Category Archives: KURASA ZA MAISHA

Kila siku mpya kwenye maisha yako ni sawa na ukurasa mpya wa kitabu.
Kwa kila siku mpya unachagua ufanye nini na maisha yako.
Kupitia makala hizi za KURASA ZA MAISHA, utajifunza mambo muhimu ya kufanya ili uwe namaisha bora zaidi.
Makala hizi za kurasa zinakujia kila siku.

2530; Mnyoo Mjinga.

By | December 4, 2021

2530; Mnyoo Mjinga. Kwenye baiolojia kuna dhana kwamba mnyoo (parasite) mwenye akili anahakikisha kiumbe anayemtegemea hafi. Hivyo hata kama anamnyonya virutubisho mbalimbali, anahakikisha hachukui kila kitu mpaka kupelekea afe. Hiyo ni kwa sababu kama kiumbe ambaye mnyoo anamtegemea atakufa, basi na yeye atakufa pia. Hivyo tunaweza kusema mnyoo ambao unamuua (more…)

2529; Mrefu halafu mfupi.

By | December 3, 2021

2529; Mrefu halafu mfupi. Kwenye ukurasa uliopita (2528), tumejifunza tamaa ya kutaka vingi kwa pamoja inavyokuwa kikwazo kwa wengi kufanya maamuzi. Watu wanachelewa kufanya maamuzi kwa sababu hawataki kukosa fursa nzuri zinazoweza kujitokeza baadaye na hilo linakuwa kikwazo kwao. Huo ni upande mmoja ambao watu wamekuwa wanatumia kukwepa kufanya maamuzi. (more…)

2528; Kutaka vingi kwa pamoja.

By | December 2, 2021

2528; Kutaka vingi kwa pamoja. Hadithi tulizokuwa tunajifunza utotoni zilikuwa na masomo makubwa sana kuhusu maisha. Lakini kwa bahati mbaya sana tumekuwa hatuzipi uzito na hivyo kufanya makosa ambayo hadithi hizo zilikuwa zinatuasa tuyaepuke. Chukua hadithi ya sungura kualikwa kwenye sherehe mbili. Kwa ulafi wake akapanga asikose vyote. Hivyo akawa (more…)

2527; Kila suluhisho ni tatizo.

By | December 1, 2021

2527; Kila suluhisho ni tatizo. Kwenye maisha huwa tunapitia matatizo na changamoto mbalimbali. Hilo hutusukuna kutafuta suluhisho ili maisha yetu yaweze kwenda vile tunavyotaka. Tunachosahau au ambacho tunakuwa hatujui wakati tunatafuta suluhisho ni kwamba kila suluhisho huwa lina tatizo ndani yake. Ndiyo ni suluhisho la tatizo ambalo unalo, lakini ndani (more…)

2526; Mtego wa mateso.

By | November 30, 2021

2526; Mtego wa mateso. Haya maisha huwa yana mitego ya mateso ambayo usipoijua utaishi maisha ya kuteseka sana. Mitego hii haijaanza sasa, wanafalsafa wa kale waliielewa sana na wakawa na mafunzo ya kuwatahadharisha watu. Kuna mifano mikubwa miwili ya mafunzo ya kale yanayoonyesha mitego hii. Wa kwanza ni Promethus ambaye (more…)

2525; Mbadala Ndiyo Unaokuponza.

By | November 29, 2021

2525; Mbadala Ndiyo Unaokuponza. Kadiri unavyokuwa na machaguo mengi, ndivyo inavyokuwa vigumu kwako kuchukua hatua. Pale unapokuwa na mbadala wa chochote unachofanya, ukikutana na ugumu utakimbilia kwenye mbadala huo. Hiki ni kikwazo kikubwa kwa mafanikio ya wengi, kuwa na mbadala kunawafanya wasikomae na kitu kimoja mpaka wakapata matokeo makubwa. Kujua (more…)

2524; Pesa ziko wapi?

By | November 28, 2021

2524; Pesa ziko wapi? Wahenga walisema, mali bila daftari, hutumika bila habari. Kama hutunzi vizuri kumbukumbu zako za kila senti inayoingia na kutoka, hutajua pesa zako zinapotelea wapi. Utaona tu umeshika pesa nyingi, lakini hujui zimeenda wapi. Na hapo ndipo wengi huamini kuna chuma ulete, hali ya ushirikina ambapo fedha (more…)

2523; Tatizo unataka kusikia unachotaka.

By | November 27, 2021

2523; Tatizo unataka kusikia unachotaka. Zoezi la kutoa na kupokea ushauri limekuwa zoezi lisilo na manufaa kwa wengi wanaoshiriki. Hiyo ni kwa sababu watu wengi wanaoomba ushauri, siyo kama wanataka ushauri kweli, ila wanataka wajue kama maamuzi waliyofanya ni sahihi. Yaani ndani yao wanakuwa tayari wameshafanya maamuzi, ila wanaomba ushauri (more…)

2522; Kama unajua sana, mbona matokeo hayaonyeshi huo ujuaji?

By | November 26, 2021

2522; Kama unajua sana, mbona matokeo hayaonyeshi huo ujuaji? Kwenye safari ya mafanikio, hakuna sumu kubwa kama ujuaji. Sumu hii huanza pale mtu anapoona yale anayofundishwa tayari anayajua. Kwa sababu maarifa na siri za mafanikio ni zile zile, wengi hufika mahali na kuona wameshajua kila kitu, hakuna tena kitu kipya. (more…)

2521; Tofauti inaanzia kwenye kujali.

By | November 25, 2021

2521; Tofauti inaanzia kwenye kujali. Watu wawili, wanaweza kuwa wanafanya kazi au biashara ya aina moja, mmoja akafanikiwa sana na mwingine akashindwa kabisa. Watu wamekuwa wakitafuta sababu za tofauti hiyo, wakiona labda ni bahati, fursa, upendeleo na uwezo tofauti. Yote hayo yanaweza kuchangia, ila kuna kimoja kikubwa ambacho huwa hakipewi (more…)