Category Archives: BIASHARA NA UJASIRIAMALI

Njia Tano (05) Za Kuongeza Mauzo Kwenye Biashara Yako Unazoweza Kuanza Kuzitumia Mara Moja Na Kufaidika.

By | May 15, 2017

Mauzo ndiyo moyo wa biashara yoyote ile, kwa kuwa mzunguko wa fedha ni damu ya biashara, hivyo kinachosukuma mzunguko wa fedha ni mauzo, kama moyo unavyosukuma damu. Hii ina maana kwamba, kama biashara haiuzi, basi biashara hiyo inaelekea kufa, na hakuna namna ya kuiokoa bila ya kuongeza mauzo. Leo tutakwenda (more…)

Mambo Haya Manne Yanakuzuia Wewe Kufikia Ukuu Kwenye Maisha Yako. Yajue Na Uyaepuke Ili Kufanikiwa.

By | May 11, 2017

Hakuna mtu ambaye hapendi kuwa bora, kila mtu anapenda kufanya mambo makubwa, kuwasaidia wengi, kupata mafanikio na pia kukumbukwa na wengi kwa namna walivyofanya makubwa. Kila mtu ana ukuu ndani yake, ana uwezo mkubwa wa kufanya mambo ya kipekee hapa duniani, mambo ambayo hakuna mwingine awezaye kuyafanya, mambo ambayo dunia (more…)

Sheria Tano Muhimu Za Kufuata Wakati Wa Kuchagua Hisa Za Kununua.

By | May 10, 2017

Hisa ni moja ya aina ya uwekezaji ambapo unaweka fedha yako kwenye makampuni ya umma, fedha inatumika kwenye kuendesha makampuni hayo na baadaye unanufaika kwa thamani ya hisa kuongezeka na/au kupata gawio kutoka kwenye kampuni pale inapotengeneza faida. Uwekezaji kwenye hisa ni moja ya maeneo muhimu ambayo kila mwekezaji anapaswa (more…)

Tabia Za Wajasiriamali Wakubwa Ambazo Huwezi Kuzikuta Kwa Watu Wengi.

By | May 8, 2017

Kama wapo watu tofauti, ambao wanafanya kitu kimoja, na kati yao wachache wakawa wanafanya vizuri kuliko wengine, ni dhahiri kuna tofauti kati yao katika utendaji. Hata kama wanaonekana wanafanya kwa usawa kabisa, ukichunguza kwa ndani, utaona zipo tofauti, hata kwa kuanzia kwenye tabia na mtazamo ambao watu hao wanao katika (more…)

PESA NA BIASHARA; Misingi Mitatu Muhimu Ya Kuifuata Ili Kuwa Na Biashara Yenye Mafanikio.

By | May 1, 2017

Biashara ni sawa na kiumbe hai, na kama viumbe hai vyote vilivyo, huzaliwa na kufa, na ili kukua, basi kiumbe hai lazima kipate matunzo yote muhimu. Biashara inahitaji matunzo muhimu sana ili iweze kukua, na kama itapata matunzo yote muhimu kwa wakati, basi inaweza kuvunja sheria moja ya viumbe hai, (more…)

UKURASA WA 707; Mteja Mgumu Kumpata Kwenye Biashara Yako Ni Huyu…

By | December 7, 2016

Watu wengi wamekuwa wakianzisha biashara, ila pale mapema kabisa wanagundua jambo moja muhimu, hawana wateja wa biashara zao. Wakati wanajipanga kuanza biashara wanaona mafanikio yapo nje nje, wanajua kabisa wakishaanza biashara watapata wateja wengi. Ila wanapoanza biashara, ndipo wanapokutana na ukweli, kwamba biashara zao hazina wateja. Tatizo la biashara kukosa (more…)

UKURASA WA 705; Misingi Mitano Ya Kuanza Na Kuendesha Biashara Yoyote Ile…

By | December 5, 2016

Kila siku ninapowasiliana na watu, hasa wanaoniadikia wakitaka ushauri, wengi wanakuwa wamekwama, wanataka kuanza biashara lakini hawajui waanzie wapi. Wengine wanasema mtaji ndiyo hawana. Wengine tayari wana biashara ila wanashindwa kuzikuza. Visingizio na sababu ni nyingi sana linapokuja swala la biashara. Lakini ukweli ni kwamba misingi ya kuanzisha na kuendesha (more…)

BIASHARA LEO; Fukuza Wateja Hawa…

By | August 31, 2016

Nimekuwa nakuandikia na kukushauri kuhusu biashara kwa muda sasa, nafikiri unashangaa ninapokuambia ufukuze wateja. Kabla hujashangaa, soma kwa makini ili mwisho uweze kufanya maamuzi sahihi ya biashara yako. Tatizo la wafanyabiashara wengi. Wafanyabiashara wengi wamekuwa na tatizo moja, ambalo limekuwa linawasumbua sana na kuwazuia kukuza biashara zao. Tatizo hilo ni (more…)

BIASHARA LEO; Cross-Selling Na Up-Selling, Mbinu Mbili Za Kuongeza Mauzo Bila Kuongeza Wateja.

By | August 29, 2016

Linapokuja swala la kuongeza mauzo ili kuongeza faida kwenye biashara, wafanyabiashara wengi huwa wanaangalia sehemu moja pekee, kuongeza wateja wengi zaidi. Kuongeza wateja ni mbinu muhimu ya kibiashara kwa sababu biashara yako inaweza kuwafikia watu wengi zaidi. Na kadiri unavyokuwa na wateja wengi, ndivyo unavyotengeneza uhuru wa biashara yako. Lakini (more…)

BIASHARA LEO; Hakuna Kitakachotokea Kwenye Biashara Yako Mpaka Ufanye Vitu Hivi Viwili…

By | August 3, 2016

Hakuna kitakachotokea kwenye biashara yako mpaka pale utakapofanya vitu hivi viwili muhimu sana na kwa mfuatano sahihi. Kwanza muuzie mtu kile unachotoa, iwe ni huduma au bidhaa. Pili mtu aridhishwe na kile ulichomuuzia. Hii ndiyo misingi inayobeba biashara yako. Mengine yote unayofanya kwenye biashara kama hayaipeleki biashara kwenye misingi hii (more…)