Author Archives: Dr. Makirita Amani

About Dr. Makirita Amani

Dr. Makirita Amani ni daktari wa binadamu, mwandishi, mhamasishaji na mjasiriamali. Dhumuni lake kubwa kwenye maisha ni KUWASAIDA WATU KUBORESHA MAISHA YAO NA KUFIKIA MAFANIKIO MAKUBWA KUPITIA KAZI ANAZOFANYA. Mawasiliano 0717396253 email makirita@kisimachamaarifa.co.tz

3040; Raha ya mchezo.

By | April 28, 2023

3040; Raha ya mchezo. Rafiki yangu mpendwa,Watu wengi huwa wanapenda kufuatilia michezo mbalimbali.Japokuwa hakuna mtu anapenda kuona timu anayoshabikia ikifungwa, kama timu hiyo inaweza kushinda mara zote bila ya kusumbuka, mchezo hauwi na raha ya kuangalia. Kadhalika sinema na maigizo mbalimbali.Kama mhusika mkuu hakutani na changamoto mbalimbali kwenye safari yake, (more…)

3039; Gharama ya kulipa.

By | April 27, 2023

3039; Gharama ya kulipa. Rafiki yangu mpendwa,Kila kitu kwenye maisha huwa kina gharama ambayo mtu anapaswa kulipa ili kukipata.Gharama hiyo siyo tu kwenye fedha, bali pia kwenye kazi, muda, nguvu n.k. Thamani ambayo watu wanakipa kitu, inaendana na gharama ambayo wamelipa kukipata.Kama kitu kinapatikana kirahisi, watu wanakipa thamani ndogo na (more…)

3038; Kuamua unachotaka.

By | April 26, 2023

3038; Kuamua unachotaka. Rafiki yangu mpendwa,Hatua ya kwanza muhimu ya kufanikiwa kwenye maisha ni kuamua nini hasa unachotaka.Hayo ni maelezo mafupi na rahisi kueleza, lakini ambayo utekelezaji wake ni mgumu sana. Kuna kutaka na kuna kuamua.Kila mtu kuna vitu vingi anavyokuwa anataka, vitu anavyotamani awe navyo au kuvifikia.Halafu kuna kuamua (more…)

3037; Uwajibikaji haukwepeki.

By | April 25, 2023

3037; Uwajibikaji haukwepeki. Rafiki yangu mpendwa,Mafanikio ya aina yoyote ile kwenye maisha huwa yanaambatana na uwajibikaji.Ni uwajibikaji wa hali ya juu sana ndiyo unaozalisha mafanikio makubwa ambayo watu wanayapata kwenye maisha yao. Mafanikio pia yanategemea sana watu ambao mtu anaambatana nao.Kwa sababu hakuna mtu anayeweza kufanya kila kitu peke yake, (more…)

3036; Ndiyo ni Hapana kubwa.

By | April 24, 2023

3036; Ndiyo ni Hapana kubwa. Rafiki yangu mpendwa,Wakati tupo kwenye msimu wa HAPANA, tukumbushane jambo muhimu sana kuhusu NDIYO na HAPANA. Unaposema HAPANA kwenye kitu kimoja, unakuwa umekikataa kitu hicho kimoja tu.Hilo linakupa fursa ya kuweza kuangalia mambo mengine mazuri yanayoendana na kile unachofanya na kuweza kuyasemea NDIYO.Kwa maana hiyo (more…)

3035; Huwajibiki kumridhisha yeyote.

By | April 23, 2023

3035; Huwajibiki kumridhisha yeyote. Rafiki yangu mpendwa,Moja ya vitu vinavyotuchelewesha kufanikiwa kwenye maisha ni kujipa wajibu mwingi usiotuhusu. Na moja ya wajibu tuliojipa ambao unatutesa bure ni kutaka kumridhisha kila mtu.Huu ni wajibu unaotuchosha na usio na tija yoyote kwetu, kwa sababu hauna mchango kwetu kufikia mafanikio makubwa tunayoyataka. Tumekuzwa (more…)

3034; Fanya kwa ajili yako.

By | April 22, 2023

3034; Fanya kwa ajili yako. Rafiki yangu mpendwa,Huenda umewahi kutumia muda na nguvu zako kufanya kitu kwa ajili ya wengine.Ukitegemea kwamba watakushukuru kwa namna ulivyojitoa.Au watakulipa fadhila kwa uliyowafanyia. Lakini matokeo yanakuwa ni tofauti kabisa.Watu unaokuwa umejitoa kufanya vitu kwa ajili yao hawajali kabisa.Hawakushukuru kwa namna ulivyojitoa.Lakini pia hata pale (more…)

Misingi Mikuu Kumi Ya Falsafa Ya Ustoa.

By | April 21, 2023

Misingi Mikuu Kumi Ya Falsafa Ya Ustoa. Ustoa ni falsafa ya vitendo iliyoanzia Ugiriki ya kale na baadaye kuhamia Roma ya kale.Falsafa hii ilianzishwa na Zeno ambaye alikuwa mfanyabiashara na kwenye moja ya safari zake za kibiashara meli yake iliharibika na kupata hasara kubwa. Ni katika kutafuta namna ya kujiliwaza (more…)

3033; Wasiwe na pengine pa kwenda.

By | April 21, 2023

3033; Wasiwe na pengine pa kwenda. Rafiki yangu mpendwa,Mafanikio makubwa unayoyataka kwenye maisha yako, yatatokana na watu.Unahitaji sana watu ili kuweza kufikia ndoto kubwa ulizonazo.Na kadiri ndoto zako zinavyokuwa kubwa, ndivyo unavyowahitaji watu wengi na kwa muda mrefu. Lakini changamoto moja kubwa kwenye watu ni huwa hawaeleweki. Unaweza kuwapata watu (more…)