Category Archives: KURASA ZA MAISHA

Kila siku mpya kwenye maisha yako ni sawa na ukurasa mpya wa kitabu.
Kwa kila siku mpya unachagua ufanye nini na maisha yako.
Kupitia makala hizi za KURASA ZA MAISHA, utajifunza mambo muhimu ya kufanya ili uwe namaisha bora zaidi.
Makala hizi za kurasa zinakujia kila siku.

2480; Ishi ulaumiwe, kufa usifiwe.

By | October 15, 2021

2480; Ishi ulaumiwe, kufa usifiwe. Nikiwa kwenye basi safarini niliona igizo moja la kichekesho, lakini pia lenye funzo kubwa. Palikuwa na bwana mmoja ambaye alikuwa na uwezo mkubwa kwenye mtaa wake kuwazidi wengine. Kila mtu kwenye mtaa wake alipopata shida alienda kumwomba msaada. Na yeye hakuwa mtu wa kukataa, pale (more…)

2479; Kufanya na kuonyesha unafanya.

By | October 14, 2021

2479; Kufanya na kuonyesha unafanya. Kadiri ninavyoendelea kutafakari maisha ya mafanikio, nazidi kuona jinsi nguvu ilivyo rasilimali muhimu. Msisitizo mkubwa sana umekua unawekwa kwenye muda, kwamba una uhaba na kama mtu atashindwa kuudhibiti vizuri basi hawezi kufanya makubwa. Lakini nguvu ndiyo rasilimali ambayo tunapaswa kuwa na udhibiti nayo mkubwa. Kwa (more…)

2478; Njia za mkato kwenye teknolojia.

By | October 13, 2021

2478; Njia za mkato kwenye teknolojia. Njia za mkato kwenye safari ya mafanikio ni mtego, usizipite, maana zitakupoteza zaidi. Lakini kwenye teknolojia, njia za mkato ni njia ya kuokoa muda na nguvu, ili uweze kutumia kwa mambo mengine muhimu. Jana nilienda kwenye steshenari kuchapa nyaraka fulani. Kulihitajika marekebisho kabla ya (more…)

2477; Hakuna nguvu za ziada.

By | October 12, 2021

2477; Hakuna nguvu za ziada. Moja ya kanuni muhimu niliyojifunza kwenye fizikia na ambayo inaendana sana na maisha ya mafanikio ni kuhusu nguvu. Kanuni ya nguvu kwenye fizikia inasema nguvu haiwezi kuzalishwa wala kuharibiwa, bali inaweza kubadilishwa kutoka mfumo mmoja kwenda mwingine. Kwa mfano gari iliyo kwenye mwendo ina nguvu (more…)

2475; Angalia Muda.

By | October 10, 2021

2475; Angalia Muda. Tumekuwa tunaona jinsi watu wanalaghaiwa na kutapeliwa kwenye zama hizi. Kwa kuitwa kwenye fursa mbalimbali ambazo zinawahamasisha kweli kweli na wanaziamini, lakini baadaye wanakuja kugundua wametapeliwa. Nilishakushirikisha njia moja ya kupima kama fursa ni ya kweli au utapeli, ambayo ni kujiuliza kazi unayopaswa kuweka na thamani unayotoa. (more…)

2474; Fanya vichache kwa ubora.

By | October 9, 2021

2474; Fanya vichache kwa ubora. Moja ya sababu za wengi kushindwa kufanya wanayofanya kwa ubora ni kuhangaika na mambo mengi. Watu wanakazana kufanya mambo mengi kwa wakati mmoja, kitu ambacho kinaathiri ufanisi wao. Unapofanya mambo mengi kwa wakati mmoja, unatawanya sana nguvu na umakini wako na kuishia kupata matokeo ya (more…)

2473; Uimara ndani ya udhaifu.

By | October 8, 2021

2473; Uimara ndani ya udhaifu. Tumeshajifunza sana jinsi ambavyo hakuna aliyekamilika. Kwamba kila mmoja wetu ana madhaifu yake. Wengi huwa wanalipokea hilo kwa mtazamo wa kuyaondoa madhaifu yao na ili yasiwe kikwazo. Kinachotokea ni madhaifu yao yanazidi kuwa imara huku uimara wao ukiwa dhaifu. Yaani unapoweka nguvu kuyaondoa madhaifu yako, (more…)

2472; Muda na Umakini…

By | October 7, 2021

2472; Muda na Umakini… Watu wengi wamekuwa wanasingizia muda kama kikwazo kwao kufanya yale yaliyo muhimu. Wanasema hawana muda wa kufanya mambo hayo. Mimi nimekuwa nalikataa hilo, nikisema kila mtu ana muda sawa. Hivyo ambao wanasema hawana muda, wanatafuta tu visingizio na wamekosa vipaumbele kwenye maisha yao. Nimekuwa nawakatalia kabisa (more…)

2471; Watu wanaamini msimamo.

By | October 6, 2021

2471; Watu wanaamini msimamo. Kuahidi kila mtu anaweza na wengi wanafanya hivyo. Kujaribu kufanya kila mtu anaweza na wengi huanza na kuacha. Wanachohitaji watu ili wakuamini ni msimamo wako kwenye kile ulichoahidi. Kama una biashara ambayo umeahidi kitu fulani, lakini mwanzoni huna wateja wengi, ni rahisi kutokutimiza ahadi hiyo, ukijiambia (more…)