Author Archives: Dr. Makirita Amani

About Dr. Makirita Amani

Dr. Makirita Amani ni daktari wa binadamu, mwandishi, mhamasishaji na mjasiriamali. Dhumuni lake kubwa kwenye maisha ni KUWASAIDA WATU KUBORESHA MAISHA YAO NA KUFIKIA MAFANIKIO MAKUBWA KUPITIA KAZI ANAZOFANYA. Mawasiliano 0717396253 email makirita@kisimachamaarifa.co.tz

3031; Muda wa kutosha kwenye kazi.

By | April 19, 2023

3031; Muda wa kutosha kwenye kazi. Rafiki yangu mpendwa,Tupo kwenye msimu wa HAPANA, kipindi cha kusema HAPANA kwa mengine yote isipokuwa kujenga biashara zetu kuu na kufanya uwekezaji. Lengo kuu la kuingia kwenye msimu huu wa HAPANA ni kuondokana na mambo ambayo huwa yanakuwa usumbufu kwetu na kupunguza muda wetu (more…)

3030; Unafanya ambavyo hawafanyi.

By | April 18, 2023

3030; Unafanya ambavyo hawafanyi. Rafiki yangu mpendwa,Imezoeleka kwamba, kama unataka kufanikiwa, angalia yale ambayo waliofanikiwa wanayafanya kisha na wewe uyafanye. Kwamba mafanikio huwa yanaacha alama, kama utaangalia waliyofanya waliofanikiwa na wewe ukayafanya, utafanikiwa sana. Ni kweli kwamba mafanikio huwa yanaacha alama.Lakini kwenye kufanya yale ambayo waliofanikiwa wanayafanya, kuna ugumu mkubwa.Hiyo (more…)

3029; Msimu wa HAPANA.

By | April 17, 2023

3029; Msimu wa HAPANA. Rafiki yangu mpendwa,Hakuna neno moja lenye nguvu kubwa sana kwenye safari yako ya mafanikio kama neno HAPANA.Hapana siyo tu neno, bali ni sentensi inayojitosheleza. Ili uweze kupata mafanikio makubwa kwenye maisha yako na kufika kule unakotaka kufika, lazima useme HAPANA kwa mambo mengi sana. Kusema HAPANA (more…)

3028; Maamuzi ya mtu mmoja.

By | April 16, 2023

3028; Maamuzi ya mtu mmoja. Rafiki yangu mpendwa,Makosa mengi kwenye maisha huwa yanafanyika wakati wa kufanya maamuzi.Na kadiri watu wengi wanavyohusika kwenye kufanya maamuzi, ndivyo nafasi za kufanya makosa zinavyokuwa nyingi. Maamuzi bora ni yale yanayofanywa na mtu mmoja, ambaye ana uelewa wa kina kuhusu kile anachokiamulia.Mtu huyo anaweza kuchukua (more…)

3027; Watu wa aina yako.

By | April 15, 2023

3027; Watu wa aina yako. Rafiki yangu mpendwa,Kuna vitatu muhimu sana nilivyojifunza wakati naanza kwenye hii safari ya kujenga mafanikio makubwa kwenye maisha yako. Kimoja ni kutoka kwa aliyekuwa maandishi na mnenaji Jim Rhon ambaye alisema; maisha yako ni wastani wa maisha ya watu watano wanaokuzunguka. Akimaanisha unakuwa kama wale (more…)

3025; MIMI ni…

By | April 13, 2023

3025; MIMI ni… Rafiki yangu mpendwa,Wakati wa sikukuu ya Pasaka, kuna jumbe nyingi ambazo watu walikuwa wanatumiana.Mtu mmoja alinitumia ujumbe wa picha ambao ulinasa umakini wangu na kunifikirisha kwa kina. Ujumbe huo ni kauli saba za Yesu akisema MIMI NI…Kuna ujumbe mkubwa sana kwenye kujitamkia maneno hayo, kitu ambacho nimeona (more…)

3024; Kazi itakayokulipa vizuri wakati wote.

By | April 12, 2023

3024; Kazi itakayokulipa vizuri wakati wote. Rafiki yangu mpendwa,Ukitaka upotee na kukosa kabisa mafanikio kwenye hizi zama tunazoishi, sikiliza na fanyia kazi kila aina ya ushauri unaopewa na kila mtu. Kumekuwa na ushauri mwingi kinzani ambao umekuwa unatolewa na watu wengi kwenye mambo mbalimbali. Na sehemu kubwa ya ushauri huo (more…)

3023; Tatizo na suluhisho.

By | April 11, 2023

3023; Tatizo na suluhisho. Rafiki yangu mpendwa,Huwa kuna kauli inayosema, ukiwa na nyundo, kila kitu kinaonekana kama msumari ambao utashawishika kuugonga na nyundo hiyo. Hiyo ina maana kwamba unapokuwa na suluhisho fulani ambalo unalikubali na kulipenda sana, ni rahisi kuona kila tatizo linaweza kutatuliwa na suluhisho hilo. Unapokuwa unapenda suluhisho (more…)

3022; Kushindwa kabla ya kuanza.

By | April 10, 2023

3022; Kushindwa kabla ya kuanza. Rafiki yangu mpendwa,Kufanya jambo lolote jipya na kubwa kwenye maisha yako, huwa kunaambatana na hatari ya kushindwa. Hatari ya kushindwa huwa inakuwa kubwa pale mtu unapokuwa unafanya kwa mara ya kwanza.Kukosa uzoefu kunapelekea mtu kufanya makosa mengi yanayomuathiri. Lakini kushindwa huwa kunakuwa ni kwa uhakika, (more…)