Category Archives: KURASA ZA MAISHA

Kila siku mpya kwenye maisha yako ni sawa na ukurasa mpya wa kitabu.
Kwa kila siku mpya unachagua ufanye nini na maisha yako.
Kupitia makala hizi za KURASA ZA MAISHA, utajifunza mambo muhimu ya kufanya ili uwe namaisha bora zaidi.
Makala hizi za kurasa zinakujia kila siku.

2310; Njia ya kupunguza msongo…

By | April 28, 2021

2310; Njia ya kupunguza msongo… Chanzo kikuu cha msongo wa mawazo huwa ni kuyaruhusu mawazo yazurure yatakavyo. Unakuwa unafanya kitu kimoja, ila mawazo yako yako kwenye kitu kingine tofauti kabisa. Kwa mawazo yako kuzurura, yanatengeneza kitu kisichokuwepo, wakati kilicho mbele yako hukofanyi vizuri. Kinachotokea ni muda unakuwa umeisha, umejipa hofu (more…)

2309; Vitu vya kushangaza…

By | April 27, 2021

2309; Vitu vya kushangaza… Waliofanikiwa wanajua kuna mengi hawajui na hivyo kuwa tayari kuendelea kujifunza kupitia kila fursa wanayoweza kuitumia. Ambao hawajafanikiwa wanaamini wanajua kila kitu na hawana haja ya kijifunza, na hivyo hawajifunzi. Matajiri wana fedha nyingi, lakini matumizi yao huwa siyo makubwa. Masikini hawana fedha, ila matumizi yao (more…)

2308; Mambo muhimu ya kujikumbusha…

By | April 26, 2021

2308; Mambo muhimu ya kujikumbusha… Katika safari ya mafanikio, unakabiliana na mambo mengi kiasi kwamba usipojikumbusha yale muhimu unaweza kuyasahau na ukajiingiza kwenye wakati mgumu. Hapa kuna mambo muhimu ya kujikumbusha katika safari hii ya mapambano. Usijiwashe moto ili kuwapa joto wengine. Ni muhimu kuwajali wengine na kuweka maslahi yao (more…)

2307; Wanachokulipa ndiyo thamani yako…

By | April 25, 2021

2307; Wanachokulipa ndiyo thamani yako… Ni kawaida kuwasikia watu walioajiriwa wakilalamika kwamba waajiri wao wanawalipa mshajara kidogo, ambao hauendani kabisa na thamani yao. Pia wapo waliojiajiri na walio kwenye biashara ambao wanalalamika kipato au faida wanayoingiza ni ndogo ukilinganisha na thamani yao. Iko hivi rafiki, kama umeajiriwa na mwajiri wako (more…)

2306; Hadhi inaanzia mfukoni…

By | April 24, 2021

2306; Hadhi inaanzia mfukoni… Kuna watu hawana fedha, lakini wakishauriwa hatua za kuchukua ili watoke kwenye hali hiyo ya kutokuwa na fedha huwa wanaleta ubishi. Wanasema hawawezi kuchukua hatua hizo kwa sababu zitashusha hadhi yao. Iko hivi rafiki, kama huna fedha, hakuna njia halali ya kuingiza fedha ambayo siyo ya (more…)

2305; Vitu vinne vinavyoathiri kipato chako.

By | April 23, 2021

2305; Vitu vinne vinavyoathiri kipato chako. Kuna kanuni mbili muhimu sana za kipato ambazo unapaswa kuzizingatia katika safari yako ya utajiri na mafanikio. Kanuni ya kwanza ni unalipwa kulingana na thamani unayozalisha. Kanuni ya pili ni hupaswi kuweks ukomo kwenye kipato chako. Kwa kuzifuata kanuni hizi mbili vizuri, utaweza kuongeza (more…)

2304; Alama Tatu Za Umasikini…

By | April 22, 2021

2304; Alama Tatu Za Umasikini… Kitu kikubwa kinachowatifautisha masikini na matajiri siyo kinachoonekana, bali kisichoonekana. Kwa maana kuwa zile sababu wengi wanafikiri ndiyo zinawatofautisha siyo, bali namna ya kufikiri ndiyo inawatofautisha. Wanavyofikiri matajiri ni tofauti kabisa na wanavyofikiri masikini na hapo ndipo tofauti inapoanzia. Kuna alama kubwa tatu za umasikini (more…)

2303; Kujiunga na kundi, kukimbia kundi…

By | April 21, 2021

2303; Kujiunga na kundi, kukimbia kundi… Binadamu huwa hatupendi kuona tunafanya kitu kwa kulazimishwa. Huwa tunapenda kufanya kile ambacho tumechagua wenyewe. Na hiyo ndiyo sababu kwa nini baadhi ya watu wako tayari kufanya mambo ambayo yana madhara kwao, ili tu kuonesha wamechagua wenyewe. Tukiielewa saikolojia hii ya binadamu, itatusaidia kwenye (more…)

2302; Jumbe Zinazokinzana…

By | April 20, 2021

2302; Jumbe Zinazokinzana… Katika kujifunza na kupata ushauri mbalimbali, unakutana na jumbe za aina nyingi. Kuna baadhi ya jumbe zitakuwa zinakinzana. Mmoja anakuambia kifanya kitu A ni sahihi, mwingine anakuambia kitu A siyo sahihi. Je katika hali kama hiyo unapaswa kuchukua hatua gani? Hapo wengi hukwama, kwa sababu hung’ang’ania jumbe (more…)

2301; Kinachokukasirisha kikutofsutishe…

By | April 19, 2021

2301; Kinachokukasirisha kikutofsutishe… Sheria ya kwanza na muhimi sana kwenye biashara ni kuwa na kitu kinachokutofautisha na wafanyabiashara wengine. Kuwa na kitu au vitu ambavyo wateja wanavipata kwako tu na hawawezi kuvipata sehemu nyingine yoyote. Yaani hata kama bidhaa au huduma yako itaondolewa jina na nembo, bado mteja aweze kuitambua (more…)