Category Archives: BIASHARA NA UJASIRIAMALI

BIASHARA LEO; Anza Kuiua Biashara Yako Wewe Mwenyewe….

By | June 18, 2017

Ukweli ni kwamba, watu wamekuwa wanaua biashara zao wao wenyewe, bila ya kujua kama wanafanya hivyo. Na hili linakuwa changamoto kwao kwa sababu wanakuja kustuka mambo yakiwa yameshaharibika sana. Wateja wameshaondoka, hasara imeshakuwa kubwa na hakuna namna ya kuiokoa tena biashara ile. Mimi ninachotaka kukuambia leo ni uanze kuiua biashara (more…)

BIASHARA LEO; Urahisi Wa Biashara Na Thamani Ya Biashara…

By | June 17, 2017

Biashara rahisi kufanya, thamani yake ni ndogo, na biashara ngumu kufanya, thamani yake ni kubwa. Kwa maneno mengine, biashara rahisi kufanya faida yake ni kidogo, na biashara ngumu kufanya faida yake ni kubwa. Watu wengi wamekuwa wakikimbilia kutafuta biashara rahisi kufanya, biashara ambayo haitawapa stress, biashara ambayo wana uhakika wa (more…)

BIASHARA LEO; Vitu Viwili Vinavyojenga Biashara Yenye Mafanikio.

By | June 16, 2017

Biashara zote zenye mafanikio, zinajengwa kwenye vitu viwili vikuu; Bidhaa au huduma nzuri. Wateja wanaojirudia. Unahitaji kuwa na bidhaa au huduma nzuri, siyo nzuri kwa sura, bali nzuri kwa uhitaji wa watu. Kile unachouza lazima kiwe kinatatua tatizo au kutimiza mahitaji ya wateja wako. Kiwe na thamani kwao inayowafanya kuwa (more…)

Njia Tano (05) Bora Za Kutoa Mafunzo Kwa Wafanyakazi Wa Biashara Yako.

By | June 16, 2017

Huwezi kuendesha biashara yenye mafanikio makubwa wewe peke yako. Unahitaji msaada wa watu wengine wengi ambao watafanyia kazi majukumu muhimu kwenye biashara yako. Hivyo kuajiri ni kitu ambacho kila mfanyabiashara akifikirie hata kama biashara ni ndogo kabisa. Lakini pia kuajiri pekee hakutoshi kukuletea mafanikio kwenye biashara yako. Bali unahitaji kutoa (more…)

Jinsi Ya Kumjua Mpumbavu Na Kumwepuka Ili Kupunguza Matatizo Kwenye Maisha Yako.

By | June 7, 2017

Kitu pekee ambacho unaweza kukipata kwa mpumbavu ni matatizo, hakuna la ziada. Maana mpumbavu hufurahia kuleta matatizo kwake mwenyewe na kwa wengine pia. Hivyo ni muhimu sana uweze kumjua mpumbavu na kumwepuka kabisa, na kama kwa bahati mbaya ukamjua wakati umeshaingia ‘anga zake’, basi uweze kujitoa haraka. Kwenye maisha yetu (more…)

BIASHARA LEO; Mteja Mtarajiwa…

By | June 2, 2017

Biashara yako ina wateja ambao ni wale watu wanaonunua kwako sasa. Hawa tayari wanakujua na wanajua ni kipi unachotoa na kinawasaidiaje. Lakini pia biashara yako ina wateja watarajiwa. Hawa ni wale watu ambao bidhaa au huduma unayotoa inawafaa na itawasaidia, ila bado hawajawa wateja wako bado. Zipo sababu nyingi zinazoweza (more…)

NG’ANG’ANA NA KATAA; Njia Pekee Ya Kuweza Kufanya Makubwa Kwenye Zama Hizi Za Usumbufu Wa Hali Ya Juu.

By | May 30, 2017

Hakuna ambaye hapendi kufanya mambo makubwa kwenye maisha yake. Na kuonesha ni namna gani tumejitoa kufanya makubwa, tunapanga kabisa kila tunachotaka kufanya na kuona wapi tunapotaka kufika. Lakini hii ni sehemu rahisi ya kufika tunakotaka, tunaweza kusema ni asilimia moja pekee. Sehemu kubwa, ile asilimia 99, inatokana na juhudi tunazoweka (more…)

Mambo 31 Niliyojifunza Kwenye Miaka 31 Ya Forbes Kufuatilia Mabilionea.

By | May 25, 2017

Jarida la Forbes limejizolea umaarufu kwa utaratibu wake wa kutoa orodha ya mabilionea wa dunia kila mwaka. Mwaka huu 2017 limetoa orodha ya mabilionea ambapo kwa sasa wapo mabilionea 2,043 ambapo ni ongezeko la asilimia 13 kutoka idadi ya mabilionea mwaka 2016 ambao walikuwa 1,810. Utajiri wa mabilionea hao kwa (more…)

Mambo Matano (05) Muhimu Ya Kuzingatia Wakati Wa Kupanga Bei Ya Huduma Au Bidhaa Kwenye Biashara Yako.

By | May 22, 2017

Kama unazalisha bidhaa zako mwenyewe, au unaandaa huduma zako mwenyewe, kupanga bei ni eneo muhimu sana. Tofauti na wale wanaochuuza, yaani kununua kwa jumla na kuuza kwa reja reja, wao wanakuwa na wigo wa bei tayari umeandaliwa. Lakini wewe unayeandaa mwenyewe, unahitaji kuwa makini wakati unapanga bei. Unaweza kuweka bei (more…)

Uongo Huu Unaojiambia Kila Siku, Ni Adui Mkubwa Wa Mafanikio Yako.

By | May 20, 2017

Huwa najifunza mambo mengi sana kupitia watu ambao wanakuja kwangu wakiomba ushauri juu ya changamoto mbalimbali ambazo wanapitia kwenye kazi zao, biashara zao na maisha kwa ujumla. Na ili kuweza kuwashauri vizuri hatua zipi wachukue, huwa napenda kujua ni hatua gani wameshachukua mpaka pale walipofikia sasa. Kwa sababu kukimbilia tu (more…)