni wimbo wa zama hizi kila mtu kutaka kuwa huru kuyaishi maisha yake vile anavyotaka mwenyewe.Lakini je ni wangapi wanaoweza kweli kuyaishi maisha yao kwa namna hiyo?Ni wangapi wenye nidhamu ya kuweza kuyaishi maisha yao wenyewe kwa kufuata misingi sahihi? (more…)