Category Archives: KURASA ZA MAISHA

Kila siku mpya kwenye maisha yako ni sawa na ukurasa mpya wa kitabu.
Kwa kila siku mpya unachagua ufanye nini na maisha yako.
Kupitia makala hizi za KURASA ZA MAISHA, utajifunza mambo muhimu ya kufanya ili uwe namaisha bora zaidi.
Makala hizi za kurasa zinakujia kila siku.

2290; Endelea kukaa kimya…

By | April 8, 2021

2290; Endelea kukaa kimya… Kama mtu alitumia mamlaka yake kukukandamiza au kukuumiza na wewe ukachagua kukaa kimya kwa kuyaogopa mamlaka yake, hupaswi kuanza kulalamika pale mtu huyo anapokuwa hayupo au hana tena mamlaka yale aliyotumia kukuumiza nayo. Kuja kusema baadaye kwamba mtu alikuumiza, alikosea au hakuwa anafaa baada ya mtu (more…)

2289; Ulichozaliwa nacho, hupaswi kukiomba…

By | April 7, 2021

2289; Ulichozaliwa nacho, hupaswi kukiomba… Jamii huwa haipendi uwe huru kuwa vile unavyotaka. Na ili kukunyima uhuru wako, inahakikisha inakujengea aina fulani ya utegemezi ambapo utajiona bila jamii hiyo maisha yako hayawezi kwenda. Ukianza na uhuru wenyewe, ulizaliwa ukiwa huru kabisa, lakini mamlaka mbalimbali zinajihamishia uhuru huo na kukufanya uzione (more…)

2288; Watoze watu wakikukatisha kwenye hiki…

By | April 6, 2021

2288; Watoze watu wakikukatisha kwenye hiki… Joe Girard, aliyekuwa muuzaji mkubwa wa magari amewahi kusema kitu anachopenda zaidi ni kulala, hivyo kama mtu anakatisha usingizi wake, lazima awatoze. Kuna kitu kikubwa sana cha kujifunza hapa, kuhusu kuweka vipaumbele kwenye maisha yako. Tumeshajifunza umuhimu wa kufanya kile unachopenda na kuangalia namna (more…)

2287; Katili isiyo katili…

By | April 5, 2021

2287; Katili isiyo katili… Ukimuomba mtu kitu halafu akakataa, haijalishi amekupa sababu gani, unajisikia vibaya. Maana mpaka unachagua kumuomba, ulijua kabisa ipo ndani ya uwezo wake. Hivyo anapokataa inakufanya ufikirie mengi, labda hakupendi, hajali, ana roho mbaya na mengine. Lakini kama wewe ni mkulima ambaye umepanda mazao yako na ukaomba (more…)

2286; Jua ndiyo litakuangaza bure…

By | April 4, 2021

2286; Jua ndiyo litakuangaza bure… Kwenye kazi au biashara unayofanya, kuna watu waliopiga hatua zaidi yako ambao watataka uwafanyie kazi bure. Watu hao watakutega kwa kukuambia kwamba ukifanya kazi hizo wanazokupa, watakusaidia kujulikana na kuwafikia watu wengi (exposure). Wengi kwa kutamani mafanikio ya haraka, huingia kwenye mtego huo na matokeo (more…)

2285; Watu watabaki kuwa watu…

By | April 3, 2021

2285; Watu watabaki kuwa watu… Soma kauli hii; leo naenda kukutana na watu wasio waaminifu, wenye tamaa, wasiojali na watakaonikwaza na kuniumiza. Lakini hilo halitanisumbua kwa namna yoyote, kwa sababu najua ndivyo watu walivyo. Unadhani hiyo kauli ilitolewa mwaka gani? Ni miaka zaidi ya elfu 2 iliyopita na aliyekuwa mtawala (more…)

2284; Hatari za kipumbavu…

By | April 2, 2021

2284; Hatari za kipumbavu… Iko wazi kabisa kwamba huwezi kufanikiwa bila ya kuchukua hatua ambazo ni hatari. Na hiyo ni kwa sababu hizo ni hatua ambazo wengi wanaziepuka hivyo ukizichukua unakuwa huna ushindani mkubwa. Wapo watu kwa kusikia hivyo, hukimbilia kuchukua kila aina ya hatari, kwa sababu penye hatari ndiyo (more…)

2282; Kuwa sahihi ni kukosea…

By | March 31, 2021

2282; Kuwa sahihi ni kukosea… Kabla ya karne ya 21, waliofanikiwa sana ni wale waliogundua mfumo unaofanya kazi, kisha kurudia mfumo huo bila kubadili chochote. Hivyo ndivyo mapinduzi ya kilimo na viwanda yalivyoendeshwa. Na hata mfumo wa elimu ulijengwa kwenye msingi huo, ndiyo maana mtu alipohitimu masomo alitegemewa kuwa ameshajua (more…)

2281; Manne ya kuzingatia kwenye mauzo…

By | March 30, 2021

2281; Manne ya kuzingatia kwenye mauzo… Kila mmoja wetu ni muuzaji. Kuna kitu unauza kwenye maisha yako, kile unachowashawishi watu wakubaliane na wewe. Ili ufanikiwe, lazima uwe muuzaji mzuri, kwa sababu kila unachotaka kwenye maisha yako, kinatoka kwa wengine. Kuna mengi ya kufanya ili kuwa muuzaji mzuri, lakini haya manne (more…)