Author Archives: Dr. Makirita Amani

About Dr. Makirita Amani

Dr. Makirita Amani ni daktari wa binadamu, mwandishi, mhamasishaji na mjasiriamali. Dhumuni lake kubwa kwenye maisha ni KUWASAIDA WATU KUBORESHA MAISHA YAO NA KUFIKIA MAFANIKIO MAKUBWA KUPITIA KAZI ANAZOFANYA. Mawasiliano 0717396253 email makirita@kisimachamaarifa.co.tz

3021; Haina mjadala.

By | April 9, 2023

3021; Haina mjadala. Rafiki yangu mpendwa,Kwenye maisha yangu sijawahi kusikia mtu anasema amekuwa bize sana kiasi kwamba amekosa muda wa kupumua.Au mtu kusema ametingwa sana kiasi cha kushindwa kula chochote kwa siku nzima. Kuna vitu ambavyo hata iweje lazima uvifanye kwenye kila siku yako.Hata iwe umebanwa kiasi gani, lazima utapumua, (more…)

3020; Nionyeshe orodha yako.

By | April 8, 2023

3020; Nionyeshe orodha yako. Rafiki yangu mpendwa,Hakuna kipindi ambacho binadamu tumevurugwa kama nyakati tunazoishi sasa.Tunaishi kwenye usumbufu mkubwa sana ambao unawinda umakini wetu.Kuna mambo mengi sana ambayo yanaonekana tunapaswa kuyafanya, lakini siyo yote ni muhimu. Njia pekee ya kutoka kwenye mtego huo wa kuwa na mambo mengi ya kufanya lakini (more…)

3019; Kwani namba zinasemaje?

By | April 7, 2023

3019; Kwani namba zinasemaje? Rafiki yangu mpendwa,Unapokuwa na ndoto kubwa unazotaka kuzifikia kwenye maisha yako, utasikia ujinga mwingi sana. Utashauriwa mambo mengi sana unayoweza kufanya ili kufikia ndoto hizo.Lakini mengi katika hayo unayoshauriwa, yanakuwa ni ujinga mtupu. Utashauriwa kutumia njia mbalimbali za mkato, ambazo huishia kuwa njia ndefu na zinazokugharimu (more…)

3018; Ushindi wa kiongozi.

By | April 6, 2023

3018; Ushindi wa kiongozi. Rafiki yangu mpendwa.Ushindi wa kiongozi yeyote yule huwa unapimwa kwa matokeo anayozalisha.Viongozi wote bora huwa wanazalisha matokeo makubwa. Unaweza kuwa kiongozi mwenye huruma, anayejali na maarufu kwa wengi, lakini kama biashara yako itashindwa, hayo yote hayatakuwa na maana. Kama biashara yako itashindwa, hakuna atakayejali wala kusikiliza (more…)

3016; Usiwe wa kawaida.

By | April 4, 2023

3016; Usiwe wa kawaida. Rafiki yangu mpendwa,Kwa chochote unachofanya kwenye maisha yako, usikubali kuwa mtu wa kawaida.Watu wa kawaida huwa wanaweza kuonekana ni wema kwenye jamii, lakini huwa hawapati mafanikio makubwa. Mafanikio makubwa huwa yanapatikana kwa kufanya mambo kwa utofauti na ukubwa kuliko ilivyozoeleka.Mafanikio makubwa ni zao la kwenda kinyume (more…)

3015; Simba na kondoo.

By | April 3, 2023

3015; Simba na kondoo. Rafiki yangu mpendwa,Mtu mmoja amewahi kusema unapaswa kuhofia zaidi kundi la kondoo 100 wanaoongozwa na simba mmoja kuliko unavyohofia kundi la simba 100 wanaoongozwa na kondoo mmoja. Hiyo ni kauli iliyobeba ujumbe mzito sana inapokuja kwenye uongozi na timu kwenye biashara.Ubora na ufanisi wa timu inayoendesha (more…)

3014; Kama hushindwi, unashindwa.

By | April 2, 2023

3014; Kama hushindwi, unashindwa. Rafiki yangu mpendwa,Sisi binadamu huwa tunaepuka sana kushindwa.Hiyo ni kwa sababu tumekuzwa tukiaminishwa kwamba kushindwa ni kubaya.Tumeaminishwa anayeshindwa anakuwa na matatizo fulani. Tangu utotoni, kushindwa kumekuwa kukiadhibiwa kwa namna mbalimbali.Hilo limetujengea hofu kubwa kwenye kushindwa.Na hofu hiyo imepelekea tusiwe tayari kujaribu vitu vipya, kwa kuwa hatutaki (more…)

3013; Muda na biashara.

By | April 1, 2023

3013; Muda na biashara. Rafiki yangu mpendwa,Mtu mmoja aliwahi kunukuliwa akisema, kama umewapenda watu wawili na unatakiwa kubaki na mmoja, unatakiwa kumchagua wa pili, kwa sababu kama ungekuwa unampenda kweli wa kwanza, usingeenda kwa wa pili. Kwa kuhamishia msingi huo kwenye biashara nakwenda kukuambia; kama kuna kitu chochote unachokipa muda (more…)

3012; Kama hakuna tatizo ni tatizo.

By | March 31, 2023

3012; Kama hakuna tatizo ni tatizo. Rafiki yangu mpendwa,Kama unaiendesha biashara yako kwa kasi na mabadiliko tunayoenda nayo, kuna matatizo mengi ambayo utayatengeneza. Mabadiliko yoyote unayofanya, lazima yazalishe matatizo mbalimbali. Kadhalika pale unapokwenda kwa kasi kubwa, lazima ufanye baadhi ya makosa ambayo yanaleta matatizo. Kama unaendesha biashara yako na hakuna (more…)